Jasusi la kitanzania lilivyowatoka wanajeshi Uganda

Tulipita eneo lililoandikwa Nakulabye na baadae tukaelekea barabara inayoelekea eneo liitwalo Bombo lakini tulipofika eneo la Namirembe, lori likaanza kupunguza mwendo, nikahisi linakaribia kusimama. Niliruka haraka na kuanza kutembea kufuata barabara ya Balintuma hadi kwenye mzunguko wa barabara iliyooneshwa kwa kibao inaelekea Chuo Kikuu cha Makerere.
Naam, NAKULABYE (maana yake Nimekuona). Iko karibu na Kasubi,, makao ya Kabaka (ukiwa kwenye kilima cha Nakulabye, unakuwa unaikabili Ikulu ya Mfalme, ndo maana ya nimekuona Kabaka). Bombo iko karibu na Namirembe (Makao Makuu ya Kanisa Anglikana Uganda). Neno hili lina maanisha HURUMA za MUNGU. Kanisa hili (Cathedral)liko Kusini mwa Chuo Kikuu cha Makelele (kilicho eneo la Wandegeya).....
 
"Tuliamuriwa kutoka nje ya jengo kupitia mlango wa bustanini na majasusi wa shirika la ujasusi la Idi Amin.
Nje ya jengo kulikuwa na bustani nzuri iliyojaa miti midogo midogo na barabara zenye kokoto. Mbele yetu hatua kama 200 hivi iliegeshwa Land Rover.
Koplo Sudi akawa na kiherehere, akatangulia kuifata Landrover hiyo akifuatiwa na Sajini Binda.
Mimi nilikuwa nyuma yao lakini mawazo yangu yalihisi kuna hatari mbele yetu, haiwezekani watuachie kirahisi namna ile.
SAJINI BINDA NA KOPLO SUDI WAUAWA BAADA YA KUISOGELEA LANDROVER
"Wakati akili yangu ikiwaza bila kupata majibu, ghafla nikamwona Koplo Sudi ambaye alikuwa anajitayarisha kuingia ndani ya Landrover hiyo akianguka chini.
Kabla sijamuangalia vizuri, nikasikia Sajini Binda akitoa sauti ya kung'aka na kuanguka chini.
Bila kuzubaa nikaruka na kujiviringisha kama gogo linalobiringika kutoka mlimani.
Niliingia uvunguni mwa Landrover na kusikilizia wakati huo Koplo Sudi na Sajini Binda walikuwa wamelala kando huku damu zikiwavuja kwa wingi.
Utulivu waliouonesha na damu zilivyokuwa zikiwatoka nilijua kuwa wameshakufa.

JASUSI LA KITANZANIA LAWATOROKA WANAJESHI WA UGANDA KININJA

"Sasa milio ya bunduki na risasi kutoboa gari hilo zilisikika vizuri masikioni mwangu lakini gari halikulipuka.
Hii ilidhihirisha kuwa Landrover hiyo iliwekwa hapo kama chambo tu, haikuwa na petroli na labda hata haikuwa na injini.
Kilichonishangaza ni jinsi risasi hizo zilivyonikosa, sijui wapigaji hawakuwa na shabaha au ni Mungu tu.
"Huu ndio mlango wa bustanini, mlango wa mauaji unaotumiwa na wauaji wasioonekana wakiwa na bunduki zisizotoa mlio," nilijisemea kama mwehu kisha kama umeme nilitoka hapo uvunguni na kukimbia kwa kasi kwa mtindo wa zigizaga.
Risasi zilivuma karibu yangu na moja ikanipata begani lakini sikusimama.
Niliacha barabara inayoelekea kwenye mlango ambako kulikuwa na kibanda cha walinzi, nikapinda upande wa kushoto bila kujua ninapoelekea.
Walinzi hao waliponiona nao walianza kunifyatulia risasi ambazo zilitoa sauti ya kutisha lakini Mungu alikwishasema hapana.
Maofisa Usalama wa Taifa wa Idi Amin nao hawakukubali kunikosa, walikuja nyuma yangu kwa kasi sana lakini kwa vile nilishawaacha mbali hawakufanikiwa kunipata.

