Kwa sababu tumepoliticise kila kitu, uamuzi wowote in favour of Chadema then huo ndio uamuzi wa haki!. Uamuzi wowote in favour of CCM ni upendeleo!.Pasco.
Tatizo tutatibu dalili za maradhi badala ya maradhi yenyewe.
Kutoaminiana hadi kufikia vyombo vya sheria kutiliwa shaka ni hatua ya kusikitisha.
Hata hivyo kuna sehemu mbili za kujadili
1. Vyombo vya sheria:
Kumekuwepo na mtazamo usiopendeza juu yake
Hili linachangiwa kwa sehemu na vyombo vya sheria ''kupoteza'' nguvu kama mhimili
Matukio yanayoendelea hasa ya siasa yanatia shaka hata pasipohitaji shaka
Kwa maneno mengine, trust na vyombo vya kutoa sheria ipo tofauti na matarajio
2. Hatuwezi kupata suluhu ya jambo hili hadi tutakapobadili mfumo
Jaji mkuu anapaswa kupitia katika 'vetting' nyingine
Nchi za wenzetu mtu akiwa Jaji, kwanza hawezi kuondolewa, pili anawajibika maeneo mengine si kwa eneo moja
Kwa mtazamo huo hakuna mhimili 'uliozama' zaidi chini, na yote inakuwa huru
Tuangalie hili la Jaji wa sasa. Wadhifa wake anakaimu Ujaji mkuu hadi uteuzi kamili
Hii si nafasi ya kukaimu, si kuwa inamkwaza mhusika, inajenga mashaka bila ulazima.
Jaji kwa kukaimu anakuwa na conflict of interest.
Kulinda masilahi ya taasisi lakini kama binadamu naye ana matarajio binafsi
Likitokea jambo maamuzi ya Jaji yataweza kuunganishwa na 'ukaimu'
Kwavile mfumo wetu ni mbovu, unatoa fursa tu ya mteuzi kuamua lini afanye hivyo
Hivi Jaji Othman aliamka tu na kutoa taarifa au kulikuwa na taarifa siku nyingi?
Kwanini nafasi ya Ujaji mtu akaimu?
Kwa umuhimu wake katika nchi na utawala hili linatokeaje?