Katika hali isiyo ya kawaida, jaji Moses Mzuna, anayesikiliza kesi ya kupinga matokeo ya Jimbo la Singida mashariki, leo asubuhi amemlazimisha mbunge wa Jimbo hilo, TUNDU LISSU- CHADEMA, apande Kizimbani. Awali baada ya kesi kuahirishwa jana, Tundu Lissu alisema atakuja na mashahidi wasiozidi watano. Hata hivyo asubuhi ya leo baada ya mahakama kuanza, Tundu Lissu alimwomba shahidi wake wa kwanza SHABAN HAMISI LYIMU kuingia kizimbani, lakini Jaji akakataa, na kumwamuru Tundu Lissu apande kizimbani.
maelezo ya awali ya Lissu ni haya,
Mimi naitwa Tundu Antiphace Mughwai Lissu,
Umri wangu kwa sasa ni miaka 44, nakaa Ikungi Singida, Dodoma na Dar es Salaam. Mimi ni Mbunge wa Jimbo la Singida mashariki, tangu siku matokeo ya uchaguzi yalipotangazwa 31/10/2010. Vile vile mimi ni wakili wa mahakama kuu na mahakama zilizo chini yake kasoro mahakama ya Mwanzo. Vile vile Mimi ni Mwachama wa CHADEMA, tangu 2003, tangu wakati huo mimi ni mkurugenzi wa sheria, na katiba makao makuu DSM. Mimi pia ndio mnadhimu Mkuu wa kambi rasmi ya upinzani, na waziri kivuli wa sheria na katiba. Niliwahi kuwa mwanachama wa CCM, katika miaka ile ambayo usipokuwa mwana CCM usingeruhusiwa kwenda Chuo Kikuu. Nililazimika kujiunga na CCM ili niweze kwenda Chuo kikuu. Niliacha kuwa mwananchama wa CCM siku niliposajiliwa kuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu Septemba 1991, tangu baada ya hapo nimekuwa katika siasa za upinzani................ Tutaendelea kuwajuza yote yanayojiri........... Mashahidi wote watatu wapo, na Lissu anataka kukamilisha mashahidi wote leo
maelezo ya awali ya Lissu ni haya,
Mimi naitwa Tundu Antiphace Mughwai Lissu,
Umri wangu kwa sasa ni miaka 44, nakaa Ikungi Singida, Dodoma na Dar es Salaam. Mimi ni Mbunge wa Jimbo la Singida mashariki, tangu siku matokeo ya uchaguzi yalipotangazwa 31/10/2010. Vile vile mimi ni wakili wa mahakama kuu na mahakama zilizo chini yake kasoro mahakama ya Mwanzo. Vile vile Mimi ni Mwachama wa CHADEMA, tangu 2003, tangu wakati huo mimi ni mkurugenzi wa sheria, na katiba makao makuu DSM. Mimi pia ndio mnadhimu Mkuu wa kambi rasmi ya upinzani, na waziri kivuli wa sheria na katiba. Niliwahi kuwa mwanachama wa CCM, katika miaka ile ambayo usipokuwa mwana CCM usingeruhusiwa kwenda Chuo Kikuu. Nililazimika kujiunga na CCM ili niweze kwenda Chuo kikuu. Niliacha kuwa mwananchama wa CCM siku niliposajiliwa kuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu Septemba 1991, tangu baada ya hapo nimekuwa katika siasa za upinzani................ Tutaendelea kuwajuza yote yanayojiri........... Mashahidi wote watatu wapo, na Lissu anataka kukamilisha mashahidi wote leo