ARUKA SENG'ENGE ZENYE MIIBA NA KUDANDIA LORI HUKU RISASI ZA WANAJESHI WA ZIKIMKOSA KOSA

"Nilipofika kwenye seng'enge zenye miiba na urefu wa kama mita mbili hivi kwenda juu nikashtukia naruka kama karatasi kwenye upepo na kujikuta naangukia upande wa nje wa eneo hilo la wauaji.
Bila ya kufanya ajizi nikainuka na kutimua mbio huku risasi zikiendelea lakini hazikunipata.
Nilikimbia mbele zaidi nikatokea kwenye barabara kubwa ya lami ambako nililiona lori moja lililobeba mifuko ya saruji likijikongoja.
Niliongeza kasi ya mbio na kulirukia nyuma ambako nilijibwaga juu ya mifuko hiyo ya sementi huku nikitweta.
Nilipotazama nyuma sikuwaona maadui zangu hivyo nikajua wameenda kufuata magari ili wanifate.
Tulipita eneo lililoandikwa Nakulabye na baadae tukaelekea barabara inayoelekea eneo liitwalo Bombo lakini tulipofika eneo la Namirembe, lori likaanza kupunguza mwendo, nikahisi linakaribia kusimama.
Niliruka haraka na kuanza kutembea kufuata barabara ya Balintuma hadi kwenye mzunguko wa barabara iliyooneshwa kwa kibao inaelekea Chuo Kikuu cha Makerere.
Baadhi ya watu walinishangaa kutokana na damu ilivyokuwa ikinitoka lakini mimi nilisonga mbele huku nikiwakwepa polisi na askari wengine waliovaa sare.

AINGIA KANISANI NA KUANGUA KILIO KILICHOMSHITUA PADRE

"Ghafla bila kutarajia nikaona bango kubwa mbele yangu limeandikwa 'Namirembe Cathedral'.
Nilihisi hapo ndipo mahali pekee napoweza kuonewa huruma. Nikaangazo macho huku na huku kuthibitisha hakuna anayenifuata au kuniangalia kisha haraka nikaingia kwenye mlango wa uwa wa ukuta wa kanisa hilo ambako ndani nilikuta ibada ikiendele kukiwa na waumini wapatao hamsini huku padre wa kizungu akiongoza ibada.
Nikatafuta sehemu nzuri ya peke yangu nyuma kabisa na kusikiliza ibada hiyo iliyokuwa ikiendeshwa kwa lugha ya Kiingereza.
Mwisho wa ibada watu wote walitoka nje lakini mimi nikabaki ndani na kupiga magoti nikainamisha kichwa chini na kuanza kububujika machozi kama bomba la maji lililopasuka.
Nililia sana na hatimaye nikalia kwa sauti kubwa.
Kilio changu hakikuwa cha kumuomba Mungu bali maumivu, njaa na uchovu ambao binadamu mwenye afya ya kawaida lazima angezimia.

PADRE AMSAFISHA JERAHA NA KUMTOA RISASI MWILINI

"Baada ya kama nusu saa nikasikia mtu akinisemesha na kunigusa kwa mkono begani kisha akaniinua kichwa.
"Pole sana kijana, umepatwa na nini?" aliniuliza mtu huyo kwa kiingereza.
"Umetoka wapi na umeumia na nini?" aliniuliza.
Nilimuomba kwanza anisaidie chakula na matibabu ya jeraha nililokuwa nalo kisha nitamueleza kilichonisibu.
Alinitoa nje ya kanisa na kunipeleka kwenye jengo moja la ghorofa ambapo alinipa chakula na kunisafisha jeraha ambapo alinitoa risasi moja mwilini".
Nukuu ya jasusi wa Tanzania aliyetekwa nyara na wanajeshi wa Uganda.

