January Makamba naamini amepata cha kujifunza

January Makamba naamini amepata cha kujifunza

Kwenye Maisha kimbelembele hakifai kabisa, kujikweza sana karibu na wakubwa sio tiketi ya kupata wadhifa wa juu.

Nampa pole January Makamba, asubirie Uwaziri tu lakini sio Uwaziri Mkuu.

Wahenga wasema, kukaa karibu na Mahakama sio kujua sheria.
Acha ushamba wewe Dictator Musolin. Kwani yeye aliwaambia kuwa anataka huo uwaziri mkuu? ?
Nyie ndio mlikuwa mnamtajataja na kina mwakyembe, Sospeter Muongo nk. Je ulisikia wao wakijitaja??
 
Magufuli hata yeye anaona huyu kiherehere cha dogo kinaweza kuwehusha nchi
 
Binadamu ndivyo tulivyo, mtu akifanya kazi yake eti kajipendekeza, January ana malengo yake na wala siyo uwaziri mkuu,,, acha kuanzisha mada za kiumbea na zisizo na msingi kwa nchi yetu
Kazi ipi moja unayoikumbuka na manufaa kwa Taifa??!!!
 
Acha majungu ww....Makamba ni president in the making....mliwekewa front kwenye kampeni kama strategy ya kuvutia vijana na pia mumzoee kwenye mambo makubwa ya kichama....ataingia kwa cc ya ccm, atapewa muda wa kukomaa na kuiva and finally mtaletewa kama mgombea urais...
 
Huyu dogo hafai kuwa hata mkuu wa wilaya sembuse uwazili achilia mbali w/mkuu na huo ubunge sijui ameupata kwa misingi gani.
 
ila hao hao wahenga walisema ukikaa karibu na waridi na wewe utanukia uwaridi. ongera Kijana Makamba January utakuwa waziri wa mambo ya nje ya nchi
 
Acha ushamba wewe Dictator Musolin. Kwani yeye aliwaambia kuwa anataka huo uwaziri mkuu? ?
Nyie ndio mlikuwa mnamtajataja na kina mwakyembe, Sospeter Muongo nk. Je ulisikia wao wakijitaja??
Poleni sana ndugu jamaa na marafiki wa hao wanaotajwatajwa nasikia muko wengi kweli hapo Dodoma mukisubiri jamaa zenu wapewe vyeo.
 
Kwenye Maisha kimbelembele hakifai kabisa, kujikweza sana karibu na wakubwa sio tiketi ya kupata wadhifa wa juu.

Nampa pole January Makamba, asubirie Uwaziri tu lakini sio Uwaziri Mkuu.

Wahenga wasema, kukaa karibu na Mahakama sio kujua sheria.

January anakujikweza sana. Nadhani nguvu ya baba yake kisiasa inambeba na anaitumia vilivyo. Uwaziri atapata
 
kishaandaliwa uwaziri wa mambo ya nje na miaka kumi ijayo ndo atakuja kuwa mgombea wa uraisi!!! kila kitu kwenye siasa kimeshapangwa kabla....
Hakuna aijuae kesho hata membe aliandaliwa kiko wapi leo. Jipe moyo
 
Kwenye Maisha kimbelembele hakifai kabisa, kujikweza sana karibu na wakubwa sio tiketi ya kupata wadhifa wa juu.

Nampa pole January Makamba, asubirie Uwaziri tu lakini sio Uwaziri Mkuu.

Wahenga wasema, kukaa karibu na Mahakama sio kujua sheria.

Mnaongea sana wabongo. Kijana wawatu kafanya kazi kwa mahaba na chama chake,,,uwaziri mkuu mmezusha nyinyi
 
Makamba hafai kuwa hata waziri. Magufuli akiwatosa yeye pamoja na riz watz watazidi kumwamini na kumuona hatoi vyeo kishkaji
 
Historia haikosei ni wazir mkuu mmoja tu tena wa Tanganyika ndiye aliweza kua rais wa JMT. Hivyo Makamba kukosa uwaziri mkuu ilipangwa ili aje kupitishwa na ccm 2025 kama mgombea urais wao.
 
kishaandaliwa uwaziri wa mambo ya nje na miaka kumi ijayo ndo atakuja kuwa mgombea wa uraisi!!! kila kitu kwenye siasa kimeshapangwa kabla....

Japo siipendi CCM ila ndio ukweli wenyewe, watu wepesi sana kusahau kuwa siasa ni mipango,Makamba hakuwa na uwezo wa kuwa PM kwa sasa hata kwenye mawazo yangu binafsi hakuwa kwenye list.
 
Back
Top Bottom