Nilikuwa napitia pitia mitandaoni nikakutana na kitu ambacho kikanifanya niandike kitu hapa Usiku wa Manane
Mdau mmoja anasema hakupenda kabisa baba yake amtembelee shuleni kwako,kisa eti baba yake ana MVI, lakini siku moja alikuja mzazi ambaye hana miguu pale shuleni kwao. Baada ya kumuona mtu yule akamuona baba yake ana afadhali sana,basi kuanzia siku hiyo akawa anapenda baba aje pale shuleni
Hizi ndio akili za watoto wetu,kumbe sometime wapo watoto wapuuzi wachache wako ashamed na wazazi wao kwa vitu vya ajabu kabisa
Lakini kwenye maoni ya wadau kuna watoto ambao wako proud na wazazi wao haijalishi wako na hali gani au wako na muonekano gani,wewe msomaji wangu sijui uko kundi gani,hope haupo kama yule mpuuzi wa kwanza
Siku zote kuwa proud na wazazi wako haijalishi ni maskini au matajiri, wazima au vilema,wamesoma au hawajasoma,kumbuka huwezi kuwabadilisha wazazi wako,hao ni wako na jivunie kuwa nao hapa duniani.