MKUU UMETOKA SEHEMU YA 4 UMEENDA SEHEMU YA 6 NAOMBA NIWEKEE SEHEMU YA 5 PLEASE
 
Hadithi nzuri, ya kutunga of course, fiction. Mtunzi amejitahidi kuwianisha na historia, mfano ametaja kwa usahihi kuwa mkuu wa SRB alikuwa Col Farouk Minowa. Lakini amekosea vitu vingine vya kihistoria ambavyo angepatia hii hadithi ingekuwa na uhalisia zaidi. Mifano:
  1. Pesa aliyopewa ya uhamisho kutoka Dar shilingi laki tatu. Mwaka 1978 sh laki tatu ilikuwa pesa nyingi za kutisha. Mwaka huo nilikuwa shule ya msingi darasa la nne, na ninakumbuka kaka yangu alianza kazi mwaka huo alikuja nyumbani akaomba misa ya shukrani kwa kupata kazi yenye mshahara mzuri wa shilingi 750 kwa mwezi. Haiwezekani kwa mwaka huo mtu alipwe fedha za uhamisho ambazo ni sawa na mishahara ya karibu miaka 3! Mtunzi akarekebishe historia hapo.
  2. Mtunzi ametaja mtaa wa Luwum kule Kampala. Mtaa huo ulipewa jina hilo baada ya Iddi Amin kuondoka madarakani, kwa kumuenzi Askofu wa kianglikana Janan Luwum aliyeuawa na Amin. Kwa kuwa hadithi ni ya kipindi cha Amin, mtaa huo haupaswi kutajwa kwa jina hilo, anapaswa afanye utafiti ajue jina lililokuwa likitumika wakati huo.
  3. Matumizi ya simu. Mtunzi anasema huyo mwanamke aliyemrubuni na kwenda naye kwake alipopigiwa simu aliondoka nayo eti akazungumzie mbali. Kifupi mtunzi anataka kutuaminisha kuwa hiyo ilikuwa simu ya kiganjani. Mwaka 1978 simu za kiganjani hazikuwepo, simu zote zilikuwa za mezani, zile za kuzungusha tarakimu.
Licha ya makosa hayo ya kihistoria, mtunzi ana makosa ya kumbukumbu pia. Anatusimulia kuwa huyu mhusika mkuu alipigwa risasi ya bega alipokuwa anawatoroka SRB, eti akatibiwa na padre wiki moja, halafu akawa mzima kabisa hadi anafukuzia mademu, anaoga kwenye bathtub na jeraha lake la risasi begani!
 
