Jana nimeng'atwa na nyoka mguuni!

Jana nimeng'atwa na nyoka mguuni!

maelezo ya PDF na field ni tofauti kabisa.

kijijini inapigwa yowe nyumba ya jirani tu watu wanakusanyika dk 2 tu na wanasutana nani kachelewa ili adhabu zihusike. ukizubaa unapewa kesi.

kicheche au siafu wanavamia kuku au mwizi anakaba mbuzi na kunyonga au anamkunjia kwenye gunia mzima mzima. ukisikia sauti ya mfugo kuomba msaada ukiwa usingizini, unakurupuka kama umekoswa koswa na risasi. lini utakumbuka kombati na boots!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Akhsante sana mkuu kwa ushauri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabisa kabisa mkuu, hata kama watakuwa wanakupiga vita namna gani lakini tafuta wa kuelewana nao miongoni mwao iwapo itashindikana kwa wote.

Sent using Jamii Forums mobile app
Miaka mingi ya nyuma nilikuwa ninaishi maeneo ambayo sasa tunayaita 'uswahilini' lakini enzi zile tulikuwa tunasema 'kwa wenyeji' Hapo jirani yetu mzee mmoja wa kihaya alinunua nyumba akawa anaishi pamoja na familia yake.

Tabia zake zilikuwa akitoka kwenye biashara zake basi huenda msikitini na akitoka huko anarudi kwake hivyo hakuwa na maingiliano sana na wenyeji.

Mzee huyu alipewa majina mengi tu ambayo kwa kweli hayakuwa mazuri.
Bahati mbaya alifariki ghafla na baadhi ya jirani walikwenda msibani[ kwani naye alikuwa anafanya hivyo pia]. Ikatokea kuna bibi mmoja jirani ya nyumba ya marehemu alilia kama vile amefiwa na mwanawe na katika udadisi ikagundulika kuwa yule mzee alikuwa ndiye anamsaidia yule bibi pamoja na wajukuu zake ambao wote walifiwa na wazazi wao.

Kumbe marehemu ndiye aliyekuwa msaada wa hali na mali kwa ile familia bila ya wengine kufahamu. Mwisho wa siku wengi tu jirani ilibidi wainamishe vichwa vyao kwa kujuta kumnanga marehemu kuwa anaringa sana.'TENDA WEMA NENDA ZAKO'
 
Miaka mingi ya nyuma nilikuwa ninaishi maeneo ambayo sasa tunayaita 'uswahilini' lakini enzi zile tulikuwa tunasema 'kwa wenyeji' Hapo jirani yetu mzee mmoja wa kihaya alinunua nyumba akawa anaishi pamoja na familia yake.
Tabia zake zilikuwa akitoka kwenye biashara zake basi huenda msikitini na akitoka huko anarudi kwake hivyo hakuwa na maingiliano sana na wenyeji.
Mzee huyu alipewa majina mengi tu ambayo kwa kweli hayakuwa mazuri.
Bahati mbaya alifariki ghafla na baadhi ya jirani walikwenda msibani[ kwani naye alikuwa anafanya hivyo pia]. Ikatokea kuna bibi mmoja jirani ya nyumba ya marehemu alilia kama vile amefiwa na mwanawe na katika udadisi ikagundulika kuwa yule mzee alikuwa ndiye anamsaidia yule bibi pamoja na wajukuu zake ambao wote walifiwa na wazazi wao.
Kumbe marehemu ndiye aliyekuwa msaada wa hali na mali kwa ile familia bila ya wengine kufahamu. Mwisho wa siku wengi tu jirani ilibidi wainamishe vichwa vyao kwa kujuta kumnanga marehemu kuwa anaringa sana.'TENDA WEMA NENDA ZAKO'
Waswahili tuna tabu sana, mimi pia yalinikuta kuonekana naringa kisa nikipita nimefunga vioo mitaani! Wanataka usalimie kila nyumba kama unatembea kwa miguu, ila nilipowasoma nikaenda nao sawa ķuwanyenyekea wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waswahili tuna tabu sana, mimi pia yalinikuta kuonekana naringa kisa nikipita nimefunga vioo mitaani! Wanataka usalimie kila nyumba kama unatembea kwa miguu, ila nilipowasoma nikaenda nao sawa ķuwanyenyekea wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
'When in Rome do as the Romans do'
 
Mkuu hongera umezunguka Sana kutunga story tumeshajua kumbe una Gari!!!!!
Nyumbani kwetu sikukuta gari wala pesa ila ndani ya miaka 27 nilishakuwa na gari langu mwenyewe, na hii ilichangiwa sana na kupenda michezo ya magari na marafiki zangu wengi walikuwa na sports car ziwe zao au za nyumbani kwao.
Nilijituma tu na kuwekeza na hapo nilikuwa naishi nyumba ya kupangisha na nilibadili sana magari kwa mtindo wa kuuza na kununua kufuata fashion na ilifika wakati nikawa na matatu uwani na hapo waswahili wakaanza kelele kuwa nina magari naishi nyumba ya kupanga ndipo nikaangusha mjengo, umeelewa?
Magari ni vitu vidogo sana na vinajadilika msiogope kujadili, sasa hivi umri umekwenda nina familia sioni tena gari ni jambo la ajabu kama awali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari

Waswahili wanasema hujafa hujaumbika, lakini pia wanasema usimdharau mtu....naam haya jana niliyathibitisha katika maisha yangu.

