Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,842
- 10,765
Wakuu niwatakieni weekend njema na yenye amani tele. Leo nitaandika kifupi tu kwani wengi wamekuwa wakilalamika mada ziwapo ndefu. Tuendelee na mada:
Mwanamke na mwanamume wameumbwa tofauti kwa malengo tofauti. Utofauti huo haufanyi mmoja awe inferior kwa mwenzake bali wawe umoja ili kutimiliza malengo ya uwepo wao duniani ambayo lengo kuu ni kuendeleza kizazi (procreation). Nasema wameumbwa tofauti kwa malengo tofauti kwa sababu zifuatazo:
Maisha ya kijamii
Mfumo wa maisha wa mwanamke umetofautiana kwa kiasi kikubwa na mwanamume. Mwanamke amepewa maisha ya kuhusiana na jamii inayomzunguka, ndio maana utaona wanawake wanakuwa na makundi mtaani, kwamba huyu ni rafiki yangu wa karibu huyu sio. Wanakutana kupeana simulizi za kuhusu maisha ya wengine, nani kapigwa na mume, nani hajui kuvaa, nani kanyang'anya mchumba wa mwingine n.k. Kama huamini fuatilia aina ya maongezi ya wanawake wote bila kujali elimu zao. Hili si baya hata kidogo, ndivyo walivyoumbwa. Mwanamke ni kiumbe anayestahili kuwa kwenye mazingiri ya nyumbani kwake kwa muda mwingi zaidi, ni mlezi.
Mwanamume kwa upande wake ameumbiwa maisha ya kutangatanga. Maongezi yao mengi ni kuhusu nani kapataje utajiri, nani kamtapeli mwingine, nani kavusha mzigo nje ya nchi n.k. Mwanamume ni mtafutaji, kwa ajili ya mke na watoto, tena kwa ajili ya wazazi. Mwanamume ni mlezi wa jamii kwa ujumla wake na ndio maana akili yake imeumbwa kufikiri namna ya kupata mali kwa ajili ya familia. Hivi umewahi kujiuliza ni kwa nini hatuna majambazi wanawake?
Uumbaji
Mwanamke na mwanamume hushiriki uumbaji kwa kuunganisha mbegu na yai. Kwa sababu mwanamke sio mtafutaji kiasili, yeye amewekewa mfuko wa uzazi na mfumo wa uleaji wa mtoto mpaka awapo mtu mzima. Mwanamume hajapewa mfumo huo ili awe mtafutaji, amepewa kuwa na nguvu zake mwaka mzima apate kumtunza mke na familia. Kila mfumo uliwekwa kwa kusudi lake.
Jinsi jamii ilivyopora nafasi ya mwanamke
Mapinduzi ya wanawake kuingia kwenye majukumu ya kufanya kazi yalianza wakati wa vita kuu ya pili ya dunia. Hapa kuna hoja nyingi mno lakini siongelei kwa sasa kwa kuogopa kuifanya thread kuwa ndefu. Lakini niseme tu, tuchunguze mfumo wa elimu sasa na kabla.
Zamani mtoto wa kike alipewa elimu yenye ubora wa hali ya juu, iliyomjenga vema kutambua majukumu yake. Shule yao kuu ilikuwa ni wazazi wake ambao aliumia muda mwingi kuwa nao nyumbani. Elimu hii ilimfanya kuwa mwanamke bora aliyejitambua nafasi yake na majukumu yake pia. Mwanamke ni mlazi wa familia, hivyo elimu ililenga kumjengea uwezo kwenye eneo hilo.
Kwa mtoto wa kiume elimu yake iliendana na majukumu yake pia, utafutaji. Kwa kuwa kiasili mwanamume ni mtafutaji, jamii ilijikita kumpatia elimu itakayomwezesha kutafuta mali ili kumudu majukumu ya kumtunza mke na watoto. Ndio maana zamani mtoto wa kiume alipewa nafasi kubwa kusoma elimu ya kizungu (mashuleni na vyuoni). Wapi mambo yalipobadilika?
Pale dunia ilipobadili mfumo na kuanza kuwajengea mtazamo wanawake na jamii kwa ujumla kuwa mwanamke anastahili kuwa na kipato chake, asiwe tegemezi kwa mume (hoja inayoondoa kabisa maana ya ndoa na majukumu yaliyomo humo), ndoa zikatazamwa kama gereza la mwanamke. Kwamba mwanamke anapoingia kwenye ndoa kwa mtazamo wa zamani ananyimwa uhuru wa kujitafutia kipato chake mwenyewe. Ndipo likaja swala la elimu.