Hadithi nzuri, ya kutunga of course, fiction. Mtunzi amejitahidi kuwianisha na historia, mfano ametaja kwa usahihi kuwa mkuu wa SRB alikuwa Col Farouk Minowa. Lakini amekosea vitu vingine vya kihistoria ambavyo angepatia hii hadithi ingekuwa na uhalisia zaidi. Mifano:
  1. Pesa aliyopewa ya uhamisho kutoka Dar shilingi laki tatu. Mwaka 1978 sh laki tatu ilikuwa pesa nyingi za kutisha. Mwaka huo nilikuwa shule ya msingi darasa la nne, na ninakumbuka kaka yangu alianza kazi mwaka huo alikuja nyumbani akaomba misa ya shukrani kwa kupata kazi yenye mshahara mzuri wa shilingi 750 kwa mwezi. Haiwezekani kwa mwaka huo mtu alipwe fedha za uhamisho ambazo ni sawa na mishahara ya karibu miaka 3! Mtunzi akarekebishe historia hapo.
  2. Mtunzi ametaja mtaa wa Luwum kule Kampala. Mtaa huo ulipewa jina hilo baada ya Iddi Amin kuondoka madarakani, kwa kumuenzi Askofu wa kianglikana Janan Luwum aliyeuawa na Amin. Kwa kuwa hadithi ni ya kipindi cha Amin, mtaa huo haupaswi kutajwa kwa jina hilo, anapaswa afanye utafiti ajue jina lililokuwa likitumika wakati huo.
  3. Matumizi ya simu. Mtunzi anasema huyo mwanamke aliyemrubuni na kwenda naye kwake alipopigiwa simu aliondoka nayo eti akazungumzie mbali. Kifupi mtunzi anataka kutuaminisha kuwa hiyo ilikuwa simu ya kiganjani. Mwaka 1978 simu za kiganjani hazikuwepo, simu zote zilikuwa za mezani, zile za kuzungusha tarakimu.
Licha ya makosa hayo ya kihistoria, mtunzi ana makosa ya kumbukumbu pia. Anatusimulia kuwa huyu mhusika mkuu alipigwa risasi ya bega alipokuwa anawatoroka SRB, eti akatibiwa na padre wiki moja, halafu akawa mzima kabisa hadi anafukuzia mademu, anaoga kwenye bathtub na jeraha lake la risasi begani!
Nilinunua copy moja ya kitabu cha huyu jamaa nahisi hela yangu haikutendewa haki.
 
Hadithi nzuri, ya kutunga of course, fiction. Mtunzi amejitahidi kuwianisha na historia, mfano ametaja kwa usahihi kuwa mkuu wa SRB alikuwa Col Farouk Minowa. Lakini amekosea vitu vingine vya kihistoria ambavyo angepatia hii hadithi ingekuwa na uhalisia zaidi. Mifano:
  1. Pesa aliyopewa ya uhamisho kutoka Dar shilingi laki tatu. Mwaka 1978 sh laki tatu ilikuwa pesa nyingi za kutisha. Mwaka huo nilikuwa shule ya msingi darasa la nne, na ninakumbuka kaka yangu alianza kazi mwaka huo alikuja nyumbani akaomba misa ya shukrani kwa kupata kazi yenye mshahara mzuri wa shilingi 750 kwa mwezi. Haiwezekani kwa mwaka huo mtu alipwe fedha za uhamisho ambazo ni sawa na mishahara ya karibu miaka 3! Mtunzi akarekebishe historia hapo.
  2. Mtunzi ametaja mtaa wa Luwum kule Kampala. Mtaa huo ulipewa jina hilo baada ya Iddi Amin kuondoka madarakani, kwa kumuenzi Askofu wa kianglikana Janan Luwum aliyeuawa na Amin. Kwa kuwa hadithi ni ya kipindi cha Amin, mtaa huo haupaswi kutajwa kwa jina hilo, anapaswa afanye utafiti ajue jina lililokuwa likitumika wakati huo.
  3. Matumizi ya simu. Mtunzi anasema huyo mwanamke aliyemrubuni na kwenda naye kwake alipopigiwa simu aliondoka nayo eti akazungumzie mbali. Kifupi mtunzi anataka kutuaminisha kuwa hiyo ilikuwa simu ya kiganjani. Mwaka 1978 simu za kiganjani hazikuwepo, simu zote zilikuwa za mezani, zile za kuzungusha tarakimu.
Licha ya makosa hayo ya kihistoria, mtunzi ana makosa ya kumbukumbu pia. Anatusimulia kuwa huyu mhusika mkuu alipigwa risasi ya bega alipokuwa anawatoroka SRB, eti akatibiwa na padre wiki moja, halafu akawa mzima kabisa hadi anafukuzia mademu, anaoga kwenye bathtub na jeraha lake la risasi begani!
Good observation mkuu, nami nilikuwa nahubiri nikimaliza nicorment hivyohivyo, pia maji ya chupa mwaka 78 hayakuwepo
 
Back
Top Bottom