Bususwa
JF-Expert Member
- Sep 30, 2021
- 429
- 1,011
Toka mwaka mpya umeanza nipo kusini mikoa ya Lindi na Mtwara napambana na maisha yangu yakujiandaa na uzee wangu, maana kula na tafuna kabisa mfupa ukiwa bado na meno mdomoni, hapa maana yangu nikufanya kazi kwa nguvu zote nakujiandaa kwa ajiri ya uzee!
Basi bwana, jana nikiwa pale Lindi hospitali ya Mkoa, Sokoine! Nikaona msururu wa magari yakipanda kwenda kule juu Mtanda! Polisi wa usalama barabarani wakizuia magari ili ule msafara uweze kupita! Basi bwana kuna jamaa akaniambia huyo ni Kikwete yupo hapa ana siku zaidi ya 3!
Leo asubuhi mida ya saa tano hivi,nikaanza safari yakurudi zangu Dodoma! Nikiwa njiani dereva aliona gari ya polisi inakuja kwa kasi mno,ikiashiria tupishe njia, bila hiyana dereva alipisha! Ukapita msururu wa magari yakiwa yanatembea kwa mwendo kasi sana!
Basi tukafika pale SOMANGA! Tukayaona yale magari yakiwa yamesimama kwa pembeni kuna watu wengi, nami nikatupa jicho nikamuona Mzee Kikwete akinunua samaki pale, sababu pale ni sehemu ya kula chakula,tukasimama pale,tukala na Mzee Kikwete aliingia hadi ndani ndani kabisa kununua samaki!
Basi sisi tukaanza safari tukawaacha wao pale, kabla hatujamaliza mpaka wa Lindi na Pwani, tulimkuta pale RPC wa Pwani akisubiri msafara ule aupokee na RPC wa Lindi arudi zake Lindi!
Sasa swali langu, kwa nini Mzee Kikwete ana msururu wa magari mengi vile?? Yaani zilikua gari zaidi ya 10! Na zote ni V8 VX na gari yake Nissan VX zile walizopewa marais wastaafu!
Basi bwana, jana nikiwa pale Lindi hospitali ya Mkoa, Sokoine! Nikaona msururu wa magari yakipanda kwenda kule juu Mtanda! Polisi wa usalama barabarani wakizuia magari ili ule msafara uweze kupita! Basi bwana kuna jamaa akaniambia huyo ni Kikwete yupo hapa ana siku zaidi ya 3!
Leo asubuhi mida ya saa tano hivi,nikaanza safari yakurudi zangu Dodoma! Nikiwa njiani dereva aliona gari ya polisi inakuja kwa kasi mno,ikiashiria tupishe njia, bila hiyana dereva alipisha! Ukapita msururu wa magari yakiwa yanatembea kwa mwendo kasi sana!
Basi tukafika pale SOMANGA! Tukayaona yale magari yakiwa yamesimama kwa pembeni kuna watu wengi, nami nikatupa jicho nikamuona Mzee Kikwete akinunua samaki pale, sababu pale ni sehemu ya kula chakula,tukasimama pale,tukala na Mzee Kikwete aliingia hadi ndani ndani kabisa kununua samaki!
Basi sisi tukaanza safari tukawaacha wao pale, kabla hatujamaliza mpaka wa Lindi na Pwani, tulimkuta pale RPC wa Pwani akisubiri msafara ule aupokee na RPC wa Lindi arudi zake Lindi!
Sasa swali langu, kwa nini Mzee Kikwete ana msururu wa magari mengi vile?? Yaani zilikua gari zaidi ya 10! Na zote ni V8 VX na gari yake Nissan VX zile walizopewa marais wastaafu!