Mwanamke akatakiwa kupatiwa elimu sawa na mwanamume, mambo ya haki sawa. Hili lilikuwa jambo jema kwa kulitazama kwa juu juu, lakini ukiangalia kwa undani, mwanamke kupatiwa elimu ya utafutaji ni kumwondoa kwenye nafasi yake kama mke. Elimu iliyolenga kutafuta mali tangu awali ilimlenga mtafutaji, mwanamume. Sasa badala ya dunia kuleta elimu inayolenga kuboresha nafasi ya mwanamke, ikaleta elimu inayolenga kumfanya mwanamke awe sawa na mwanamume. Mwanamke hawezi kuwa sawa na mwanamume na ndio maana kinachotokea ni kuigiza kuwa kama mwanamume.
Wanawake wamekuwa wakiishi maisha ya uigizaji, na hii imewafanya kutokujitambua, kutokujua thamani yao na nafasi yao katika jamii. Jamii imemshusha hadhi mwanamke na kumfanya kama mwanamume, isipokuwa tu ameshindwa kabisa kuenenda kwa jinsia hiyo. Matokeo yake wanawake wamegeuzwa kuwa chombo cha starehe, matangazo ya biashara. Mwanamke ambaye zamani alikuwa akiishi na jamii iliyomzunguka huku akijiweka kumliwaza mume, sasa anaishi na jamii za mbali kwa sababu ni mfanya biashara ama mfanyakazi. Zamani alivaa kuteka hisia za mume leo anavaa kuteka hisia za watu wa nje kwa sababu ndiko anakotumia muda wake mwingi. Zamani alikuwa na marafiki waliomzunguka anapoishi leo ana marafiki wa mbali, ambao wana nafasi ya kumjengea mtazamo tofauti.
Mwanamke ameondolewa kwenye nafasi yake ambapoalikuwa chombo cha thamani kubwa na sasa amegeuka mshindani na wanaume. Jamii imemshusha hadhi mwanamke naye amefumbwa macho kuikubali hali hihyo, ndio maana anaishi maisha yasiyo na malengo na matokeo yake ni kuishia kwenye majuto makuu.
Najua mada kama hizi ni ngumu lakini lazima tuangalie ni wapi tulipojikwaa. Feminism ilipaswa kuboresha majukumu ya mwanamke, badala yake imefanya mwanamke awe kama mwanamume.
Mwanamke na mwanamume wameumbwa tofauti kwa malengo tofauti. Utofauti huo haufanyi mmoja awe inferior kwa mwenzake bali wawe umoja ili kutimiliza malengo ya uwepo wao duniani ambayo lengo kuu ni kuendeleza kizazi (procreation). Nasema wameumbwa tofauti kwa malengo tofauti kwa sababu zifuatazo:
Maisha ya kijamii
Mfumo wa maisha wa mwanamke umetofautiana kwa kiasi kikubwa na mwanamume. Mwanamke amepewa maisha ya kuhusiana na jamii inayomzunguka, ndio maana utaona wanawake wanakuwa na makundi mtaani, kwamba huyu ni rafiki yangu wa karibu huyu sio. Wanakutana kupeana simulizi za kuhusu maisha ya wengine, nani kapigwa na mume, nani hajui kuvaa, nani kanyang'anya mchumba wa mwingine n.k. Kama huamini fuatilia aina ya maongezi ya wanawake wote bila kujali elimu zao. Hili si baya hata kidogo, ndivyo walivyoumbwa. Mwanamke ni kiumbe anayestahili kuwa kwenye mazingiri ya nyumbani kwake kwa muda mwingi zaidi, ni mlezi.
Mwanamume kwa upande wake ameumbiwa maisha ya kutangatanga. Maongezi yao mengi ni kuhusu nani kapataje utajiri, nani kamtapeli mwingine, nani kavusha mzigo nje ya nchi n.k. Mwanamume ni mtafutaji, kwa ajili ya mke na watoto, tena kwa ajili ya wazazi. Mwanamume ni mlezi wa jamii kwa ujumla wake na ndio maana akili yake imeumbwa kufikiri namna ya kupata mali kwa ajili ya familia. Hivi umewahi kujiuliza ni kwa nini hatuna majambazi wanawake?
Uumbaji
Mwanamke na mwanamume hushiriki uumbaji kwa kuunganisha mbegu na yai. Kwa sababu mwanamke sio mtafutaji kiasili, yeye amewekewa mfuko wa uzazi na mfumo wa uleaji wa mtoto mpaka awapo mtu mzima. Mwanamume hajapewa mfumo huo ili awe mtafutaji, amepewa kuwa na nguvu zake mwaka mzima apate kumtunza mke na familia. Kila mfumo uliwekwa kwa kusudi lake.
