Jamani eh, sasa nimeamini, panapofuka moshi kweli panaficha moto......

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Kuna rafiki yangu wa karibu anaishi nyumba za kupanga na kwa yale ambayo amenielezea hadi sasa yananithibitishia ya kuwa kwenye mapango hayo kweli kuna mambo.

Huyu njema ana kidosho wake mrembo haswaa yaani ile ya mithili ya maandiko ya Shabaan Robert kama vile. Hawa wanandoa wanaishi wote bali yeye ni mtu wa masafa marefu kwa maana ya kuendesha malori makubwa na muda mwingi yupo nje ya pango lake.

Sasa amejawa na hofu sana katika nyumba aishio ambayo ina makapera wengi sana na jinsi awaonavyo hasa wanaposalimiana na mke wake machale yanamcheza cheza kuwa hapa siyo bure ipo shughuli kubwa inaendelea wakati yeye yupo safarini akitafuta ugali wa familia. Hadi sasa bado hawajajaliwa kupata mtoto.

Siku moja usiku alirudi mapema kidogo kuliko ilivyotarajiwa na aliyoyakuta yalimwongezea wasiwasi.............alikuta njemba nyingine imetuna kwenye kiti chake huko ikitwanga biryani ya nguvu na bia ikiwemo hapo pembeni kwake.

Yaani memsapu alipomwona jamaa yake alishtuka sana na hili liliongezea ule wasi wasi wa jamaa yangu mbona hawa majirani huwa hawamtembelei akiwepo lakini akiwa hayupo ndiyo vikumbo kwake vinapata kasi sana? Na swali jingine lililomkera ni kuwa kwanini mama watoto alishtuka hivyo kama hakuna mpango wowote ule wa dhuluma dhidi yake?

Jamaa yangu huyu ameanza hata kukonda maana ana wasiwasi sana hawa majirani zake wanaweza kuwa wanamlisha memsapu wake visivyofaa kuliwa na madhara yake sote tunayajua...

Sasa jamaa yangu amekuja kwangu kwa ushauri wa kiutu uzima na mimi nimemweleza nina ndugu zangu kwenye Jamii Forums kwa hiyo anipe muda wa kukusanya ushauri wa kujitosheleza...............

Sasa kazi kwenu ajitoe vipi hapa huyu ndugu yangu ambaye simanzii yake sasa ni mlima......anampenda mama watoto wake ile mbaya lakini hayupo tayari kuona njema zinamfanyia unyama huo anaouhisi na anadai machale yake siyo ya utani utani ni ya uhakika vile.............
 
Ruta,
Kwani jamaa hakuwahi kumuliza mkewe kuwa kwanini hizo njemba huwa zinakuja akiwa tu hayupo?siku hiyo ya njemba kula msosi na mamie kushtuka jamaa hakumuliza baadae kuwa ni nini kilimshtua? Je ni njemba tofautitofauti au ni aina moja huwa anaikuta?zote zinaishi around?
Kama utafafanua hapo naweza sema kitu.
 
kama demu sio mwaminifu vile! yani mumeo hayupo wewe unaingiza njemba ingine tena ni jirani anakula na glass ya bia pembeni!?
 
Keep it up ruta I will the first to congrats when u reach 1000 posts. I hope you will be in JF records as you recently joined and turn 1000 in a short period. NAkuaminia muzee:biggrin1:
 
Keep it up ruta I will the first to congrats when u reach 1000 posts. I hope you will be in JF records as you recently joined and turn 1000 in a short period. NAkuaminia muzee:biggrin1:

Sokomoko umenifurahisha sana,,close follow up
 
Sokomoko umenifurahisha sana,,close follow up

Jamaa leo moja ameanzisha threads 8 na post alizofanya ni 36 hadi hapa tu mie nampa hongera sana aendelee hivi hivi na kutu encourage na sie tupige mabandiko 50 per day!
 
Kuna rafiki yangu wa karibu anaishi nyumba za kupanga na kwa yale ambayo amenielezea hadi sasa yananithibitishia ya kuwa kwenye mapango hayo kweli kuna mambo.

Huyu njema ana kidosho wake mrembo haswaa yaani ile ya mithili ya maandiko ya Shabaan Robert kama vile. Hawa wanandoa wanaishi wote bali yeye ni mtu wa masafa marefu kwa maana ya kuendesha malori makubwa na muda mwingi yupo nje ya pango lake.

Sasa amejawa na hofu sana katika nyumba aishio ambayo ina makapera wengi sana na jinsi awaonavyo hasa wanaposalimiana na mke wake machale yanamcheza cheza kuwa hapa siyo bure ipo shughuli kubwa inaendelea wakati yeye yupo safarini akitafuta ugali wa familia. Hadi sasa bado hawajajaliwa kupata mtoto.

