kisanganyakiswata
JF-Expert Member
- Jan 28, 2014
- 1,302
- 553
Mwanadiwani uchambuzi murua kabisa :
Ndugu,MwanaDiwani
Hamna kitu umeeleza hapo zaidi ya kujitahidi kufanya kitu kinaitwa MCHEZO WA UBONGO! Ok! labda tukuulize nikwanini kifungu kilichotaka viongozi wawajibishwe mmekitoa!!??
Either way, kama utakubaliana au kutokubaliana na uamuzi wa Kamati ya Uandishi, majibu utayaweka kwenye sanduku la Kura ya Maoni!Haki ya wapiga kura kumwajibisha Mbunge
Mheshimiwa Mwenyekiti,
Ibara hii inahusu haki ya wapiga kura kumwajibisha Mbunge. Kamati moja imependekeza Ibara hii ibaki kama ilivyo kwenye Rasimu ya Tume. Kamati saba zimependekeza Ibara hii ifutwe, na Kamati Nne zimependekeza marekebisho madogo ikiwemo kuwepo kwa haki ya wapiga kura kumwajibisha mbunge ambaye ameshindwa kuwasilisha au kutetea kero za wapiga kura wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti,
Kamati ya Uandishi baada ya kutafakari maoni hayo inapendekeza ibara hii ifutwe kwa kuwa, haki inayopendekezwa inaweza kutumika vibaya ikiwemo kumwekea vikwazo vya kiutendaji Mbunge aliyeko madarakani. Aidha, wapiga kura wanayo haki ya kumwajibisha kwa kutompigia kura Mbunge katika kipindi cha miaka mitano endapo wananchi wataona Mbunge anayewawakilisha hafai, wanaweza kumwajibisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti,
kwa kuzingatia mapendekezo hayo Kamati ya Uandishi inapendekeza Ibara hii ifutwe.
Mkuu FF, much respect kwa jibu lalo kwangu, japo mode wameifuta post yako, niliigongea thanks, na naona kwa vile imefutwa, nakushukuru sana!.Umesahau ulivyomshambulia Membe?
Ndugu,
Hakuna mchezo wa ubongo niliyofanya. Nimeeleza kama zilivyo hoja za Jaji Warioba katika uwanja wa siasa.
Kuhusiana na kifungu cha Wabunge kuwajibishwa, Tume ya Uandishi wakati ikiwasilisha Katiba Inayopendekezwa kwenye Bunge Maalum ilitoa ufafanuzi na kusema,
Either way, kama utakubaliana au kutokubaliana na uamuzi wa Kamati ya Uandishi, majibu utayaweka kwenye sanduku la Kura ya Maoni!