Nilifanikiwa kukamilisha kibanda pembeni ya mji ndipo ninapoishi na sina muda mrefu sana tangu nihamie hapo, kama ilivyo sehemu kama hizo nikaona nianzishe mifugo hivyo nikawa nao kadhaa.

Jana usiku nilisikia mbuzi na kuku wanajipiga piga katika mabanda yao hali ambayo si ya kawaida, kuangalia saa ni saa nane usiku nikahisi huenda ni mbwa ninaemfuga anawafanyia tabu hivyo nikatoka na kwenda kucheki, kufika nikakuta mlango wao umefunga kama kawaida na mbwa wala hana mishe nao yupo pembeni kabisa akidumisha ulinzi.

Nikazunguka nyuma ya banda eneo lenye wavu na huko kuna giza taa haifiki, mara ghafla kufumba na kufumbua kuna kitu kikanipiga mguuni! Nikamulika tochi ya simu nakuta kidole cha mguu kinavuja damu nyeusi na kwa mbali nyoka mkubwa akitoweka!

Awali niliishiwa nguvu kutokana na presha ya tukio hilo na kuwaza kuwa hiki ni kifo lakini nikaamsha wenzangu (walikuwa wanawake na watoto tu kwani kulikuwa na shughuli za kifamilia mjini hivyo ninaoishi nao walikwenda huko) wakanipa ujasiri na wazo la kuufunga mguu ili sumu isipande.

Nilikwenda kwa jirani ambae ni mzee wa makamo mwenye familia yake, akaniambia mwanangu tuwahi hospital tusipoteze muda maana hatujui nyoka huyo limit ya kuua kulingana na sumu yake.

Niliendesha gari kama mwendawazimu saa tisa tukawa mbele ya geti la hospital, niliwahiwa kupigwa sindano ya kuondoa sumu maana hali yangu ilianza kuwa tete na kisha wakasafisha sehemu husika na kuyatoa meno, pia wameshangaa nimefikaje umbali wote huo kulinganisha na tatizo husika....nikapewa dawa kadhaa pia na kuruhusiwa. Nimeamka naendelea vema na nakanyaga kama kawaida Alhamdulillah.

Kwa nini nimesema hujafa hujaumbika? Kwa sababu mpaka usiku nakwenda kulala nilikuwa mzima wa afya hivyo sikujua kuwa linaweza kunitokea jambo la kuhatarisha uhai wangu usiku huo.

Kwa nini nimesema usimdharau mtu?
Kwa sababu wengi wanapokua na visenti, usafiri au kibanda chenye angalau katika eneo husika haswa wakiwa wageni, huwadharau wenyeji au hata kuchagua watu wa kujenga nao mazoea, tazama nimesaidiwa na mzee nilimchukulia kama baba tangu nahamia pale...mzee ambae hupata riziki zake kwa kutumia baiskeli na panga kufanikisha kubeba mizigo ya kuni porini na kwenda kuuza mjini.

Dunia si yetu hatujui siku wala saa

Sent using Jamii Forums mobile app
katika vitu nilivyojaliwa na mungu ni uwezo wa kuua nyoka,hata awe mkubwa vipi akishaingia kwenye 18 zangu hawezi kuwa salama abadan pole sana.
 
Vuta picha huna gari sasa na nyoka ni black mamba mzee tungekuwa tumekuzika
Huyu nyoka anaonekana wa kawaida kwa sababu hakuwadhulu hata mifugo ile we ulienda ukamkanyaga au alikuwa akijihami pia na yeye akakung'ata na kwa uwoga wake akasepa zake akakimbia
Kuanzia SAA NNE mpka SAA Tisa ndio unafika hospital huyu nyoka hakuwa na sumu Kali
Ingekuwa aina ya nyoka wenye sumu Kali usingefika mda huo wote hata kama uliufunga mguu
Ungekosa nguvu au kuzimia au kufa kabisa
Kuisha na watu ni jambo zuri
Kilicho kuokoa mzee ni gari na sio kitu kingine ndio maana ulivyofika hospital hali yako ilikuwa ishaanza kubadilika kuwahi kwako ndio pona yako

Fyeka vicha vya kalibu choma moto fuga wanyama ambao ni adui wa nyoka una watoto ukiona nyoka mmoja jua wapo wengi huwa wanaishi kimakundi watakusumbua na kukuletea madhara makubwa ukizalau safisha eneo lako mkuu
TAHADHARI KABLA YA HATARI
hao watoto wanacheza nje usiku akiingia ndani na kashajua una mifugo ataludi tena Leo kwenye kidole kesho shingoni au kichwani

Sent using Jamii Forums mobile app
Akhsante sana mkuu kwa ushauri mzuri, siyo saa nne ni saa nane.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mie siku nahamia makazi yangu mapya nilihakikisha hamna wadudu wowote kama nyoka, ng'e, tandu na ujinga ujinga mwingine niliimarisha usafi ndani na mita mbili nje ya ukuta ambako majirani bado hawajaendeleza. Pia uwa napiga fumigation kila miezi sita ile kubwa kabisa. Ila kwa maajabu ya muumba juzi nimekuta nyoka wa kijani kajilaza tulii juu ya mpapai na nilikuwa naenda kuchuma papai. Tulimuua
Akhsante sana mkuu kwa maelezo mazuri, nitafuata njia zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom