Jaji mstaafu hajui TZ ina mikoa mingapi?

Hata mimi kwa kweli sina hakika kuna mikoa mingapi maana nasikia kuna Njoluma, Geita, Shimiyu, naskia na kwa Pinda kuna mkoa hata sina hakika na jina la mkoa wenyewe. Ni ngumu kujua kwa kweli hasa ukizingatia si mikoa yote yenye uongozi ngazi ya mkoa (RC, RPC, nk.)
 
Kwa kumbukumbu zangu tanzania bara ina mikoa 20. Zanzibar mikoa 5.

Hi ni data za zamani sana, za kipindi cha Mzee Ruksa, maana Mkapa alishaongeza mmoja, unaitwa Manyara. JK kaongeza kadhaa ambayo idadi yake ndo bado inatuchanganya. Maana nasikia wengine ndo kwanza wanagombea makao makuu yawe wapi!!!!
 
Unaona hata we unavyochemka, hy njoluma haipo nni Njombe na wala Mpanda haipo ni Katavi
 
Sikumshangaa sana maana ni vigumu kuijua mikoa na wilaya zinazoundwa kama zawadi kwa wanasiasa! Ni juzi tu umeundwa mkoa wenye wilaya mbili! Nani ataweza kukumbuka vitu kama hivyo?

hata mimi sijui maana kila leo kuna mabadiliko utafuatilia vingapi jamani. Msimlaumu, angalia kazi aliyopewa atifanya vema? CCM haitam-corrupt akatoa maamuzi kama ya mgombea binafsi!!!
 
Si uzee kila siku watu wanagawa mikoa kwa maslai ya kisiasa ni ngumu kujua hata kwa watoto wetu wanaosoma
 
Chaajabu hapo nini maana mikoa na wilaya zake kila mwaka kama si siku inaongezeka. Hapo hapaswi kulaumiwa hata baadhi watu wengi tu hawajui idadi ya mikoa.
 
Nimeshangaa nimemsikia jaji mkuu mstaafu Agustino Ramadhani BBC anasema 'Tanzania ina mikoa 22 sijui 23' My take: sikufurahia kwa mkubwa huyu kushindwa kuweka kichwani mambo ya msingi kama hili; uzee nao tatizo tunahitaji hata tume kuzingatia kuwa na vijana zaidi kuliko wazee
Nadhani ni rahisi kuchanganya, hasa kunapotokea uongezaji wa mikoa na wilaya kila siku.
 
mikoa ianyojilikana ni 26, hiyo ambayo hata mipaka haijawekwa wala haiko katika ramani rasmi ya Tanzania sio mikoa bado
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
....mwenyewe sijui!

Miaka yote nilikuwa najua mikoa ishirini bara, mitano visiwani,..sasa naskia kuna mkoa wa Manyara,
mkoa wa Rukwa, ....sijui ingekuwaje mawaziri wakuu waliopita nao wangetuwekea mikoa mipya ya
Monduli, Mwanga nk....
 
Nimeshangaa nimemsikia jaji mkuu mstaafu Agustino Ramadhani BBC anasema 'Tanzania ina mikoa 22 sijui 23' My take: sikufurahia kwa mkubwa huyu kushindwa kuweka kichwani mambo ya msingi kama hili; uzee nao tatizo tunahitaji hata tume kuzingatia kuwa na vijana zaidi kuliko wazee

Mimi mwenyewe sijuhi Tz ina mikoa mingapi kwa sasa ..naona kila kukicha mikoa na wilaya zinaongezeka.
JeTz ina mikoa mingapi? ,seriously!!
 
Nimeuliza tu wala msinitemee cheche, angalau ukijua ilikuwa 25 kabla kuongezewa mmoja na baadaye Simiyu,Geita,Njoluma na Mpanda. Lakini kusema 22 sijui 23 lazima nishangae!
Wrong..hakuna Njoluma ila upo mkoa wa Njombe na hakuna Mpanda ila mkoa wa Katavi. You see...usishangae Mtu kukosea haya mambo siku hizi...
 
Mi mwenyewe cjui labda unisaidie nisije nikaaibika mbele ya mwanangu.
 
Kwani wewe mwenyewe unajua ipo mikoa mingapi?

Kama unajua tutajie hapa bila ku-consult vyanzo vingine vya habari

JK mwenyewe ukimkurupusha kwa swali umuulize kuna mikoa mingapi ... mwenyewe hajui!

29 - Simuyu + Geita + Njombe + Katavi = 25
 
unamshangaa kwani yeye waziri wa tawala za mikoa?
ningemshangaa kama angesema hajui mfumo wa mahakama tanzania lol
 
Siyo mbaya ningemsikia akisema 25 au 26 ukiacha hii mipya 4: lakini 22/23 siyo kabisa. Kwa kizazi cha dot com wewe ukiwa lawyer au surveyor bado unatakiwa kujua juujuu mambo ya kijamii na siasa pia
 
Back
Top Bottom