BabaDesi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2007
- 6,032
- 3,944
Kila mara ninapoangalia kipindi cha Jambo kinachorushwa hewani na Televisheni ya Taifa TBC napata wasiwasi kwamba ama viongozi wa kitaifa wa Tanzania hawafahamu kuwa Time is Money, hata dakika moja tu, ama hawajali.
Utaratibu wa kipindi hiki ni kumuita mheshimiwa kiongozi yoyote na kuanza kuhojiana naye lakini katikati ya mahojiano hayo kipindi kinapelekwa kwa mtangazaji mwingine ambaye husoma taarifa za michezo ama za magazeti kwanza ndipo hurejeshwa kwa mtangazaji anayehojiana na mgeni wa kipindi ambaye atakuwa amekaa tu akisubiri!
Nimekuwa nikijiuliza kwa nini hawaendelei kumhoji tu mgeni aliye studio wakamalizana naye kabisa akajiondokea kuendelea na shughuli zake nyingine ndipo waendelee na habari za nagazeti na michezo.
Ninajiuliza sana kuhusu aina ya viongozi, wakiwemo hata mawaziri, wanaokubali kuwekwa kando kwanza kwa dakika kumi ili kupisha habari za magazeti na za Michezo!
Dakika kumi ni nyingi sana kwa kiongozi kukaa tu Studio akisubiri kuhojiwa!
TBC, mhojini kiongozi,malizaneni naye kabisa ajiondokee akaendelee na shughuli zake za kujenga nchi na nyinyi muendelee na habari za michezo na magazeti! Kwani kuna tabu gani kufanya hivyo? Time is Money, jamani! Unless Viongozi wa Kitanzania wanaoitwa studio za TBC hawalioni hili!
Utaratibu wa kipindi hiki ni kumuita mheshimiwa kiongozi yoyote na kuanza kuhojiana naye lakini katikati ya mahojiano hayo kipindi kinapelekwa kwa mtangazaji mwingine ambaye husoma taarifa za michezo ama za magazeti kwanza ndipo hurejeshwa kwa mtangazaji anayehojiana na mgeni wa kipindi ambaye atakuwa amekaa tu akisubiri!
Nimekuwa nikijiuliza kwa nini hawaendelei kumhoji tu mgeni aliye studio wakamalizana naye kabisa akajiondokea kuendelea na shughuli zake nyingine ndipo waendelee na habari za nagazeti na michezo.
Ninajiuliza sana kuhusu aina ya viongozi, wakiwemo hata mawaziri, wanaokubali kuwekwa kando kwanza kwa dakika kumi ili kupisha habari za magazeti na za Michezo!
Dakika kumi ni nyingi sana kwa kiongozi kukaa tu Studio akisubiri kuhojiwa!
TBC, mhojini kiongozi,malizaneni naye kabisa ajiondokee akaendelee na shughuli zake za kujenga nchi na nyinyi muendelee na habari za michezo na magazeti! Kwani kuna tabu gani kufanya hivyo? Time is Money, jamani! Unless Viongozi wa Kitanzania wanaoitwa studio za TBC hawalioni hili!