Wakuu,
Nilikuwa nimesitisha kwa muda kuingia humu JF kwa ajili ya kutoa mchango wangu wa aina yoyote au kuanzisha bandiko kutokana na kuwa na kazi nyingi, lakini kwa hili nimeamua nije na kuwaandikia ili muone tulipofikia.
Majira ya saa 11 na nusu jioni nikiwa natokea eneo langu la kazi, nikakutana na vurumai njiani, watu wamekusanyika kelele nyingi, sasa ikabidi nisimame na kujionea kulikoni!
Hiki nakichukulia kama kisa kibaya zaidi kuwahi kushuhudia maishani mwangu. Kisa chenyewe ni kwamba mke wa mtu amefumaniwa na mme wake, akiwa pamoja na watu wengine, akifuturu penzi jioni hii (kwa mjibu wa mme wake huyo mke alikuwa amefunga).
Nilimshuhudia mwanaume akilia kwa uchungu usiosemekana, hasira zimempanda, akisema kwa sauti niachieni niue mtu. Bora nikafungwe maisha au ninyongwe. Watu walikuwa wamemkamata wakimfariji na kumsihi atulie.
Taarifa za awali kabla ya vurumai hilo zinadai kwamba, jamaa alishtuliwa na watu kuwa mke wake yupo kwenye kibanda fulani, ambapo huwa naona kundi la vijana wamerundikana mahali hapo; inasemekana ni studio ya muziki. Baada ya jamaa kuja na kundi la watu na kupafanyia "ambush" mahali hapo, wale wazinifu walifanikiwa kukurupuka na kutokea mlango mwingine wa hiyo studio (watu wanadai wameshtuliwa wasepe).
Ndani ya hiyo studio, wavamizi walikuta mkoba, chupi; na simu ambayo ilikuwa imezimwa. Yule mme amedai mkoba, simu, chupi na baadhi ya vitu vilivyokuwemo ndani ya mkoba ni vya mke wake. Pia amedai kumwona mke wake akitokomea na pikipiki upande wa pili na mtu ambaye hakumfahamu.
Kulikuwa na mvurugano usiokuwa wa kawaida, jamaa anaongea kwa uchungu na kudai kwamba mpango mzima wa mke wake kuzini na huyo mtu, umeratibiwa na hao vijana.
Hao vijana walikuwa wakimtia machungu zaidi kwa kurusha maneno machafu, kwamba wao hawamjui mke wake wala mtu aliyezini naye, wala yeye, halafu inakuwaje yeye anakomaa na wao badala ya jamaa aliyemmega mkewe! Nanukuu "usituzingue, acha mambo ya kifamba, kwanza we wa wapi? Yule mshikaji kaja kwetu na huyo demu ambaye sie tulijua ni mtu wake wakitaka kutengeneza nyimbo, sasa tumewakaribisha ndani chumbani, kama wamemegana sie inatuhusu nini, achana na sisi tupotezee, kama vipi kwa nini usikomae na jamaa aliyemega mkewe!".
Mme wa mama aliyefumaniwa amedai kwamba, majira ya saa saba mchana amempa mke wake hela sh 30,000/= kwa ajili ya kwenda Kariakoo kufanya manunuzi ya maandalizi ya sikukuu ya Idd; vyakula, nguo za watoto (maana amedai kuwa na watoto watatu), ikiwemo nguo za mkewe (alitaja gauni), lakini baadae, mida ya saa tisa na nusu alipewa taarifa na rafiki yake wa karibu kwamba mke wake ameonekana maeneo hayo, ndipo alipotafuta wenzake na kuamua kuja kupavamia mahali hapo.
Kulikuwa na kila dalili ya kwamba huenda umaskini ndio uliomfanya huyo mke kuasi, lakini kamwe hiyo haiwezi kuwa sababu ya msingi! Vile vile, sidhani kama huu mwezi walikuwa hawapeani mapenzi kwa sababu ya mfungo.
"I have made this letter longer than usual, because I lack the time to make it short. " Blaise Pascal
Nilikuwa nimesitisha kwa muda kuingia humu JF kwa ajili ya kutoa mchango wangu wa aina yoyote au kuanzisha bandiko kutokana na kuwa na kazi nyingi, lakini kwa hili nimeamua nije na kuwaandikia ili muone tulipofikia.
Majira ya saa 11 na nusu jioni nikiwa natokea eneo langu la kazi, nikakutana na vurumai njiani, watu wamekusanyika kelele nyingi, sasa ikabidi nisimame na kujionea kulikoni!
Hiki nakichukulia kama kisa kibaya zaidi kuwahi kushuhudia maishani mwangu. Kisa chenyewe ni kwamba mke wa mtu amefumaniwa na mme wake, akiwa pamoja na watu wengine, akifuturu penzi jioni hii (kwa mjibu wa mme wake huyo mke alikuwa amefunga).
Nilimshuhudia mwanaume akilia kwa uchungu usiosemekana, hasira zimempanda, akisema kwa sauti niachieni niue mtu. Bora nikafungwe maisha au ninyongwe. Watu walikuwa wamemkamata wakimfariji na kumsihi atulie.
Taarifa za awali kabla ya vurumai hilo zinadai kwamba, jamaa alishtuliwa na watu kuwa mke wake yupo kwenye kibanda fulani, ambapo huwa naona kundi la vijana wamerundikana mahali hapo; inasemekana ni studio ya muziki. Baada ya jamaa kuja na kundi la watu na kupafanyia "ambush" mahali hapo, wale wazinifu walifanikiwa kukurupuka na kutokea mlango mwingine wa hiyo studio (watu wanadai wameshtuliwa wasepe).
Ndani ya hiyo studio, wavamizi walikuta mkoba, chupi; na simu ambayo ilikuwa imezimwa. Yule mme amedai mkoba, simu, chupi na baadhi ya vitu vilivyokuwemo ndani ya mkoba ni vya mke wake. Pia amedai kumwona mke wake akitokomea na pikipiki upande wa pili na mtu ambaye hakumfahamu.
Kulikuwa na mvurugano usiokuwa wa kawaida, jamaa anaongea kwa uchungu na kudai kwamba mpango mzima wa mke wake kuzini na huyo mtu, umeratibiwa na hao vijana.
Hao vijana walikuwa wakimtia machungu zaidi kwa kurusha maneno machafu, kwamba wao hawamjui mke wake wala mtu aliyezini naye, wala yeye, halafu inakuwaje yeye anakomaa na wao badala ya jamaa aliyemmega mkewe! Nanukuu "usituzingue, acha mambo ya kifamba, kwanza we wa wapi? Yule mshikaji kaja kwetu na huyo demu ambaye sie tulijua ni mtu wake wakitaka kutengeneza nyimbo, sasa tumewakaribisha ndani chumbani, kama wamemegana sie inatuhusu nini, achana na sisi tupotezee, kama vipi kwa nini usikomae na jamaa aliyemega mkewe!".
Mme wa mama aliyefumaniwa amedai kwamba, majira ya saa saba mchana amempa mke wake hela sh 30,000/= kwa ajili ya kwenda Kariakoo kufanya manunuzi ya maandalizi ya sikukuu ya Idd; vyakula, nguo za watoto (maana amedai kuwa na watoto watatu), ikiwemo nguo za mkewe (alitaja gauni), lakini baadae, mida ya saa tisa na nusu alipewa taarifa na rafiki yake wa karibu kwamba mke wake ameonekana maeneo hayo, ndipo alipotafuta wenzake na kuamua kuja kupavamia mahali hapo.
Kulikuwa na kila dalili ya kwamba huenda umaskini ndio uliomfanya huyo mke kuasi, lakini kamwe hiyo haiwezi kuwa sababu ya msingi! Vile vile, sidhani kama huu mwezi walikuwa hawapeani mapenzi kwa sababu ya mfungo.
"I have made this letter longer than usual, because I lack the time to make it short. " Blaise Pascal