January Makamba amenitapeli kisiasa na CCM yao. Mungu anaishi anaona

Deogratius Nalimi Kisandu
Chief Chairman elect ACA expected.
27 Jan 2017.[/QUOTE]
Chief Chairman ERECT!! kwikwikwi

Kijana umejivua nguo
 
Huyu jamaa mimi nimesema kwenye uzi mmoja hivi,alikuja kutoka huko Lushoto enzi hizo tuko chuo ndo tumeianzisha CHASO na tayari tumeshaizindua katika mkutano uliofanyika ktk viwanja vya Makuburi na kuhutubiwa na Dr.Slaa, Kisandu alipokuja akasema hata wao walikuwa na wazo kama hilo la kuanzisha umoja kama huo hivyo yeye ndo anapaswa awe mwenyekiti wa CHASO maana ana mikakati mingi kichwani na akalazimisha kweli kweli.Tangu siku ile nikajua jamaa kumkichwa kuna bonge la rift valley!
 
Hapa ndio nyie mnaojiita wanasiasa huwa mnanishangaza. Hivi hasa wewe ndugu unaamini au kusimamia nini kwenye siasa? Wewe hasa ni mfuasi wa itikadi ipi na nini kinakusukuma kuwa mwanasiasa?
 
Wewe utakuwa mfano kwa wachumia tumbo wote wanaokubali kulaghaiwa kutoka upinzani na kujiunga na CCM kwa ahadi za vyeo na ujinga mwingine.

Ukome.
 
Hakika la kwako sio jipya kwenye medani ya siasa kwani Politics is not pure Mathematics. Achana na political interests utapoteza kila kitu hakuna ulingo mbaya wa mapambano kama siasa itafikia wakati utapoteza heshima yako hata kwa wanao uliowazaa mwenyewe. Huenda wewe ukajiona mjanja kama Kirikou lakini unatakiwa ujue kuwa No where is Safe.

Cha ajabu zaidi kuhusu huyo adui unayepambana naye yuko kwenye kila chama unachokijua wewe na hata hicho unachokianzisha tayari adui yako yuko humo tayari.

To humbly advice you Oldman! Achana na siasa, drop political interests wholly.

Hata Mlema aliwahi kuitwa shujaa lakini leo hakuna anayemuheshimu wala anayekumbuka kuwa aliwahi kuwa bora kuliko Sokoine wakati fulani mpaka watoto wadogo walizaliwa wakaitwa jina lake.

POLITICIANS ARE DEVILS IN A HUMAN SKIN. THEY MOVE TOWARDS ANY DIRECTION OF THEIR INTERESTS
 
Haya ndiyo malipo ya wasaliti na wanafiki, mimi natamani wakufanyizie zaidi ya hapo. Kule SA watu wa namna yako dawa yao ilikuwa ni kufa bila huruma. Unajua kitendo chako cha kwenda kujipeleka Lushoto eti unarejea ccm kilivyowaumiza waja wa Mungu. YAKUPATA NA KUZIDI.
JANUARY MAKAMBA AMENITAPELI KISIASA NA CCM YAO.

Mwaka 2012 CCM walianza kunifatafata sana kwa kunibembeleza nitoke Chadema niende CCM, nilipata shida sana hasa nilipojikuta nakuwa MTU wa kuwekewa vikwazo Mara kwa Mara kisa sijaafiki kujiunga CCM.

Kila mbinu zilitumika, nakumbuka mpaka aliyekuwa mgombea mwenzangu wa ubunge 2010 Mh. Shekifu yeye akaniambia jitathimini kwanza ili usije kujuta kuliko kuja CCM kwa kushinikizwa. Wakaona sasa wamtumie Majid Mwanga mkuu wa wilaya ya Lushoto wakati Huo ambaye sasa ni DC Bagamoyo. Kiukweli walipandikiza chuki chama nilichokuwa kukawa na migogoro sana, kiasi kwamba hata nilipowaambia mnadanganywa na CCM hawakunielewa kabisa.

Niliamua kuondoka na kwenda NCCR Mageuzi, kitu ambacho CCM walipaniki sana na wengine walikuwa wakinipigia simu kuwa watanifata hukohuko. Mara nikashangaa tena nikiwa Nccr Mageuzi kukaanza kupandikizwa chuki ambazo hazina msingi wowote.

Mwaka 2014 wakavuruga mipango yangu ya kimaisha wakitumia baadhi ya matajiri vijana na makatibu WA CCM wilaya. Hapa Mwanza akawa anatumika DC aliyekuwepo kupandikiza chuki kila eneo kwa kutumia dhamana ya cheo. Niliumia sana kwa kuwa ukweli WA yote yanayoendelea naujua ila sina MTU WA kunitetea, nikajikuta nimebaki peke yangu. Hapo ndipo January Makamba, DC Majid Mwanga, DC Mpyesa aliyekuwa kahama, DC Komisaga na Katibu WA CCM Bw. Loti. HAWA ndio wakaanza kunipigia simu zisizo isha za kuwa ni bora nijiunge CCM ili niwe na Amani. Kwakuwa nilikuwa tayari nimewekewa vikwazo na kila nikitamka kuwa Niko Detention watu walipotoshwa na Mimi kuendelea kuumia huku wakitumia baadhi ya viongozi WA dini kupotosha ukweli.

