Jaji Warioba ni Muongo au Msahaulifu?

Jaji Warioba ni Muongo au Msahaulifu?

Mwanadiwani na spins zako!
nimeuliza je Rasimu ya tume ni legal na legitimate?
1. kama ndio kwa nini mmefuta maoni ya wananchi?
2. kama hapana kwa nini mmetumia 80% ya document ambayo haina uhalali kuleta katiba pendekezwa? je ina derive legality na legitimacy toka wapi?

hujajibu umepiga njia za sungura tu zinazoelekea nowhere
 
Ndugu,

Hata mtu asiyefahamu kama hafahamu, hawezi kufahamu kama hafahamu.

Inawezekana UKAWA ni mmoja wa watu katika kundi ninalolisema!.

CCM kwenye siasa za Tanzania inapimwa kwenye sanduku la kura.

Kwa mara ya mwisho ilipimwa kwenye chaguzi za madiwani 27 na chaguzi za ubunge katika Jimbo la Kalenga na Chalinze.

Kuna vyama fulani baada ya kutumia helikopta 3 kwenye kampeni, vilijikuta vikiambulia madiwani 3 katika ya madiwani 27. CCM ilipata madiwani 24.

Kwenye uchaguzi katika jimbo la Kalenga, walitumia helikopta 1 kuambulia 20% ya kura zilizopigwa wakati CCM wakipata 79% ya kura.

Kwenye Jimbo la Chalinze waliamua kutumia magari na kuambulia 10.5% ya kura, wakati CCM ilipata 86.6%.

Hiyo ndiyo ''mental and intellectual leprosy'' ya CCM kwa mtazamo wako.

of course hata jambazi huwa anafurahia matunda ya kazi yake. jambazi atavunja benki na hata kutoa watu roho....mwisho wa siku anatambia ule utajiri.

but ana siku zake 40 tu, hazizidi hapo.
 
Mwanadiwani na spins zako!
nimeuliza je Rasimu ya tume ni legal na legitimate?
1. kama ndio kwa nini mmefuta maoni ya wananchi?
2. kama hapana kwa nini mmetumia 80% ya document ambayo haina uhalali kuleta katiba pendekezwa? je ina derive legality na legitimacy toka wapi?

hujajibu umepiga njia za sungura tu zinazoelekea nowhere
Ndugu Stefano Mtangoo,

Hakuna spins katika mada yangu!.

Tume ya Jaji Warioba ilikusanya maoni kama Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 inavyobainisha. Kazi ya kuchambua maoni ya wananchi na kuyaweka kwenye waraka unaoitwa Rasimu ya Katiba ilifanyika kulingana na utashi wao ndani ya msingi wa sheria. Kwa msingi huo, Ndiyo maana sheria ya Mabadiliko ya Katiba imeweka nguzo za kisheria katika msingi wa checks and balance ili kuhakikisha kile ambacho Tume ya Jaji Warioba haikukiweka au ilikiweka isivyo, basi kifanyiwe marekebisho, kifutwe au kiwekwe kingine kilichoko ndani ya maoni ya wananchi.

Checks and balance imeanzia kwenye Mabaraza ya Katiba, Bunge Maalum na wananchi wenye uwezo kisheria wa kupiga kura ya maoni.

Ikumbukwe kuwa, Tume ya Jaji Warioba ilipokea jumla ya maoni 772,211 kwa njia ya mdomo na maandishi kutoka kwa wananchi wapatao 351,664. Ielewe kuwa, siyo maoni yote ya wananchi yaliwekwa kwenye Rasimu ya Jaji Warioba.

Sheria iliweka msingi wa Checks and balance kwa maana ya kuwepo kwa Bunge Maalum ambalo litaipitia Rasimu ya Katiba A.K.A Waraka ili kufanya marekebisho kadri linavyoona inafaa. Ndiyo maana Bunge la Katiba liliamua kuongeza na kupunguza baadhi ya Sura au Ibara kadri lilivyoona inafaa.

Kwa sasa Checks and balance imebaki kwa wananchi kupitia Kura ya Maoni ambapo kama watadhani Katiba Inayopendekezwa imeingiza yale yenye manufaa kwa maisha yao, basi wataamua kuipigia Kura ya NDIYO. Kama watadhani kuna mapungufu, basi wataipigia Kura ya HAPANA.

Kitu cha muhimu lazima tuelewe kuwa, Katiba haiweza kuweka kila kitu anachokipenda mtu mmoja mmoja katika Taifa.

Uamuzi uko kwa wananchi ambao kila mwanachi ana kura moja katika sanduku la kura ya maoni.
 
Hivi mnajua kwamba wananchi wengi walitaka serikali ya majimbo lakini Mzee warioba akasema bado turn wachanga? Kapuuza maoni ya wananchi na kuweka aliyoyapeda yeye?
 
Mkuu Mwana Diwani, kumuita mtu wa rika la baba yako mzazi kuwa ni muongo!, ni ukosefu wa nidhamu!.

Warioba amekiri kama ni idadi ya ibara, then ni asilimia 81%, lakini ukija kwenye maudhui, ni ndio hiyo asilimia 20%!.

