Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Kuna rafiki yangu wa karibu anaishi nyumba za kupanga na kwa yale ambayo amenielezea hadi sasa yananithibitishia ya kuwa kwenye mapango hayo kweli kuna mambo.
Huyu njema ana kidosho wake mrembo haswaa yaani ile ya mithili ya maandiko ya Shabaan Robert kama vile. Hawa wanandoa wanaishi wote bali yeye ni mtu wa masafa marefu kwa maana ya kuendesha malori makubwa na muda mwingi yupo nje ya pango lake.
Sasa amejawa na hofu sana katika nyumba aishio ambayo ina makapera wengi sana na jinsi awaonavyo hasa wanaposalimiana na mke wake machale yanamcheza cheza kuwa hapa siyo bure ipo shughuli kubwa inaendelea wakati yeye yupo safarini akitafuta ugali wa familia. Hadi sasa bado hawajajaliwa kupata mtoto.
Siku moja usiku alirudi mapema kidogo kuliko ilivyotarajiwa na aliyoyakuta yalimwongezea wasiwasi.............alikuta njemba nyingine imetuna kwenye kiti chake huko ikitwanga biryani ya nguvu na bia ikiwemo hapo pembeni kwake.
Yaani memsapu alipomwona jamaa yake alishtuka sana na hili liliongezea ule wasi wasi wa jamaa yangu mbona hawa majirani huwa hawamtembelei akiwepo lakini akiwa hayupo ndiyo vikumbo kwake vinapata kasi sana? Na swali jingine lililomkera ni kuwa kwanini mama watoto alishtuka hivyo kama hakuna mpango wowote ule wa dhuluma dhidi yake?
Jamaa yangu huyu ameanza hata kukonda maana ana wasiwasi sana hawa majirani zake wanaweza kuwa wanamlisha memsapu wake visivyofaa kuliwa na madhara yake sote tunayajua...
Sasa jamaa yangu amekuja kwangu kwa ushauri wa kiutu uzima na mimi nimemweleza nina ndugu zangu kwenye Jamii Forums kwa hiyo anipe muda wa kukusanya ushauri wa kujitosheleza...............
Sasa kazi kwenu ajitoe vipi hapa huyu ndugu yangu ambaye simanzii yake sasa ni mlima......anampenda mama watoto wake ile mbaya lakini hayupo tayari kuona njema zinamfanyia unyama huo anaouhisi na anadai machale yake siyo ya utani utani ni ya uhakika vile.............
Huyu njema ana kidosho wake mrembo haswaa yaani ile ya mithili ya maandiko ya Shabaan Robert kama vile. Hawa wanandoa wanaishi wote bali yeye ni mtu wa masafa marefu kwa maana ya kuendesha malori makubwa na muda mwingi yupo nje ya pango lake.
Sasa amejawa na hofu sana katika nyumba aishio ambayo ina makapera wengi sana na jinsi awaonavyo hasa wanaposalimiana na mke wake machale yanamcheza cheza kuwa hapa siyo bure ipo shughuli kubwa inaendelea wakati yeye yupo safarini akitafuta ugali wa familia. Hadi sasa bado hawajajaliwa kupata mtoto.
Siku moja usiku alirudi mapema kidogo kuliko ilivyotarajiwa na aliyoyakuta yalimwongezea wasiwasi.............alikuta njemba nyingine imetuna kwenye kiti chake huko ikitwanga biryani ya nguvu na bia ikiwemo hapo pembeni kwake.
Yaani memsapu alipomwona jamaa yake alishtuka sana na hili liliongezea ule wasi wasi wa jamaa yangu mbona hawa majirani huwa hawamtembelei akiwepo lakini akiwa hayupo ndiyo vikumbo kwake vinapata kasi sana? Na swali jingine lililomkera ni kuwa kwanini mama watoto alishtuka hivyo kama hakuna mpango wowote ule wa dhuluma dhidi yake?
Jamaa yangu huyu ameanza hata kukonda maana ana wasiwasi sana hawa majirani zake wanaweza kuwa wanamlisha memsapu wake visivyofaa kuliwa na madhara yake sote tunayajua...
Sasa jamaa yangu amekuja kwangu kwa ushauri wa kiutu uzima na mimi nimemweleza nina ndugu zangu kwenye Jamii Forums kwa hiyo anipe muda wa kukusanya ushauri wa kujitosheleza...............
Sasa kazi kwenu ajitoe vipi hapa huyu ndugu yangu ambaye simanzii yake sasa ni mlima......anampenda mama watoto wake ile mbaya lakini hayupo tayari kuona njema zinamfanyia unyama huo anaouhisi na anadai machale yake siyo ya utani utani ni ya uhakika vile.............