PreGE2025 Janeth Rithe: Wanawake msimchague tena Rais Samia, haoni dira mbele yake

PreGE2025 Janeth Rithe: Wanawake msimchague tena Rais Samia, haoni dira mbele yake

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Sio kwamba huyu ndio kachanganyikiwa?

By the way ni lini wanawake wakachaguana? Wanaume ndio tutamchagua na hivyo bibi amekazidi uzuri basi ndio kubinua midomo kutazidi 😁😁
Alikuws Diwani wetu hapa Kunduchi enzi za mbunge Ritha Mlaki 😁😁🇹🇿
 
Mwenyekiti wa Ngome ya Wanawake Taifa kupitia chama cha ACT Wazalendo, Janeth Rithe, ametaka Wanawake nchini kutomchagua tena Rais Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi ujao, akidai kuwa kiongozi huyo mkimuangalia "amechanganyikiwa".

Pia, Soma: Polisi wavamia Ofisi za ACT Wazalendo kumkamata Janeth Rithe kwa agizo la ZCO

Kauli hiyo ameitoa akihutubia kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Ubungo, tarehe 18 Juni 2025

"Ndugu zangu Wana Ubungo na Watanzania kwa ujumla, Nchi yetu imejaa na Majonzi na Masikitiko mengi na hata ukituona tunavyotembea wote tumejawa na majonzi na masikitiko"

"Haki yetu ya msingi inaporwa kila baada ya Uchaguzi toka mwaka 2020, lakini wanao-sababisha mambo haya yatokee ama uporwaji huu wa Uchaguzi ni CCM na dola la CCM"

"Sasa tunakwenda kwenye Uchaguzi mwezi wa 10, naomba Wanawake wa Tanzania, kila Mwanamke popote alipo ajue kwamba anajukumu la kupiga Kura lakini pia anajukumu la kulinda."

Tukubaliane kama mnapenda siasa basi ziwe fair kwa wote sio mmoja anaruhusiwa kuwararua wenzie yeye hataki kuguswa.

mraruane kwa hoja sie wananchi tunawasikiliza na tutaamua kwenye sanduku.
 
Watu waliojitambulisha kuwa ni Askari Polisi, wamevamia ofisi za ACT Wazalendo, zilizopo maeneo ya Magomeni jijini Dar, kumsaka Mwenyekiti wa Ngome ya Wanawake Janeth Rithe wakidai anahitajika kwa mahojiano maalumu kuhusu hotuba aliyoitoa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Manzese jumatano June 28, 2025. Watu hao wamesema Janeth anatuhumiwa kwa kudai kuwa Rais amechanganyikiwa.!
 
Huyu kwa ufupi anasema "NO REFORMS NO ELECTION.


Na anasema Samia ni chizi. Kwa kauli hii, huyu sasa ndiyo mhaini.
Kusema mwenzake anaonekana kachanganyikiwa ndio unaona ni mhaini...hii mentality ndio inatupaka waTanzania wengi matope.Kama wewe humwoni Mh Rais katika hali hiyo ,una Haki ya kusema kuwa Mh Rais hajachanganyikiwa na utakuwa hujavunja Sheria yoyote.
 
Amos Makala wa CCM anasema kuwa chama flani inayo mpango wa kununua virusi kwa ajili ya kudhuru waTanzania hivyo alileta taharuki. Amos Makala hakuchuliwa hatua yoyote kama kuitwa au kukamatwa na kuhojiwa ili awasilishe ushahidi.

Leo mwingine kusema mgombea flani amechanganyikwa asichanguliwe tayari polisi amefika.
Polisi kwani mlienda kumkamata Amos Makala mkakatazwa? Mnajisiakiaje?
 
Mimi niliona hii kitu zamani kwenye ndoto lakini!

Nasisitiza ni ndoto tu, labda ni maharagwe niliyokula usiku, mm sijui.

Tusubiri
 
Naunga hoja mkono.
Sema mr.price a.k.a zito atakua kakwazika MNO. Yy ni CCM B.
KAZI ni kipimo cha utu
 
Back
Top Bottom