Jinsi jamii ilivyopora nafasi ya mwanamke
Mapinduzi ya wanawake kuingia kwenye majukumu ya kufanya kazi yalianza wakati wa vita kuu ya pili ya dunia. Hapa kuna hoja nyingi mno lakini siongelei kwa sasa kwa kuogopa kuifanya thread kuwa ndefu. Lakini niseme tu, tuchunguze mfumo wa elimu sasa na kabla.
Zamani mtoto wa kike alipewa elimu yenye ubora wa hali ya juu, iliyomjenga vema kutambua majukumu yake. Shule yao kuu ilikuwa ni wazazi wake ambao aliumia muda mwingi kuwa nao nyumbani. Elimu hii ilimfanya kuwa mwanamke bora aliyejitambua nafasi yake na majukumu yake pia. Mwanamke ni mlazi wa familia, hivyo elimu ililenga kumjengea uwezo kwenye eneo hilo.
Kwa mtoto wa kiume elimu yake iliendana na majukumu yake pia, utafutaji. Kwa kuwa kiasili mwanamume ni mtafutaji, jamii ilijikita kumpatia elimu itakayomwezesha kutafuta mali ili kumudu majukumu ya kumtunza mke na watoto. Ndio maana zamani mtoto wa kiume alipewa nafasi kubwa kusoma elimu ya kizungu (mashuleni na vyuoni). Wapi mambo yalipobadilika?
Pale dunia ilipobadili mfumo na kuanza kuwajengea mtazamo wanawake na jamii kwa ujumla kuwa mwanamke anastahili kuwa na kipato chake, asiwe tegemezi kwa mume (hoja inayoondoa kabisa maana ya ndoa na majukumu yaliyomo humo), ndoa zikatazamwa kama gereza la mwanamke. Kwamba mwanamke anapoingia kwenye ndoa kwa mtazamo wa zamani ananyimwa uhuru wa kujitafutia kipato chake mwenyewe. Ndipo likaja swala la elimu.
Mwanamke akatakiwa kupatiwa elimu sawa na mwanamume, mambo ya haki sawa. Hili lilikuwa jambo jema kwa kulitazama kwa juu juu, lakini ukiangalia kwa undani, mwanamke kupatiwa elimu ya utafutaji ni kumwondoa kwenye nafasi yake kama mke. Elimu iliyolenga kutafuta mali tangu awali ilimlenga mtafutaji, mwanamume. Sasa badala ya dunia kuleta elimu inayolenga kuboresha nafasi ya mwanamke, ikaleta elimu inayolenga kumfanya mwanamke awe sawa na mwanamume. Mwanamke hawezi kuwa sawa na mwanamume na ndio maana kinachotokea ni kuigiza kuwa kama mwanamume.
Wanawake wamekuwa wakiishi maisha ya uigizaji, na hii imewafanya kutokujitambua, kutokujua thamani yao na nafasi yao katika jamii. Jamii imemshusha hadhi mwanamke na kumfanya kama mwanamume, isipokuwa tu ameshindwa kabisa kuenenda kwa jinsia hiyo. Matokeo yake wanawake wamegeuzwa kuwa chombo cha starehe, matangazo ya biashara. Mwanamke ambaye zamani alikuwa akiishi na jamii iliyomzunguka huku akijiweka kumliwaza mume, sasa anaishi na jamii za mbali kwa sababu ni mfanya biashara ama mfanyakazi. Zamani alivaa kuteka hisia za mume leo anavaa kuteka hisia za watu wa nje kwa sababu ndiko anakotumia muda wake mwingi. Zamani alikuwa na marafiki waliomzunguka anapoishi leo ana marafiki wa mbali, ambao wana nafasi ya kumjengea mtazamo tofauti.
Mwanamke ameondolewa kwenye nafasi yake ambapoalikuwa chombo cha thamani kubwa na sasa amegeuka mshindani na wanaume. Jamii imemshusha hadhi mwanamke naye amefumbwa macho kuikubali hali hihyo, ndio maana anaishi maisha yasiyo na malengo na matokeo yake ni kuishia kwenye majuto makuu.
Najua mada kama hizi ni ngumu lakini lazima tuangalie ni wapi tulipojikwaa. Feminism ilipaswa kuboresha majukumu ya mwanamke, badala yake imefanya mwanamke awe kama mwanamume.