Siku moja usiku alirudi mapema kidogo kuliko ilivyotarajiwa na aliyoyakuta yalimwongezea wasiwasi.............alikuta njemba nyingine imetuna kwenye kiti chake huko ikitwanga biryani ya nguvu na bia ikiwemo hapo pembeni kwake.

Yaani memsapu alipomwona jamaa yake alishtuka sana na hili liliongezea ule wasi wasi wa jamaa yangu mbona hawa majirani huwa hawamtembelei akiwepo lakini akiwa hayupo ndiyo vikumbo kwake vinapata kasi sana? Na swali jingine lililomkera ni kuwa kwanini mama watoto alishtuka hivyo kama hakuna mpango wowote ule wa dhuluma dhidi yake?

Jamaa yangu huyu ameanza hata kukonda maana ana wasiwasi sana hawa majirani zake wanaweza kuwa wanamlisha memsapu wake visivyofaa kuliwa na madhara yake sote tunayajua...

Sasa jamaa yangu amekuja kwangu kwa ushauri wa kiutu uzima na mimi nimemweleza nina ndugu zangu kwenye Jamii Forums kwa hiyo anipe muda wa kukusanya ushauri wa kujitosheleza...............

Sasa kazi kwenu ajitoe vipi hapa huyu ndugu yangu ambaye simanzii yake sasa ni mlima......anampenda mama watoto wake ile mbaya lakini hayupo tayari kuona njema zinamfanyia unyama huo anaouhisi na anadai machale yake siyo ya utani utani ni ya uhakika vile.............

nakushauri, ukamshauri......ahame hiyo nyumba
 
Akihama na baadaye njemba zikaja alikohamia na hapa mama akadai zimekuja kumsalimia kwani walikuwa majirani wazuri kwenye nyumba ya awali!!!
amweleze kisa cha kuhama kuwa anakimbiza mzingo toka kwa hao manjemba anahisi wanamwibia...
 
1 aongee na mkewe juu ya wasi wasi km kweli ama si kweli atajua kutoka kwenye mdomo wa mkewe
2 aafanye kauchunguzi kdg japo kwa kuwauliza majirani wengine au aweke kijimtego au amtume mtu awe anamfatilia mkewe wakat hayupo
3ahame nyumba
 
1 aongee na mkewe juu ya wasi wasi km kweli ama si kweli atajua kutoka kwenye mdomo wa mkewe
2 aafanye kauchunguzi kdg japo kwa kuwauliza majirani wengine au aweke kijimtego au amtume mtu awe anamfatilia mkewe wakat hayupo
3ahame nyumba
Kutumia mbinu namba 1 hapo juu ni sawa na kumpatia JK nafasi ya kukoment kuhusu kukamatwa kwa karatasi za kupigia kura huko Tunduma....! Kwani ungetegemea jibu gani?

No. 2 huenda ikazaa matunda ya ukweli, lakini mara nyingi jamii huwa tunafichiana maovu kama haya...! Katika watu waliowagumu kukupa ukweli ni marafiki, na maadui wako, hasa pale wanapojua ungefanya maamuzi gani....! La msingi ni kwamba aelewe kuwa kumfumania nyoka si lazima umkute akiingia shimoni, bali hata ukimkuta akitoka ni kumfumania pia....! Mwenye macho haambiwi tazama, na akiambiwa ni tusi...! Sasa yeye anataka tumtusi? For an act to be cheating is not necessarily to be confirmed by the cheater....!

No 3 pia sio solution, maana huko atakapohamia na manjemba wapo...! Matokeo yake atazidi kuongeza idadi tu....!
 
wasi wasi wa mapenzi mwenzangu wauaaaaaaaaaaaa,its beta said if nothing is said at all.afanye uchunguzi kwanza kwa kina kwenye ukweli uhongo hujitenga,everything happen for a reason,smtimes silent has the loudest voice.
 
Kutumia mbinu namba 1 hapo juu ni sawa na kumpatia JK nafasi ya kukoment kuhusu kukamatwa kwa karatasi za kupigia kura huko Tunduma....! Kwani ungetegemea jibu gani?

No. 2 huenda ikazaa matunda ya ukweli, lakini mara nyingi jamii huwa tunafichiana maovu kama haya...! Katika watu waliowagumu kukupa ukweli ni marafiki, na maadui wako, hasa pale wanapojua ungefanya maamuzi gani....! La msingi ni kwamba aelewe kuwa kumfumania nyoka si lazima umkute akiingia shimoni, bali hata ukimkuta akitoka ni kumfumania pia....! Mwenye macho haambiwi tazama, na akiambiwa ni tusi...! Sasa yeye anataka tumtusi? For an act to be cheating is not necessarily to be confirmed by the cheater....!

No 3 pia sio solution, maana huko atakapohamia na manjemba wapo...! Matokeo yake atazidi kuongeza idadi tu....!


kwani huku ni kwenye ukumbi wa uchaguzi au siasa???
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom