Je, Askari akiua ni dhambi kwa Mungu?

Je, Askari akiua ni dhambi kwa Mungu?

Mgiriki MTz

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2019
Posts
330
Reaction score
273
Habari wana jamii intelligence,

Kutokana na kichwa cha uzi nini maoni yako kwamba askari mfano mwanajeshi,polisi akiua mtu pindi awapo katika majukumu yake ya kazi ni dhambi kwa Mungu?

Nimemuuliza kiongozi wangu wa dini naona hana hoja za msingi binafsi Mimi naona ni dhambi kwa sababu kila mtu ana haki ya kuishi.

Nawasilisha.
 
Habari wana jamii intelligence,

Kutokana na kichwa cha uzi nini maoni yako kwamba askari mfano mwanajeshi,polisi akiua mtu pindi awapo katika majukumu yake ya kazi ni dhambi kwa Mungu?

Nimemuuliza kiongozi wangu wa dini naona hana hoja za msingi binafsi Mimi naona ni dhambi kwa sababu kila mtu ana haki ya kuishi.

Nawasilisha.
Inategemea kamuua nani,maana haiwezekani aue tu halafu asipate dhambi,hata sheria za nchi tu kama zikiwa imara zina muhukumu na kama hakuna wale wanaojiita watetezi wa haki za binaadamu bandia,basi askari huyo alitakiwa kula kitanzi kiroho safi kabisa.
Lakini askari yupo vitani,anatetea nchi yake,analinda watu wake dhidi ya maadui,askari huyo ana haki ya kuua hapo dhambi hakuna.
Askari yupo ana pambana na majambazi yenye silaha,ni haki yake kuyaua kiroho safi.
Ila akiua asie na hatia,askari huyo ajiandae kuingia motoni kula mateso na firauni.
 
hakuna dhambi kwangu mimi huchukulia neno dhambi kama makubaliano ya watu ama taasisi fulani kuna baadhi ya jumuia hata kula baadhi ya vyakula ni dhambi na taasisi nyingine ikala na isiwe dhambi hivyo sioni dhambi hapo labda kuvunja sheria juu kila binadamu anahaki ya kuishi jumuiya zilizoko juu zimetoa tamko hilo na sisi tunafuata aaaah kwanza wanatuchanganya tu
 
Cha msingi azingatie sheria kama askari yupo sahihi kisheria na kamuua mhalifu ambaye analazimika kumuua kutokana na mazingira ya tukio basi amfyatue kama mazingira yanamwezesha askari kumkamata kwa njia ya kawaida amkate,


hakuna dhambi tii sheria bila shuruti!
 
Ni sawa na kuuliza je wale askari wa Roma waliomuua Yesu kwa kumgongelea misumari msalabani wana dhambi?
Maana kimazingira walikua wanatekeleza majukumu yao ya kazi kisheria baada ya hakimu (pilato) kuidhinisha hukumu ya kusulubiwa.
 
Inategemea anamuua nani na kwa sababu zipi, kama ni raia asiye na hatia hiyo ni dhambi ila kama ni mhalifu au gaidi mwenye silaha ambaye huenda na yeye akaua raia au askari husika hapo hakuna tatizo akimuua.
 
Ninachojua mkipambana kwa lengo la kuuana, kifo kikitokea, aliyeua na aliyeuawa wote wana dhambi ya mauaji.

Mkipambana kwa lengo la mmoja kuua na mwingine kujihami asiuawe, basi mwenye lengo la kuuwa ndio pekee mwenye dhambi

Mfano 1: Umeingiza mifugo yako kwenye shamba langu, umejiandaa na sime na mkuki kwamba nikitokea tu unaniua, nami nikatokea nikaona mifugo yako inakula mazao yangu, nikaenda kuchukua panga na mshale nikaanza kukusaka nikumalize, hapo sote tuna dhambi ya mauaji.

Mfano 2: Umeingiza mifugo yako kwenye shamba langu, umejiandaa na sime na mkuki kwamba nikitokea tu unaniua, nami nikatokea nikaona mifugo yako inakula mazao yangu, nikaenda kukuripoti kwenye ofisi za serikali, ukakamatwa. Wewe una dhambi ya mauaji.

Mfano 3: Umeingiza mifugo yako kwenye shamba langu kwasababu malisho ya mifugo yameadimika, uko tayari ukikutwa na mwenye shamba ulipe fidia, nami nikatokea nikaona mifugo yako inakula mazao yangu, nikaenda kuchukua panga na mshale nikaanza kukusaka nikumalize, hapo nina dhambi ya mauaji.

So, kwa upande wa askari, pia inaangaliwa nia yake hasa ni ipi, basi.
 
Isaya 2:4. Mungu atasuluhisha mizozo ya mataifa atakata mashauri ya watu wengi.Watu watafua panga za vita kuwa majembe na mikuki yao kuwa miundu ya kupogolea.Taifa halitapigana na taifa lingine wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.
 
Inategemea una toa uhai wa mtu kwa lengo gani.... Askari akimuua adui au jambazi hiyo sio dhambi lakini Askari akimuua mtu kwa Nia ya uonevu au tamaa binafsi hiyo Ni dhambi...

Pia Askari akitumwa kumuua mtu kwa sababu binafsi za kiongozi wake hapo wote walioshiriki watakuwa na dhambi ikiwezekana Hadi na kizazi Chao kitapata dhambi hiyo...

Rejea kisa Cha Daudi na Goliathi, Musa alivyokimbia Misri, pia rejea kisa Cha Kaini na Abel, Na Yule aliyemweka Askari kikosi Cha kwanza ili afe Kisha amtwae mkewe..
 
Habari wana jamii intelligence,

Kutokana na kichwa cha uzi nini maoni yako kwamba askari mfano mwanajeshi,polisi akiua mtu pindi awapo katika majukumu yake ya kazi ni dhambi kwa Mungu?

Nimemuuliza kiongozi wangu wa dini naona hana hoja za msingi binafsi Mimi naona ni dhambi kwa sababu kila mtu ana haki ya kuishi.

Nawasilisha.
Elijah Mtishbi alichinja manabii wa baali zaidi ya 100+, Nabii Musa ameua watuwengi sana.. 😀😀😀
 
Ni dhambi kubwa sana... bora ya askari ana chaguo aue au asiue...

Je wale ambao kazi yake ni kukatisha uhai wa binadamu mwezake baada ya hukumu ya kunyongwa kutolewa... wana mtihani sana...


Cc: mahondaw
 
Habari wana jamii intelligence,

Kutokana na kichwa cha uzi nini maoni yako kwamba askari mfano mwanajeshi,polisi akiua mtu pindi awapo katika majukumu yake ya kazi ni dhambi kwa Mungu?

Nimemuuliza kiongozi wangu wa dini naona hana hoja za msingi binafsi Mimi naona ni dhambi kwa sababu kila mtu ana haki ya kuishi.

Nawasilisha.
Uhai ni uumbaji wa mwenyezi Mungu.. Kuuhitimisha kuna madhara yake labda tu kama ulifanya hivyo kuwaokoa wengine

Jr[emoji769]
 
Back
Top Bottom