Ikawa mwaka 2014 Mwigulu Nchemba anakuja Mwanza kama Naibu katibu Mkuu, nikamwambia Januari Makamba basi niingilie hapa Mwanza ili Mwigulu anipokee lakini Januari akaniambia Mwigulu ni mbabaishaji atakupotezea, naye DC Mpyesa akaniambia usipokelewe na HAWA mawaziri, wewe usubiri mpaka Mh Kinana katibu Mkuu WA chama.

Basi Kinana mwezi septemba 2014 akawa na ziara MKOA WA Tanga. DC Majid Mwanga akanitumia Nauli ili niende Lushoto kupokelewa na Kinana kutokana na hadhi ya vyeo nilivyopitia kichama upinzani. Na Januari akanitia moyo sana. Nilifunga safari kutoka Mwanza mpaka Lushoto na mkutano ulifanyika kata ya MLOLA ambapo Kinana na Nape Nnauye walinipokea hadharani. Wakuu wote WA wilaya za MKOA WA Tanga walikuwepo kwenye hiyo ziara akiwemo mkuu WA MKOA WA kipindi kile. Tulifanya ziara pamoja baaada ya mapokezi.

Na hapo baada ya zoezi Kuisha la ziara MKOA WA Tanga ndipo nikarejea Mwanza.

Huku DC Komisaga akawa analalamika yeye na RC mulongo kuwa kwanini nimeenda kupokelewa Lushoto, na hivyo Mwanza yote ikanuia kuwa watanitesa mpaka nijute kujiungia CCM Lushoto. Kwa kweli nakiri hadharani CCM wamenitesa sana na wamenifilisi sana na wameniharibia mambo yangu mengi sana. Ikafikia hatua wakawa wanatumia wazazi wenzangu ili wafanikiwe kuharibu maisha yangu. Wakatumia watumishi wenzangu kutoa taarifa za uongo.

CCM imenifedhehesha mpaka nimekuwa kama chokoraa. Nalipotaka kugombea ubunge jimbo la kahama wakawa wanakimbia ofisi, na hata nilipotangaza kugombea Uspika WA bunge Ndipo napo wakanipotezea hasa wakiogopa nitapita.

CCM Mwanza na CCM Lushoto wakaungana na kuanza kutoa taarifa za uongo kuhusu Mimi Deogratius Kisandu. January Makamba akiwa nyuma ya mchezo wote huku nikiwa nimemwandikia kitabu "January Makamba hadhina ya vijana Tanzania" kupitia kampuni yangu ya Teachers and Students Forums Tanzania.

Mpaka Leo CCM na baadhi ya waandamizi Serikalini wamenijaribu kama lipoyoyo lao huku wakitumia mawazo yangu kuendesha nchi.

Leo wanajisifia tumekaweza, lakini mwaka hautaisha CCM itabaki mabua tu.

Mh. Rais nachelea kusema kuwa unafanya kazi na watu wadanganyifu.

Sisi tumeamua kuanzisha chama kipya cha Siasa cha Arena for Correcting Africa Tanzania (ACA) ili tuifundishe CCM kuacha kupotosha.

Ninalia CCM walivyokuwa wameijipanga mpaka kugawana watoto wangu kama nikifa. Wakawa chonganisha mpaka ndugu zangu. Hakika CCM ikifa tutaitupa ziwa Tanganyika iwe chakula cha mamba. Wamekanyanga pabaya.

Imekula kwenu.

Deogratius Nalimi Kisandu
Chief Chairman elect ACA expected.
27 Jan 2017.
 
A rolling stone gathers no moss,and he who goes to bed while his anus is itching,wakes up with smelly fingers,my brother take care
Unamtisha nani pimbi wewe, ameshasema ccm imemfanya chizi sasa Unaongea nini tena utumbo mtupu, nyie ndo muwe makini maana tumewachoka kabisa na hata Mungu hawataki na li avatar lako hilo unadhani sifa.
 
Dada yetu kapata bwana kiazi aisew, duuuu! Cc. Chakaza , MANI
Ni aibu kuwa hata na shemeji wa aina hii. Ushauri wa mpwa Elli ni wa kiungwana sana hata mie nimewahi kumwambia hivyo huyu jamaa. Kutafuta tiba kabla hali haijawa mbaya zaidi. Ni kweli wengi walioko ccm wanahitaji tiba ya akili lakini "shemeji" kazidi.
 
Back
Top Bottom