Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma katika Utendaji

Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma katika Utendaji

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma, Jaji wa Mahakama ya Rufani,hakuwahi kuiangusha Serikali kwenye maamuzi yake. Tangu akiwa Mahakama Kuu,Jaji Juma aliilinda kwa nguvu zake zote Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Analipa fadhila kwa rafikiye Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Kiuweledi, Jaji Prof.Juma ni msomi washeria aliyebobea. Ana uwezo mkubwa sana. Lakini,maisha yanampokonya matumizi sahihi ya weledi wake. Ndivyo mambo yanavyotakiwa kuwa?!Akiwa Mkuu wa Kitivo cha Sheria,Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jaji Prof.Juma aliwahi 'kumsave' Wakili Msomi Ridhiwani Kikwete ambaye 'alidisco'. Alimsimamia kidete hadi akabaki nakumaliza masomo yake mwaka 2005 na kutunukiwa Shahada ya Kwanza ya Sheria.

Jaji Prof. Juma alianza kulipwa alichokifanya kwa Ridhiwani mwaka 2007 pale alipoteuliwa kweye Tume ya Kuchunguza Mauaji ya wafanyabiashara watatu maeneo ya Sinza. Tume hiyo iliyoundwa na Rais iliongozwana Jaji Kipenka Musa. Baadaye, Jaji Prof. Juma aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu mwaka 2008. Akiwa hapo,Shauri la uchaguzi kati ya Makongoro Mahanga na Fred Mpendazoe likaletwa mbele yake. Kila mtu anafahamu kilichotokea. Kwa kukumbuka tu,Mahanga aliibuka mshindi na CCM 'ikapeta'.

Mwishoni mwa mwaka jana,Jaji Prof.Juma alipandishwa cheo na kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani. Hapo ndipo lilipomkuta Shauri lililotolewa uamuzi jana:Shauri la Aeshi Hilary dhidi ya Norbert Yamsebo. Mlitegemea matokeo tofauti? Ingawa shauri la Yamsebo lilisikilizwa na jopo la Majaji watatu: Jaji Edward Rutakangwa, Jaji Stephen Bwana na Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma, bado Jaji Juma alikuwa na nafasi yake kubwa katika shauri hilo.

Tasnia ya sheria inafanana na ya jeshi. 'Mdogo' hutumwa na kutumikia zaidi. 'Seniority' ndio kila kitu. Kwa 'ukubwa' katika jopo hilo, Jaji Rutakangwa anaanza,halafu Jaji Bwana na tena Jaji Prof. Juma. Hivyo basi, kazi kubwa ilifanywa na Jaji Prof. Juma. Mwenye kuamini na aamini. Majaji wawili waliobaki wao 'wali-vet' kilichoandaliwa na Jaji Prof. Juma.

Sina mashaka na uwezo wa Jaji Prof. Juma. Nina mashaka na mahusiano yake na mkuu wa Serikali na chama. Kwa mahusiano hayo, CHADEMA waweza kufurukuta mbele ya Jaji huyu? Sidhani. CHADEMA watakuwa wanapiga mwereka mbele yake kila shauri. Labda aamue kutumia weledi wake ipasavyo.

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dares Salaam(sasa Dodoma)

 
sio kweli, majaji wanapo kaa full benchi kwenye uamuzi kama mmoja hajaridhia anaunwezo wa kukataa bila wenzake kumlazimisha( decending judge) kesi nyingi za Lord Denning alikuwa asipo ridhia na maamuzi ya wenzake anakataa. hakuna seniority pale. wacha kupotosha umma. unless kama interest zako zimeguswa na hukumu zake.
 
oyaaa hivi inakuaje pale unaposhinda kesi mahakamani!!HAKI imetendeka!!!! ukishindwa HAKI HAIJATENDEKA!!! na mlolongo mzima wa lawama kwa majaji - mkuu hii sio kwako tu ni kwa wote wanaoshindwa au kushinda kesi. Ila nikusifie kitu kimoja, kuwa una kila dalili ya kuwa mtunzi mzuri sana wa haditi za kusimulia kwani unajua kupangilia vizuri matukio kuendana na mhusika!!! unaweza kupunguza umasikini ukijikita upande huo zaidi kwa kuandika vitabu!! labda kama utaamua kutumia ujuzi wako vibaya kama ambavyo naona hapo juu kwenye post yako!! LABDA Niulize tena Unachotaka sisi wasomaji tuelewe na hatuelewi au tuchangie ni nini kwenye post yako? ........
 
kichaa mimi naamini siyo lazima avue nguo mtu anaweza kuwa na nguo na haiba nzuri lakini ndani yake ukakuta matatizo makubwa sana,tunaishukuru jf kwa kubuni forum hii ya watu kuzungumza na kuonesha mawazo yao hii inasaidia kujua utu wa watu ulivyo,wapo wanaotukana bila sababu na wengine kuchochea chuki kama za kidini na zingine nyingi .
 