Hili la kura ya maoni, kiukweli mimi kwa upande wangu, nawashauri watu wote, tuipigie tuu kura za ndiyo hii "Bora Katiba!", kwa kutumia precedence ya zile kura za BMK, "zisipotosha, zitatosheshwa!", Ushauri huu nimeisha wapa rafiki zangu wote humu!.

UKAWA na Warioba kubalini matokeo, tuipigie wote kura ya Ndio!

Mchakato Huu wa Katiba, ni Umasikini Wetu!, Tujikubali..

Jee Wajua Kuwa Kura ya "Hapana" Kwa Katiba Mpya! Ni Kura ya

Pasco

Umesahau ulivyomshambulia Membe?

Mwanadiwani kauliwa swali, Jee, "Jaji Warioba ni Muongo au Msahaulifu?" Na katoa ufafanuzi kwanini kauliza hivyo, ulichosoma hukukielewa au umekurupuka tu?
 
Rudisheni maadili kwenye katiba acheni kubwela bwela ovyo, kwanini mnangania kufungua acc njee ya nchi wakati mnajua viongozi wakibanwa ni faida kwa nchi?

Katiba si msahafu. Maadili ni neno lenye wigo mpana, hata kupiga mke wa mtu na kuishi nae kama kimada ni Ukosefu wa maadili.

Sheria zinaweza tungwa kuhusu maadili ya uongozi bila kuathiri katiba yoyote ile.
 
Hivi leo kwenye tasnia mpya ya siasa, nani sio muongo na msahaulifu? Kaazi kweli kweli
 
Ndugu,

Hili ni jukwaa la kupashana habari na kuelimisha kwa hoja mbadala na siyo jukwaa linalopimwa kwa kiwango cha matusi na munkari!

Kwa faida yako, hii hapa chini ndiyo orodha ya wajumbe wa Kamati ya Uandishi wa Katiba Inayopendekezwa.

attachment.php

attachment.php

NOTE BANE:
Ieleweke kuwa wawakilishi wa kutoka vyama vya CUF na CHADEMA walijitoa kwenye Kamati ya Uandishi kutokana na sababu wanazozifahamu wao wenyewe!.


Mchakato mzima umeharibiwa na nyie ccm from the beginning no matter what drama mnayoicheza saizi haiwezi kuhalalisha upatikanaji wa katiba nzuri. Watu wanna elimu ya namna gani katiba bora yaweza kupatikana kwaiyo drama mnazozicheza apa tunawashangaa tu mnachukulia watu wote wajinga wa uandishi wakatiba. Watanzania wengi tumekuwa wajinga na waroho wa maslahi binafsi mtu kwavile tu unafaidika na system iliyopo upo radhi kuuita upuuzi, wizi kuwa ni haki no matter how you are educated. Mmetumia mwanya wa ukawa kutoka bungeni kupitisha upuuzi wenu na kupitisha katiba na watu 99% wa mlengo mmoja nisawa na wakristo wapitishe katiba ya kuongoza nchi pekee yao kisa tu waislamu wamesusia wakatoka nje. That is not democracy!! Kama ndugu yangu hauna elimu ya haya mambo nibora unyamaze kabisa kuliko kuandika hiki au chukua muda wako kusoma na kujifunza. Na elimu ya katiba haipatikani kwa kumsikiliza change au Sitta au warioba kasema nini ...read books and other sources.
 
MwanaDiwani kwa hiyo ndio majibu ya swlu langu hayo? No wonder katika siasa hakuna la maana ni blah blah.
 
Last edited by a moderator:
Hivi mnajua kwamba wananchi wengi walitaka serikali ya majimbo lakini Mzee warioba akasema bado turn wachanga? Kapuuza maoni ya wananchi na kuweka aliyoyapeda yeye?
Na BMK likatumia same illegitimate document, according to your post kupata katiba inayopendekezwa. What does that mean?
 
Warioba ni mnafiki na mpotoshaji sijui kichwani mwake kipi anachokiwaza zaidi lakini siku zinakimbia kwenda mbele yote haya tutayajua alichoficha moyoni mwake.

Karibu sana Bluepearl tar.16
 
MwanaDiwani kwa hiyo ndio majibu ya swlu langu hayo? No wonder katika siasa hakuna la maana ni blah blah.

Teh teh teh, huyu ndio alikuwa akiwaambia wananchi kule Tanga, "mnataka maji au katiba...?" Wananchi wakajibu majiiiiii
 
Last edited by a moderator:
kwanini kiongozi asiwajibishwe na wananchi,hapo tu mi nachoka na kuiona rasimu ya Sitta ni ya kikanyaboya
 
Umesahau ulivyomshambulia Membe?

Mwanadiwani kauliwa swali, Jee, "Jaji Warioba ni Muongo au Msahaulifu?" Na katoa ufafanuzi kwanini kauliza hivyo, ulichosoma hukukielewa au umekurupuka tu?
Mkuu FF, heshima kitu cha bure, sijatumia popote lugha ya machukizo!.

