Jakaya Kikwete na msafara mkubwa

Jakaya Kikwete na msafara mkubwa

Kutoka Sea View Hotel pale Lindi hadi pale kwake Mtanda Lindi! Unaweza kutembea hata kwa mguu tu! Sasa huo msafara na msururu wa magari ya nini??
Sasa wewe unataka kujilinganisha na kikwete,kwa kuwa wewe unasaga lami na Kikwete afanye hivio hii itakupelekea kuwa chukia wenye nacho
 
Hata kama akiwa safari! Huwezi kua na ule msafara! Labda kama kuna mambo mengine nje ya tujuayo! Mkapa kaja sana Lupaso kwao na hakua na huo msafara! Mwinyi kila siku anaenda kwenye mashamba yake huko mkuranga hana huo msafara
Kila mtu na uamuzi wake Mkapa sio Mwinyi wala Magu sio Kikwete
 
magu aliwabana sana wala kodi zetu dizain hii, huyu mama ndio anawaendekeza halafu anatutaka tulipe matozo kibao
Magu mwenyewe alikuwa anamtuma kumwakilisha baadhi ya nchi,alafu unajuaje kuwa huo msafara unagalamiwa na serikali kwa Kikwete masikini kama wewe?
 
Kwa upumbavu huu ,nchi hii ina safari ndefu ya kujikomboa maana naona middle class karibu wengi wameoza kichwani, President Mandela baada ya kustaafu msafara wake haukuzidi 3 cars (including police sweep car)na hata wakati wanampeleka hospital, Ambulance yake ilipata breakdown na ilichukua muda msaada kumfikia,President H&H misafara yake haizidi 4 cars!,President CR misafara yake haizidi 4 cars, President wa Botswana msafara wake 3 cars!!,Tanzania tumekosea wapi?
Kwanza nyiyi mnao jifanya amjui kiswahili ndio wabaya sana mkipata nafasi serikalini
 
Kikwete hana njaa mkumbuke tu. Mzee anaishi maisha yake wala haumizi kichwa kuhusu mafuta ya gari wala kula na kuvaa yeye na familia yake.

Akiamua tu anaweza hata convoy yake akaijaza Lexus tupu. Badala ya V8 na hamna kitu mtafanya.
 
Toka mwaka mpya umeanza nipo kusini mikoa ya Lindi na Mtwara napambana na maisha yangu yakujiandaa na uzee wangu, maana kula na tafuna kabisa mfupa ukiwa bado na meno mdomoni, hapa maana yangu nikufanya kazi kwa nguvu zote nakujiandaa kwa ajiri ya uzee!

Basi bwana, jana nikiwa pale Lindi hospitali ya Mkoa, Sokoine! Nikaona msururu wa magari yakipanda kwenda kule juu Mtanda! Polisi wa usalama barabarani wakizuia magari ili ule msafara uweze kupita! Basi bwana kuna jamaa akaniambia huyo ni Kikwete yupo hapa ana siku zaidi ya 3!

Leo asubuhi mida ya saa tano hivi,nikaanza safari yakurudi zangu Dodoma! Nikiwa njiani dereva aliona gari ya polisi inakuja kwa kasi mno,ikiashiria tupishe njia, bila hiyana dereva alipisha! Ukapita msururu wa magari yakiwa yanatembea kwa mwendo kasi sana!

Basi tukafika pale SOMANGA! Tukayaona yale magari yakiwa yamesimama kwa pembeni kuna watu wengi, nami nikatupa jicho nikamuona Mzee Kikwete akinunua samaki pale, sababu pale ni sehemu ya kula chakula,tukasimama pale,tukala na Mzee Kikwete aliingia hadi ndani ndani kabisa kununua samaki!

Basi sisi tukaanza safari tukawaacha wao pale, kabla hatujamaliza mpaka wa Lindi na Pwani, tulimkuta pale RPC wa Pwani akisubiri msafara ule aupokee na RPC wa Lindi arudi zake Lindi!

Sasa swali langu, kwa nini Mzee Kikwete ana msururu wa magari mengi vile?? Yaani zilikua gari zaidi ya 10! Na zote ni V8 VX na gari yake Nissan VX zile walizopewa marais wastaafu!
Muhimu alindwe maana anasagiwa kunguni mno bila sababu
 
Akatazwi kama gari zingine ni zake tu binafsi kwa ajili ya ulinzi, kuna visanii tu mkwala vina msafara wa magari kama 20 Na walinzi kem kem, sembuse raisi mstaafu
 
Kwa upumbavu huu ,nchi hii ina safari ndefu ya kujikomboa maana naona middle class karibu wengi wameoza kichwani, President Mandela baada ya kustaafu msafara wake haukuzidi 3 cars (including police sweep car)na hata wakati wanampeleka hospital, Ambulance yake ilipata breakdown na ilichukua muda msaada kumfikia,President H&H misafara yake haizidi 4 cars!,President CR misafara yake haizidi 4 cars, President wa Botswana msafara wake 3 cars!!,Tanzania tumekosea wapi?
Unaita wenzio wapumbavu Kwasababu umejawa na propaganda.
 
Back
Top Bottom