Kiranga, kwa mbali ningeweza kukubaliana na wewe ila kumbuka kwa kiongozi wa ngazi ya juu ndani CCM kufanya alilofanya Lowassa si rahisi. Wako viongozi wengi tu ambao kama wangekuwa na uhuru huo wangekuwa wameshatoka zamani lakini hawana ujasiri huo. Labda utauliza kwa nini hawana ujasiri huo na kwa nini Lowassa na Sumaye wameweza kuitosa CCM.
Kama unafuatilia bila shaka umeona mashambulizi yanayoelekezwa kwa Lowassa...ni kama vile Lowassa ndiye alibeba madhambi yote ya CCM na wakienda mbali wako wanaodai CCM sasa ni safi kwa sababu hiyo. Watu kama Warioba hawana ujasiri huo...Warioba alipojaribu kukomaa tu kutetea alichoamini ni katiba iliyozingatia maoni ya wananchi ulishuhudia yaliyomkuta hadi vijana waliodaiwa kuongoza mashambulizi dhidi wote wametunukiwa vyeo. Warioba mwanzoni aliamini ana wafuasi ndani ya chama ambao wangemtetea lakini akajikuta peke yake na timu yake.
Hivyo alipopigwa biti kidogo tu huyoo akasalimu amri, akanyamaza na sasa yuko kwenye timu ya Magufuli akiilaumu UKAWA kwa msimamo wao kuhusu katiba. CCM gave him an offer he couldn't refuse because he realized they held all the four aces! Kwa Lowassa sivyo, they don't hold all the four aces and if anything it is he who holds the trump card. To face Lowassa, the three Mwinyi, Mkapa and Kikwete have to join forces; in actual fact they must join forces in the hope thet together they cam weather the storm. Mpaka sasa Lowassa yuko kimya, anajua amewashika pabaya na ujio wa Sumaye umezidi tu kupigilia msumari kwenye jeneza.
Watu wame panic, si kidogo bali sana tu. Kuliko nchi iangukie mikononi mwa Lowassa, watafanya kila waliwezalo kuhakikisha hilo halitokei. Kwa sasa naishia hapa.