Jee wewe unaweza kumuuliza baba yako au maya yako, "Baba, hivi wewe ni muongo au msahaulifu?!". Kama huwezi, then huwezi kumuita muongo mtu yoyote wa rika la baba yako, hata kama huyo mtu ni muongo, kiukweli kabisa!.

Lugha za staha kuwasilisha ujumbe huo zipo tele!.

Huu ni muendelezo tuu wa kutaka kumdhalilisha baba wa watu!.

Pasco
 
MwanaDiwani kwa hiyo ndio majibu ya swlu langu hayo? No wonder katika siasa hakuna la maana ni blah blah.

Ndugu,

Inawezejana kwa mtazamo wako ikawa siasa na wanasiasa ni bla blah blah lakini haina maana pia kwa watu wengine ni blah blah.

Neno blah blah ni relative term mpaka hapo utakapo unyesho kigezo ulichotumia kufikia hitimisho.

Kitu ninachokielewa katika ulimwengu wa sasa, huwezi kuishi nje ya siasa kwa sababu siasa ndiyo inayobeba maisha yako ya kila siku.

Siasa mara nyingi hazijengeki katika sheria pamoja na kwamba, sheria hazina siasa.
 
Last edited by a moderator:
MwanaDiwani

Hamna kitu umeeleza hapo zaidi ya kujitahidi kufanya kitu kinaitwa MCHEZO WA UBONGO! Ok! labda tukuulize nikwanini kifungu kilichotaka viongozi wawajibishwe mmekitoa!!??
 
Last edited by a moderator:
Kila anayejarbu kumpinga warioba n fisadi au yeye na familia yake wananufaika na mfumo uliopo wa kidokoz, cku ile ya kongomano alianza kueleza maudhui ya ilani yenu ccm(co katiba) huku akiunganisha na maneno ya mwl jk mkaanza kumzomea, yan laiti msingeleta vurugu ungejua nin maana ya maudhui, make unaonekana hujui maana ya maudhui
 
kama ni lazima zitotesheshwe,why usiwashauri ccm wakaitangaza katiba Yao kuwa katiba ya nchi badala ya kuteketeza mabilioni ya fedha kuandaa Kura ya maoni fake

Wanufaikaji wahayo mabilioni yanayoteketea ni wao wenyewe unaoana priority zao vikao visivyo tija, safari, wakati wanajua hospitali hazina dawa wala vifaa vyakutosha viongozi hawa wanaendesha nchi kwa manufaa yao bila aibu,mwanadiwani anaposifia madudu ya dodoma anajua wapiga kura wanauwezo gani wa kuchambua mambo kwa kina ndiyo maana mwenyekiti wao ametangaza sikuya kupiga kura na muda wa kampeni akitegemea utawanufaisha,mwanadiwani atoe maelezo mbunge kutokuwa waziri au mjumbe kwenye bodi kuna uhusiano gani na serikali mbili?,kufungua akaunti nje kunauhusiano upi na serikali mbili?,ni aibu kuanzisha mchakato ghari kama huu wakati hamtaki mabadiliko na kutegemea hoja za kihuni kama hizi kuendelea kutawala,mwanadiwani atueleze ni kwanini mhuni mwenzie makonda yupo katikati ya sinema ya Warioba kushambuliwa na kusababisha mdahalo mhimu kama ule kuvunjika?.Nakama anahofu ya MUNGU tueleze kuhusu kura ya meghji na yule kiongozi wa nccr na kama bado kura za znz zinatosha au niubabe tu unatumika.uhuni wenu huo utaitumbukiza hiinchi kwenye matatizo makubwa.
 
Si mpaka wawe na hizo hoja, mimi mpaka leo sijaona hoja yao hata moja, naona wanahororoja na kubwabwaja bila mpango.

Mungu asaidie hili zoezi liishe maana watu wamekuwa biased mno na kusahau kuwa hii ni katiba ya watanzania. Mtu akiunga mkono ataitwa CCM na akipinga basi UKAWA. Huo sio sio mtazamo sahihi maana wapo pia ambao hawako kwenye makundi hayo mawili lakini ni watanzania na katiba inayoandaliwa ni yao.
 
MwanaDiwani

Hoja yako ya 2/3 kupatikana, tulikuuliza Meghji ameigaje kura, umekimbia. Sasa unakuja na hili la Warioba.
Nalo tutakujibu kwa kupitia majibu ya CCM

CCM wanasema maoni ya tume ya Warioba yana takwimu ambazo si za kweli. Ni kwa mujibu wa CCM na makada wake na ukitaka tutawataja kwa majina.
Sasa kama ni hivyo, wapi CCM wanaweza kutumia takwimu wasizo ziamini kuwa ni za kweli?

Pili, Je, vifungu 1 na 6 ambavyo ni moyo wa katiba vimejadiliwa? Kama hapana ni kwanini.

Tatu, Jaji Warioba kwa takwimu ambazo CCM hawazikubali alipendekeza muundo wa S3 kutokana na maoni ya wananchi.
Tueleze muundo wa S2 umependekezwa kwa maoni ya wananchi kupitia tume gani?

Tafadhali usiseme tume ya Sitta iliyohoji wafugaji na wakulima 37.
 
Back
Top Bottom