Ni mara chache mahakama ya rufaa imekuwa kinyume na serikali. Ingawa kesi hizi mbili ni chache kutosha kueleza kwa kina msimamo wa jaji Juma, bado si dalili nzuri juu ya (impartiality) yake hasa ukiangalia kesi ya Makongoro iliyokuwa straight forward
 
Kwa sie vilaza wa sheria kuna mazingira tunasema ni vizuri kukubali matokeo so long kuna kipindi pia mahakama hizo hizo zinatenda haki kwa upande mwingine usiokuwa wa serikali hasa ukizingatia mambo ya sheria wakati mwingine inategemea umeleta hoja zako vipi.
 
Jamani kwani haki iko upande mmoja tu, mie nafikili hata kushindwa ni haki pia. Mbona Lema alishinda hakukuwa na kelele?

Acheni uchochezi, haki ni kwa pande zote sio upande mwingine ukishinda basi umebebwa. Acheni kupandikiza chuki za ajabu.

Majaji wa Mahakama ya Rufaa ni Majaji makini na wenye weredi nchi hii inabidi ijivunie hilo. Jaji Prof Juma ni makini na hapindishi haki. Hakikisheni mkienda kwake muwe sawa kisheria na kufuata taratibu la sivyo hamtaambulia chochote pale sheria imelala mjipange sana na mungu ampe maisha marefu.

Huyo Ridhwani mnaemsema hamna ushahidi wowote mnaishi kwa hisia na majungu. Nashauri mpitie maamuzi ya mpendazoe na maamuzi ya aeshi mpate shule si kubwabwaja maneno tu hapa.
 
Bila kusahau Kesi ya Makongoro Mahanga na Mpendazoe ya ubunge wa segerea. Pamoja na Polisi kuthibitisha kwamba Mahanga alikimbia na masanduku ya kura na rafu nyingine za wazi. bado Mahanga alishinda iyo kesi ikiongozwa na Jaji Prof. Juma. Prof. Juma anajulikana na majaji wenzake kama ni "jaji wa ikulu".
 
Kwa vile shauri hili linahusiana na taaluma yako ya sheria haina maana kama unachokisema ni cha kweli.

Kwa kifupi, unaitumia taaluma yako vibaya nani kinyume kabisa cha misingi ya uanasheria.

Lazima uwe mkweli kama taaluma yako inavyokuasa. Hata kama unafikiria kugombea ubunge, jikite kwenye maswala halisia na siyo UDAKU kama huu ambao kila mara unaleta hapa JF.
 
Bila kusahau Kesi ya Makongoro Mahanga na Mpendazoe ya ubunge wa segerea. Pamoja na Polisi kuthibitisha kwamba Mahanga alikimbia na masanduku ya kura na rafu nyingine za wazi. bado Mahanga alishinda iyo kesi ikiongozwa na Jaji Prof. Juma. Prof. Juma anajulikana na majaji wenzake kama ni "jaji wa ikulu".

Mara nyingi hua ninazikubali sana report za bwana Tupa tupa, mzee wa Lumumba, mara baada ya kusoma hii comment yako nimeridhika pasipo shaka kwamba huyu jaji anatumika (kama ni kweli ndiye aliyehukum kesi ya Mpendazoe na Makongoro). Kama sikosei, kwenye ile hotuba ya Kikwete ya baraza la Idd mwaka juzi pale Dodoma nilisikia hili jina la huyu jaji kupitia kinywa cha Kikwete, I am starting to join the dots here! Anyway, hata hivyo CDM mwendo mdundo, 2015 sio mbali!
 
our court is a court of laws and equity......hukumu ya mpendazoe ilikua imejaa hearsay evidence na jaji Ibrahimu amelielezea hilo katika hukumu ile, mimi nakushauri uwe na tabia ya kuzisoma judgment vizuri na ikitokea hujaelewa mahali si vibaya kuuliza na siyo kulalamika, court of Appeal ina rules zake, hebu pitia zile rule vizuri na kama unaona kuna mashaka bado sheria inatoa nafasi kwa ajili ya revision/review.
 
Tasnia ya sheria inafanana na ya jeshi.‘Mdogo' hutumwa na kutumikia zaidi.'Seniority' ndio kila kitu. Kwa ‘ukubwa'katika jopo hilo,Jaji Rutakangwa anaanza,halafu Jaji Bwana na tena Jaji Prof.Juma. Hivyo basi,kazi kubwa ilifanywa na Jaji Prof.Juma. Mwenye kuamini na aamini. Majaji wawili waliobaki wao ‘wali-vet' kilichoandaliwa na Jaji Prof.Juma.
Hii siyo kweli, Jaji anaweza asikubaliane na wenzake.Rejea kesi ya Wakili Julius Nyanabo dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo Jaji Natalia Kimaro alitoa 'dissenting ruling' na kuwa na uamuzi tofauti na Majaji wenzake( Jaji Kyando na Jaji Ihema).
 
Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma, Jaji wa Mahakama ya Rufani,hakuwahi kuiangusha Serikali kwenye maamuzi yake. Tangu akiwa Mahakama Kuu,Jaji Juma aliilinda kwa nguvu zake zote Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Analipa fadhila kwa rafikiye Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Kiuweledi, Jaji Prof.Juma ni msomi washeria aliyebobea. Ana uwezo mkubwa sana. Lakini,maisha yanampokonya matumizi sahihi ya weledi wake. Ndivyo mambo yanavyotakiwa kuwa?!Akiwa Mkuu wa Kitivo cha Sheria,Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jaji Prof.Juma aliwahi 'kumsave' Wakili Msomi Ridhiwani Kikwete ambaye 'alidisco'. Alimsimamia kidete hadi akabaki nakumaliza masomo yake mwaka 2005 na kutunukiwa Shahada ya Kwanza ya Sheria.

Jaji Prof. Juma alianza kulipwa alichokifanya kwa Ridhiwani mwaka 2007 pale alipoteuliwa kweye Tume ya Kuchunguza Mauaji ya wafanyabiashara watatu maeneo ya Sinza. Tume hiyo iliyoundwa na Rais iliongozwana Jaji Kipenka Musa. Baadaye, Jaji Prof. Juma aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu mwaka 2008. Akiwa hapo,Shauri la uchaguzi kati ya Makongoro Mahanga na Fred Mpendazoe likaletwa mbele yake. Kila mtu anafahamu kilichotokea. Kwa kukumbuka tu,Mahanga aliibuka mshindi na CCM 'ikapeta'.

Mwishoni mwa mwaka jana,Jaji Prof.Juma alipandishwa cheo na kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani. Hapo ndipo lilipomkuta Shauri lililotolewa uamuzi jana:Shauri la Aeshi Hilary dhidi ya Norbert Yamsebo. Mlitegemea matokeo tofauti? Ingawa shauri la Yamsebo lilisikilizwa na jopo la Majaji watatu: Jaji Edward Rutakangwa, Jaji Stephen Bwana na Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma, bado Jaji Juma alikuwa na nafasi yake kubwa katika shauri hilo.

Tasnia ya sheria inafanana na ya jeshi. 'Mdogo' hutumwa na kutumikia zaidi. 'Seniority' ndio kila kitu. Kwa 'ukubwa' katika jopo hilo, Jaji Rutakangwa anaanza,halafu Jaji Bwana na tena Jaji Prof. Juma. Hivyo basi, kazi kubwa ilifanywa na Jaji Prof. Juma. Mwenye kuamini na aamini. Majaji wawili waliobaki wao 'wali-vet' kilichoandaliwa na Jaji Prof. Juma.

Sina mashaka na uwezo wa Jaji Prof. Juma. Nina mashaka na mahusiano yake na mkuu wa Serikali na chama. Kwa mahusiano hayo, CHADEMA waweza kufurukuta mbele ya Jaji huyu? Sidhani. CHADEMA watakuwa wanapiga mwereka mbele yake kila shauri. Labda aamue kutumia weledi wake ipasavyo.

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dares Salaam(sasa Dodoma)


Mkuu VUTA-NKUVUTE, a.k.a Tupa Tupa, kwa sisi tuliopitia mikono ya Dr. Juma tunaufahamu uadilifu wake fika!. Kwa waliopita UD wanajua kuna technical disco na ku disco kwa ukilaza!.

Hata mimi pia nilisoma UD na nilidisco wakati Dr. Juma akiwa dean!. Kiukweli wale watakaomshutumu kwa lolote, wanajichumia dhambi bure!. Ni sawa na Prof. Shivji au Fimbo awe Jaji halafu atoe rulling ya haki in favour of serikali useme analipa fadhila!.

Kwa sababu tumepoliticise kila kitu, uamuzi wowote in favour of Chadema then huo ndio uamuzi wa haki!. Uamuzi wowote in favour of CCM ni upendeleo!.

Paskali.
 
Kama ni hayo ya kutaka haki ya upande mmoja ni tatizo haki ni pande zote. Basi na U professa kwa wenye akili ndogo waseme amepewa na Serikali.

Kesi ya Mpendazoe hakuna askari aliefika kutestify mbele ya mahakama kuwa aliona masanduku wala kumuona Makongoro akiwa amekamatwa.

Uongo, someni maamuzi hayo. Askari mkuu wa kituo cha buguruni alitoa ushahidi wake na kusema hakukua na tukio kama hilo. Mashahidi wa mpendazoe walipishana hata kutaja hesabu ya masanduku mangapi yaliibiwa. Hakukua hata na ushahidi wa RB na wala askari yupi alimkamata.

Mwandishi wa habari wa gazeti alieandika habari ya kuibiwa kura hizo na makongoro alifika na kusema alichoandika alisikia watu PURE wakisema. HEARSAY EVIDENCE. Kwa mtindo huu wa majungu kama haya na kutosoma na kuelewa mtapotosha sana umma. \

Acheni majungu SOMENI na msiwe wajinga.
 
Back
Top Bottom