JokaKuu, kiukweli Jaji Joseph Sinde Warioba amejitahidi kwa nafsi yake kusimamia anachoamini lakini naomba tusisahau kitu kimoja, sisi sote ni binadamu. Kama binadamu tunayo mapungufu ila tunachozidiana ni kiwango tu cha uvumilivu na ustahimilivu katika kuyasimamia yale tunayoamini ndiyo sahihi. Ni wachache ambao kwa hivi sasa wanapitia wakati mgumu kama Warioba kwani kajikuta kama wasemavyo wazungu;
torn between a rock and a hard place.
Hii si mara ya kwanza huyu mheshimiwa anajikuta katika hali hiyo...hii inanirudisha miaka zaidi ya ishirini nyuma, 1995 wakati William Benjamin Mkapa anatangaza nia yake ya kuchukua fomu kugombea Uraisi mbele ya waandishi wa habari. Kushoto kwake alikaa Jenerali Ulimwengu na kulia kwake alikaa Joseph Sinde Warioba. Hebi jaribu kufikiria Warioba alijisikiaje ile siku Jenerali Ulimwengu ananyang'anywa uraia na serikali chini ya Benjamin William Mkapa.
Jaji Warioba alikaa kimya na hakutoa neno. Tuje 2015, wakati Jaji Joseoh Sinde Warioba anasulubiwa na vijana na wazee ndani ya CCM kwa kisa tu cha kujaribu kutetea alichoamini ni rasimu iliyowakilisha maoni ya wananchi aliyoitayarisha yeye. Watu alioamini wangejitokeza kumtetea na kusimama naye kidete katika jukumu alilojipa la kuzunguka mikoani kama alivyofanya wakati anakusanya maoni ya wananchi hawakujitokeza, walibana wakakaa kimya.
Tururdi tena nyuma kidogo hadi wakati kashfa zilizohusisha akaunti za Benki Kuu import/support na baadaye EPA, KAGODA na MEREMETA n.k. zimepamba moto. Jina la Warioba lilijitokeza kwa njia ya kampuni moja iliyoitwa
Mwananchi Gold na ingawa moto wake ulikuja kutulia, yawezekana majivu yake yalihifadhiwa kuja kutumiwa muda muafaka ukifika. Hakuna kiongozi yeyote wa juu ambaye hakuwa na doa ndani ya CCM na hii silaha imetumika sama kuwaziba mdomo wengi.
Tunapofika hapa ndipo kwangu watu kama Lowassa na Sumaye nawaita wajasiri...serikali ina mkono mrefu na hakuna sababu yoyote kwa nini mtu anayedaiwa kuwa fisadi wa mafisadi hadi leo yuko huru mtaani akitafuta kura aweze kupata ridhaa ya kuliongoza taifa hili! Watu wanakwenda mbali hadi kudai kuwa maadam kwa sasa kahamia upinzani, dhambi zote za viongozi wa taifa hili,
wa zamani na wa sasa hivi, kupitia CCM zimetakasika na sasa CCM ni safi!
Hapana iko namna.
Mpaka dakika hii nakaa najiuliza kilichomsibu Dr. W. P. Slaa lakini pamoja na kushangaa natambua kwamba hakuna binadamu aliye safi kwa asilimia 100%, hapana, huyo ni Mungu tu. Ndiyo maana mimi naunga mkono kwa asilimia 100% mabadiliko ikiwa na maana ya kuuondoa huu mfumo na kuingia mfumo mpya...mabadiliko ni mabadiliko na tukubali tusikubali Watanzania hivi sasa wanataka na wako tayari kwa mabadiliko na wengi wanapoamua, hakuna wa kuzuia.
Jaji Warioba alikuwa raw model wangu kama alivyokuwa Dr. Slaa lakini kama wahenga walivyosema kukubaliana kwa watu wawili au zaidi kwa kila kitu muda wote, lazima kutie shaka. Niliafiki misimamo yao katika nyakati fulani fulani lakini kwa hapa tulipo kama taifa naamini wamepotoka ama kwa hiari au kwa kulazimishwa na hali halisi. Jenerali Ulimwengu kama anapita humu bila shaka anakumbuka yaliyompata alipoanza kutofautiana na serikali ya Mkapa.
Kwa waliocheza mchezo wa draft, kuna kuingizwa king kwa nguvu.