Ochu
JF-Expert Member
- May 13, 2008
- 975
- 47
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, imemkamata mfanyabiashara Jack Pemba kutokana na madai ya kujipatia pesa kwa udanganyifu.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa Jack anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Kilwa Road tangu Jumapili (Juzi) na alifunguliwa jalada namba CD/IR/3657/2009.
Habari za kukamatwa kwa mfanyabiashara huyo zilitawala katika maeneo mbalimbali jijini kutokana na umaarufu wake hasa katika kumbi za starehe kutokana na tabia yake ya kumwaga fedha kwa wanamuziki na wapambe wake.
Alisema amekamatwa kutokana na kutuhumiwa kujipatia zaidi ya shilingi milioni 344 kwa njia ya udanganyifu kupitia Benki ya Exim ya Uingereza.
Pemba alifunguliwa kesi na kampuni moja ya Uingereza mwaka jana na alikuwa akitafutwa na polisi yeye na wenzake ambao bado wanasakwa, alisema Kova.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa Jack anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Kilwa Road tangu Jumapili (Juzi) na alifunguliwa jalada namba CD/IR/3657/2009.
Habari za kukamatwa kwa mfanyabiashara huyo zilitawala katika maeneo mbalimbali jijini kutokana na umaarufu wake hasa katika kumbi za starehe kutokana na tabia yake ya kumwaga fedha kwa wanamuziki na wapambe wake.
...Jack Pemba
Jana (Jumatatu) gazeti hili liliwasiliana na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum, Suleiman Kova ambaye alikiri kukamatwa kwa Pemba.
Alisema amekamatwa kutokana na kutuhumiwa kujipatia zaidi ya shilingi milioni 344 kwa njia ya udanganyifu kupitia Benki ya Exim ya Uingereza.
Pemba alifunguliwa kesi na kampuni moja ya Uingereza mwaka jana na alikuwa akitafutwa na polisi yeye na wenzake ambao bado wanasakwa, alisema Kova.