Jamii imempora mwanamke nafasi yake

Sasa unashauri wa kike wakizaliwa wasipelekwe shule wasubiri ndoa ama?.

What is your solution?.
Tatizo tumeliona
Sululisho ni elimu kutumika katika natumizi yake sahihi(kujenga jamii sio kubomoa)

Mwanamke anayetumia elimu yake kama ngao ya kushindana na jinsia pinzani huyo yuko miseducated na wala elimu yake haina msaada kijamii.

Watoto wa kike kumpelekwa shule ni haki yao ya msingi sana, halafu hapa wengi huwa mnanielewaga hivi eti sijui kwanini.
 
Asante mkuu
 
Dhambi ya kujitenga haita kuacha salama
Kama ulifunzwa kujitegemea ni vema ila tambua kutegemezana ni vema zaidi.
Mi nadhani mada hii haipo kwa ajili yako bali kwa wale wenye nia ya kua na taasisi imara ya familia
 
Mnaenda kwny extremes ambazo smtimes haziapply kwa jinsia zote
Kuna baadhi ya kazi hazifiki huko


Mbona wapo wanaume wapishi?.
Ni kweli wako wanaume wapishi, wahudumu wa mahoteli n.k. Maana ya hili ni kuwa mwanamume anaweza kufanya kazi zote, nyepesi na ngumu. Lakini mwanamk kuna kazi ambazo zimekuwa specific kwa mwanamume kwani haziwezi, mfano ni huo ukuli. Sijawahi ona mwanamke akindesha guta, kumbuka hii ni mifano tu. Hoja ya msingi ni kuwa yako majukumu maalum kwa mwanamke na yako yamhusuyo mwanamume, hivyo sio sawa kusema kuna usawa wa kimajukumu bali usawa uliopo ni wa kiroho mbele ya Mungu.

Pia niongezee kuwa, mwanamke kupika nyumbani hakumaanishi kuwa mwanamume hawezi, bali ni mgawanyo wa majukumu ambao hufundishwa mtoto na kukua nao. Mwanamume ana majukumu yake yampasayo pia ambayo hufundishwa, tofauti ni kuwa wanawake wameyakimbia majukumu yao kwa kigezo cha haki sawa na kudandia ya wanaume ingawa asili yao inawakataa.
 
Mkuu, wapinzani wengi wametekwa na elimu mpya, hawayaoni maisha katika uhalisia wake. Wacha wapinge lakini ukweli utasimama tu.
Nikwel mkuu katika andiko langu nimeeleza namna ambavyo kizazi kimetengenezwa kutokuwa na maadili
Walichokifanya wakamtoa mwanamke katika nafasi yake
Basi watoto wanakuwa hawana maadili yoyote
Mwisho wa siki tunapata kizazi kibovu
Ndio maana now days hata mwanamke kuolewa ni shida sana sababu tayari mwanaume hawez oa kila mwanamke aliye mbele yake
Yaani sijui tutaamka lini
 
Kwenye ndoa lolote linaweza kutokea, mnaweza mkaachana, au mwenzako akafariki, so kuwa na insurance ni muhimu, utakuwa naive sana kutojiweka kujitegemea kisa upo kwenye ndoa
 
Dhambi ya kujitenga haita kuacha salama
Kama ulifunzwa kujitegemea ni vema ila tambua kutegemezana ni vema zaidi.
Mi nadhani mada hii haipo kwa ajili yako bali kwa wale wenye nia ya kua na taasisi imara ya familia
aisee kwa karne hii mtu utakuwa naive sana kutojiandaa ukidai utaenda kuwa kwenye ndoa, hiyo ndoa ikifeli itakuaje? ndoa hazivunjiki? mwenza wako hawezi kufa? so utaacha kujifunza kufanya kazi kisa unaenda kuolewa?
 
Muda wa kazi unaisha saa 9, wengine wanaweza kuchelewa kidogo, muda wa watoto kutoka kwenye masomo pia ni saa 9, bado wikiend mpo wote nyumbani, so ni suala la kuamua unatumiaje muda wako tu, kuwa na familia ama kufanya mambo mengine. Mtoto kutaka jambo sio lazima apitie kwa mama,inategemea na jambo lenyewe, kuna mambo mengine anataka kwa mama kisha anapitia kwa baba, anafanya vice versa. Sema sasa kama baba hatumii muda na watoto, wanaweza wakawa wanamuogopa hata kufanya maongezi nae, ndio case unayomaanisha nadhani
 
Tunajua na kuheshimu, mama zetu waliyatenda haya, hawakutulea kwa mafundisho ya feminists bali kwa kufuata maagizo ya Mwenyezi Mungu. Tunajivunia hao na kujisikia fahari kulelewa na mama wa aina yao.

Pole,mtoto anahitaji mapenzi ya baba na mama,

bond husaidia mtoto ajifunze social skills.

..mtoto aweze kuinteract na both men and women#

,sasa nyie mliolelewa mama akiwa 'kijakazi' na baba akiwa na Authoritarian Personality

huwa mna difficulties ikija relationship na wanawake……

..sitashangaa nyie watu mkiwa bado singles au mahusiano yenu yana walakini..lol...

kupiga kelele wanawake wasome na wafanye kazi sio u feminist..

These are demands put by our environment...

simply mtu mmoja hawezi kuprovide kila kitu

inabidi tusaidiane,

sasa kusaidiana huko kusiishie kwenye bills peke yake

na majukumu ya nyumbani pia...

nyie mliolelewa kwenye familia mnazodai hazikua za kifeminist..

mtapata tabu sana.

simply wanawake 'mliojijengea' picha vichwani mwenu..hawa exist in this modern world...

mnawatafuta 'mama' zenu katika relationship zenu..??

hamjui zama zimechange??

No wonder mnakuja na topics wanawake wamepokwa na jamii...

Wanawake wapo,ila mnasearch in the wrong fields...

Due to changes in the environment, our ancestors had to move from one place to the other...

Demands put by our environment,means both of us need to work..

ni hivyooo
 
Safi kabisa Naina.
 
Kwenye ndoa lolote linaweza kutokea, mnaweza mkaachana, au mwenzako akafariki, so kuwa na insurance ni muhimu, utakuwa naive sana kutojiweka kujitegemea kisa upo kwenye ndoa
Maana yake usiingie kwenye ndoa kama hujui ndoa ni nini. Utakuwa naive zaidi kuingia kwenye ndoa mguu mmoja nje mmoja ndani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…