Jaji Mbarouk apelekwa uingereza kupata mafunzo

matokeo yote yanafutwa kuanzia A'LEVEL hadi DEGREE iliwahi kutokea kesi kama hiyo UDSM.
 
hakuna lolote wakuu hapo. hiyo kozi imetengenezwa kumuondoa mbarouk kwenye kesi ya lema kiana baada ya judiciary kuona kamanda lisu atakuwa m1 wa mawakili. zugaling ltd twaita hiyo.
 
Wakuu kwa wale ambao hawafahamu kile Lissu alichosema kuhusu huyu JA, soma hapa kwa umakini


JAJI WA RUFAA MBAROUK SALIM MBAROUK

Mbarouk Salim Mbarouk aliteuliwa kuwa Jaji wa Rufaa wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania mwaka 2008. Kabla ya uteuzi huo Jaji Mbarouk alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar. Sifa za mtu kuteuliwa kuwa Jaji wa Rufaa zimeainishwa katika ibara ya 118(3) ya Katiba: “Majaji ... wa Rufani watateuliwa na Rais, kwa kushauriana na Jaji Mkuu, kutoka miongoni mwa watu wenye sifa za kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ... zilizoainishwa katika Ibara ya 109 ya Katiba au kutoka miongoni mwa watu wanaoweza kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar kwa mujibu wa sheria zinazotumika Zanzibar na wamekuwa na sifa hizo kwa muda usiopungua miaka kumi na tano.”

Kwa mujibu wa Ibara ya 94(3) ya Katiba ya Zanzibar, 1984, “mtu hatoweza kuteuliwa kuwa Jaji au Kaimu Jaji wa Mahkama Kuu mpaka awe na shahada ya Sheria ya Chuo Kikuu kinachotambuliwa au Chuo cha aina hiyo; au awe au amewahi kuwa Jaji wa Mahkama zilizofanana na hii kwa kesi zote za jinai na madai katika Tanzania au sehemu yoyote ya Jumuiya ya Madola au Mahkama ya Rufaa kutoka Mahkama hizo; au awe Mwanasheria wa Zanzibar au Tanzania kwa kipindi kisichopungua miaka saba; au awe na uzoefu wa Jaji au mwanasheria kwa pamoja usiopungua miaka saba.” Jaji Mbarouk hajatimiza hata moja ya masharti hayo ya Katiba ya Zanzibar. Jaji huyu hana shahada yoyote ya sheria inayotambuliwa na mamlaka ya ithibati ya Tanzania kama inavyotakiwa na Ibara ya 109(7) ya Katiba. Jaji huyu ana stashahada ya juu ya sheria (Post Graduate Diploma in Law) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Shahada ya Uzamili ya Sanaa ya Chuo Kikuu cha nchini Uingereza.

Uteuzi wa Jaji Mbarouk kuwa Jaji wa Rufaa ulileta minong’ono mingi katika taaluma ya sheria kiasi kwamba marehemu Wakili Leopold Kalunga anasemekana kufungua shauri katika Mahakama Kuu ya Tanzania kutaka uteuzi huo utenguliwe. Hata hivyo, Wakili Kalunga alifariki kabla ya shauri lake kusikilizwa na kwa hiyo liliondolewa mahakamani. Aidha, monong’ono hiyo ilimfanya Jaji wa Rufaa Mbarouk kujiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambako bado ni mwanafunzi hadi ninapoandika Addendum hii.
 
Wakuu kwa wale ambao hawafahamu kile Lissu alichosema kuhusu huyu JA, soma hapa kwa umakini


JAJI WA RUFAA MBAROUK SALIM MBAROUK

Mbarouk Salim Mbarouk aliteuliwa kuwa Jaji wa Rufaa wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania mwaka 2008. Kabla ya uteuzi huo Jaji Mbarouk alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar. Sifa za mtu kuteuliwa kuwa Jaji wa Rufaa zimeainishwa katika ibara ya 118(3) ya Katiba: "Majaji ... wa Rufani watateuliwa na Rais, kwa kushauriana na Jaji Mkuu, kutoka miongoni mwa watu wenye sifa za kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ... zilizoainishwa katika Ibara ya 109 ya Katiba au kutoka miongoni mwa watu wanaoweza kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar kwa mujibu wa sheria zinazotumika Zanzibar na wamekuwa na sifa hizo kwa muda usiopungua miaka kumi na tano."

Kwa mujibu wa Ibara ya 94(3) ya Katiba ya Zanzibar, 1984, "mtu hatoweza kuteuliwa kuwa Jaji au Kaimu Jaji wa Mahkama Kuu mpaka awe na shahada ya Sheria ya Chuo Kikuu kinachotambuliwa au Chuo cha aina hiyo; au awe au amewahi kuwa Jaji wa Mahkama zilizofanana na hii kwa kesi zote za jinai na madai katika Tanzania au sehemu yoyote ya Jumuiya ya Madola au Mahkama ya Rufaa kutoka Mahkama hizo; au awe Mwanasheria wa Zanzibar au Tanzania kwa kipindi kisichopungua miaka saba; au awe na uzoefu wa Jaji au mwanasheria kwa pamoja usiopungua miaka saba." Jaji Mbarouk hajatimiza hata moja ya masharti hayo ya Katiba ya Zanzibar. Jaji huyu hana shahada yoyote ya sheria inayotambuliwa na mamlaka ya ithibati ya Tanzania kama inavyotakiwa na Ibara ya 109(7) ya Katiba. Jaji huyu ana stashahada ya juu ya sheria (Post Graduate Diploma in Law) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Shahada ya Uzamili ya Sanaa ya Chuo Kikuu cha nchini Uingereza.

Uteuzi wa Jaji Mbarouk kuwa Jaji wa Rufaa ulileta minong'ono mingi katika taaluma ya sheria kiasi kwamba marehemu Wakili Leopold Kalunga anasemekana kufungua shauri katika Mahakama Kuu ya Tanzania kutaka uteuzi huo utenguliwe. Hata hivyo, Wakili Kalunga alifariki kabla ya shauri lake kusikilizwa na kwa hiyo liliondolewa mahakamani. Aidha, monong'ono hiyo ilimfanya Jaji wa Rufaa Mbarouk kujiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambako bado ni mwanafunzi hadi ninapoandika Addendum hii.
mkuu nimekusoma ila kwa kifupi Lissu alitoautetezi uliokuwa umejitosheleza kabisa. JK inabidi aangalie kwa mapana hao wateule wake
 
Jamani mimi naomba kuuliza tu, hivi kama mtu aliferi form four baadaye akatengeneza cheti cha kijanja mpaka akapata Degree kihalali, hivi huyu kesi yake ikoje? naomba jibu kabla sijalipuwa bomu.

N:B, Mkumbuke miaka ya nyuma ulikuwa unaweza kufoji cheti cha form four na kuendelea na Elimu ya juu bila kukalili darasa, kwahiyo sitalajii swali kuhusu hilo.

Atashtakiwa kwa kesi ya kughushi cheti cha kidato cha nne. Haya lete hilo bomu na machozi a.k.a la kicheko
 
Ama kweli kama Mwl Nyerere akirudi atawatia viongozi hawa walopo madarakani viboko vingi sana,wanakurupuka tuu kuwekana katika kazi zinazohitaji ustaadi wa hali ya juu
 
Jamani mimi naomba kuuliza tu, hivi kama mtu aliferi form four baadaye akatengeneza cheti cha kijanja mpaka akapata Degree kihalali, hivi huyu kesi yake ikoje? naomba jibu kabla sijalipuwa bomu.

N:B, Mkumbuke miaka ya nyuma ulikuwa unaweza kufoji cheti cha form four na kuendelea na Elimu ya juu bila kukalili darasa, kwahiyo sitalajii swali kuhusu hilo.
Mkuu nijuavyo mimi ni kunyang'anywa kila kitu cha taaluma alichonacho kwa sasa sababu ndio kimepelekea yeye awe hapo haya
alipo sasa,sasa leta vitu mkuu
 
Hivi naomba kuuliza Mh January Msofe niaka yake inarudi nyuma??haiwezekani. Zaidi miaka 15 yeye yuko pale pale tu...Rufaa tu haina kikomo?
 
nondoz gani hiyo ya wiki moja
washaenda kibao marekani na uswizi lakini wakirudi hawabadiliki
mtindo ni ulele mazoea ni yale yale ya kuandika hukumu tatu kwa mwaka
na kuahirisha kesi kwa miezi 4 hadi 6 tena mention tu
Bila kuwa na tume huru ya kuchunguza utendaji kazi wa majaji tusitegemee kitu kipya.
 
Ina maana walikuwa wanafanya kazi bila credentials zinazotalikana? Tutahakikishaje kwamba walisimamia haki?
 
kwa nini wasiwapeleke kule Chuo Uongozi wa Mahakama cha Lushoto, Tanga ambapo wangepigwa msasa mzuri tu wa wiki moja kwa kutumia wataalam wetu kama kina majaji waliobobea wastaafu na hata kumwalika Mh. Tundu Lissu, Prof. Safari n.h badala ya kwenda wiki moja huko RIPA , Uingereza CHUO CHA UONGOZI WA MAHAKAMA - LUSHOTO kwa ajili ya customised - training Strategic and operational management, organisational development and capacity building huku RIPA hawajui mahitaji yetu watanzania.

Sasa Lushoto kuna shopping gani?
Allowance za waheshimiwa wakiwa Lushoto compared na wakiwa kwa Mama?
Na pia waheshimiwa hawa ngazi zao zimeishapita hivi vijikozi vya bongo.

Miaka 50 baada ya uhuru bado turudi kwa mkoloni kujifunza ethics?
 
Chini ya uongozi wa awamu ya nne, tasnia ya sheria imekuwa abused sana. Hayo ndiyo matokeo ya kuongozwa kiswahiliswahili.
 
Back
Top Bottom