Jamani hii ya Kamanda Kova imekaaje?

Mzee Mzima

Senior Member
Joined
Mar 31, 2008
Posts
159
Reaction score
47
Naomba msaada kujua Kweli Salute ni nani anapigiwa kwani hapa naona anatoa salute wakati wa kumuaga Kanumba, I think this is not right, wanaojua please enlight me.
 
Wewe ndi hujui protocol za kijeshi...kijeshi maiti yeyote inapigiwa salute...sasa wewe raia haya mambo huyajui bora ukae kimya...
 
Imekaa njema haina tatizo kwa kamanda Suleiman Kova kufanya hvyo.
 
Tafuta kwanza tafsiri sahihi ya neno Salute, ukishaipata maana yake basi haitakusumbuwa hata chembe.
 
Katika taratibu za kijeshi maiti yo yote, hata ya kwako inapigiwa salute na askari aiyevaa sare wakati wa kutoa heshima za mwisho.
 
eti kuna mtu anauliza kuwa sugu ni kamanda?

nenda mbeya kaulize sugu ni nani?

baada ya jeshi kushindwa ukamada chadema imeamua kusimamia mambo yote yanayohusu ukamanda.
 
Nimesoma gazeti la Tanzania Daima leo habari hii na imenishangaza sana
Ukweli ni kwamba Kova alikuwa sahihi kabisa kwa kitendo alichofanya na kwa ufafanuzi alioutoa na nimemkubali kwa elimu aliyoitoa kwani kisheria Saluti ni alama ya heshima kwa mkuu au mtu mwenye mamlaka juu yako. Kimsingi nyuma ya Majeshi yote duniani yana raia kama wawezeshaji wakuu wa uwepo wao. Katika mila na desturi za kijeshi Raia wa kawaida hapigiwi saluti isipokuwa kama yafuatayo yatajiri:
i. Akiwa na cheo cha kisiasa ambacho moja kwa moja anamwakilisha Rais , Mfalme, Malkia au Mkuu wa nchi.
ii. Akiwa amefariki ambapo askari au Afisa bila ya kujali cheo chake hata kama ni CDF (Chief of Defence Forces) IGP
au Kamishna anapaswa kusimama kwa heshima na kuupigia saluti mwili kutoa salamu na heshima kwa Raia yule
ambaye kimsingi ndiye aliyekuwa mwajiri wake. Saluti kwa mwili haijalishi umri, jinsia, wala cheo cha marehemu
alipokuwa mzima wala rika la marehemu kulinganisha na anayeitoa saluti hiyo. Kwa maana hiyo askari aliyeiva
sawasawa kama Kamanda Kova na anayejua wajibu wake ataupigia saluti hata mwili wa mtoto mdogo ukiwa
umeandaliwa kwa mazishi au ukiwa safarini kuelekea huko.
iii. Katika nchi za kifalme Malkia na familia ya kifalme hupigiwa saluti.
NB: Ninayeandika haya ni Afisa Mwandamizi Mstaafu aliyehudumia JWTZ kwa zaidi ya miaka 40 hadi kustaafu na aliyefanya mafunzo (Na kufundisha) ndani na nje ya nchi hii.
Changamoto: Maafisa na maaskari wa leo ambao awali hamkuwa mkijua hili kama huyo Afisa aliyenukuliwa na gazeti hilo (Kwenye grey bold) mjifunze kutokana na somo alilolitoa Kova.
Inatisha, kusikitisha na kukatisha tamaa kuona wapo ndani ya majeshi yetu aina ya maafisa kama huyo aliyenukuliwa na gazeti hilo.
Bravo Commander Kova.
 
Huyo mzee alikuwa anatafuta jinsi atakavyotoka kiaina. Kanumba alikuwa na title gani hadi kupigiwa saluti?
 
Kwa maoni yangu kamanda Kova hakuwa sahihi kuipigia salute maiti ya Kanumba.

Sababu salute ni salamu au heshima ya kijeshi kwa mtu aliyekuzidi cheo au mamlaka.

Kova anajua miko ya salute lakini nadhani alipitiwa tu.
 

Hata wewe hujajibu. Kwa ufupi Kova alikuwa sahihi kupiga salute ile ni msingi wake si mwili wa marehemu bali hoja ya kwanza ni kuwa alivaa uniform na pale alikuwepo Makamu wa Raisi na baadhi ya Mawaziri amabao wanapigiwa salute kwa hiyo anapopita pale pamoja na mwili salute inaonyesha utii wa kijeshi kwa wakuu waliokuwapo ktk wale waombolezaji km kusingekuwa na hao heshima kijeshi au kwa askari alovaa unform hawezi bend atakunja mikono na kuinuka kidogo lkn kwa uwepo wa viongozi wale anatoa heshima hiyo kutambua uwepo wao hapo. Tanzania daima nao wakurupukaji
 
Kama ana heshima ampigie basi Dk. Slaa kama haujasikia another version of story, labda aseme to the late Kanumba was secret service na alikua na cheo kuliko yeye, otherwise babu kachemka mazima
 
kova hajakosea.., polisi na jeshi, wote wanapaswa kum-salute marehemu YOYOTE..., awe na cheo asiwe na cheo.., ni heshima anayopewa marehemu..,

haku-salute kwa sbb ni kanumba, amesalute kwa sbb yule ni marehemu na anapewa heshima yake....,

kama hujui kanuni na nidhamu za kijeshi usibishe vitu usivovijua.., lakn ku-avoid kuchanganya watu wasiojua haya mambo ndio maana servicemen wengi wanaenda na civ clothes,

Ile ni nidhamu ya kijeshi kwa marehemu wetu si kwa sbb ni kanumba, nada!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…