I've Reached the End of the Road

I've Reached the End of the Road

binafsi changamoto ninazokumbana nazo katika maisha, huwa nazigeuza na kua fursa muhimu sana ya kujipanga upya, kujisahihisha kujirekebisha, kujisahihisha na hatimae kuziconfront nikiwa very bold na kuhakikisha natoboa kikamilifu.
Sawa ule mkopo wangu vipi
In fact Neema na Baraka za Mungu hunipa nguvu zaidi na uhakika wa kufanikiwa katika kudeal na changamoto ngumu na nyepesi maishani 🐒
Pande hizi hua umenyooka 🤗ukirudi pande zile unaanza kuzingua🫥
 
Zaburi 23:1
[1]BWANA ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
(A Psalm of David.) The LORD is my shepherd; I shall not want.🐒
Yes,
hiyo ni mbinu ya uhakika mno ya kujikwamua katika kila aina ya mkwamo.

Ni rahisi mno yaani, ni kujipanga tu 🐒
 
Amen mtumishi
Jitahidi usimamie haki utakua gentlemen kweli🐒
wajibu wangu ni kueleza ukweli mtupu kwenye mambo ya msingi tu ndugu mdau,

hiyo siwezi acha kamwe na nitaifanya kazi hiyo kwa bidii mbaya sana aise 🐒
 
wajibu wangu ni kueleza ukweli mtupu kwenye mambo ya msingi tu ndugu mdau,

hiyo siwezi acha kamwe na nitaifanya kazi hiyo kwa bidii mbaya sana aise 🐒
Ngoja ni kuache jukwaa huru hili 🙏
 
Ngoja ni kuache jukwaa huru hili 🙏
Yes,
tena unipatie nafasi nzuri na tulivu ya kumpumzika, hatimae baadae mapema kesho nije na mawazo mapya bora zaidi na fikra mbadala nzito na za maana zaidi, dhidi ya hoja mahususi katika majukwaa mbalimbali humu JF.

nimefurahi sana na kwakweli nakushukuru sana kwa yote 🐒
 
Yes,
tena unipatie nafasi nzuri na tulivu ya kumpumzika, hatimae baadae mapema kesho nije na mawazo mapya bora zaidi na fikra mbadala nzito na za maana zaidi, dhidi ya hoja mahususi katika majukwaa mbalimbali humu JF.

nimefurahi sana na kwakweli nakushukuru sana kwa yote 🐒
🙏🙏🙏
 
Hivi mkuu tamuuuuu huwa unasumbuliwa na kitu gani hasa?
Hii sio mara ya kwanza mimi kukuona umejikatia tamaa
Asante kwa kujali,kueleza hapa nitaandika mpaka niwakere watu.I wish nikae nawe nikueleze kila kitu mwanzo mpaka mwisho,nadhani utanielewa kwanini nafikia hatua hizi.
 
Safari Yangu Kutoka Lilongwe Hadi Dar es Salaam: Je, Umewahi Kuwa na Imani Kali Kiasi Hiki? 😂 Noma sana

Mwaka fulani nilikuwa Malawi, mjini Lilongwe Wakati huo nilikuwa na miaka 14, naelekea kutimiza 15

Nilikuwa nimeenda likizo, ikafika muda wa kurudi Tanzania

Mama akanipa nauli na kuniambia:

Shika hii pesa vizuri, nenda ukate tiketi.
Kwa nini hakunisindikiza sitasema leo. 😅

Basi nikachukua begi langu lenye nguo chache na mkoba mdogo uliokuwa na pesa za nauli, pesa ya kula, pamoja na kibari changu cha kusafiria Malawi

Nikafika stand ya Lilongwe ambapo magari ya Dar es Salaam yalikuwa yanapatikana

Kipindi hicho kulikuwa na kampuni moja maarufu sana, Taqwa
Sasa sijui ilikuwa bahati mbaya, uzembe sielewi mpka leo nilipochunguza mkoba wangu nikakuta umepotea 😭

Pesa zote zimeenda
Kibari kimeenda
Nauli imeenda
Kila kitu kimepotea

Aisee nilichanganyikiwa vibaya sana. Nikalia mpaka macho yakachoka
Lakini jambo moja nililokuwa na uhakika nalo ni hili

Sirudi nyumbani
Na hii ni hata leo nikisema hapana ni hapana

Kwa sababu mama yangu alikuwa mkali sana
Nilijiona nikirudi kumwambia nimepoteza nauli basi hakuna rangi ningeacha kuona

Nikajiwaza🤔

Kati ya kukutana na mama au kuvuka mipaka bila pesa, bora nijaribu bahati yangu

Nikajikaza nikamfuata dereva
Nikamsalimia kwa heshima zote za dunia
Shikamoo

Akanijibu
Marahaba binti, unasemaje?

Hapo ndipo nilipoanzisha filamu yangu ya kwanza ya maisha Uongooo pro 🤣
Nikaanza
Mimi nilikuja Malawi kufanya kazi za ndani : Astghafirullah 🙌

Dereva aliposikia hivyo akasema
Hebu njoo huku kidogo
Tukakaa pembeni

Sasa hapo nikaanza kusuka hadithi ya uongo kwa kasi ambayo hata nikikumbuka nachoka maana uongo sio tabia yangu mtu muongo na mnafiki hawajaachana mbali

Nikamuambia bosi wangu ananitesa sana, nimeamua kukimbia na kurudi Tanzania lakini sina hata senti

Dereva akaniangalia, akaangalia sura yangu ya mtoto mtulivu, akasikitika

Akamwita konda

Wakakubaliana kunibeba bure.
Mimi ndani ya moyo nikasema:
Asante Mungu, operation usirudi kwa mama imeanza rasmi🤣
Safari ikaanza

Usiku ulivyoingia, konda naye akaingia kwenye shughuli zake akanisahau kabisa kuhusu chakula
😭
Lakini Mungu alikuwa mbele
Nilikaa karibu na kaka mmoja ambaye kila alichonunua alikuwa ananipa sehemu bila kuniuliza hata MashaAllah 😍

Nilikuwa nakula kama nimepewa huduma ya full board😂

Tulipofika Karonga polisi wa Malawi walikuwa wanakagua
Konda akaniambia
Shuka ujifiche kwanza he kasheshe
Nikashuka

Ukaguzi ukaisha
Yaani simple tu ikawa imeisha hiyoo
Nikapanda tena

Mpaka leo nikiikumbuka najiona kama nilikuwa kwenye mission ya siri 🤣
Lakini ni kasheshe la kweli lilikuwa
Linaendela nahisi ningefaa kwa ujasusi🤪
Konda akasema shuka
Sisi tutapita hapa rasmi, wewe shuka upande ule vuka kwa mtumbwi 🙄
Nikabaki namtazama

Mtumbwi? Mimi ambaye hata kuangalia maji kwa muda mrefu naogopa? 😭

Akanipa hela kidogo ya kuvukia
Nikakuta mzee wa mtumbwi yupo tayari kazini Inaonekana ni michongo yake
Nikapanda

Tukiwa katikati ya mto nikaanza kuona mbele polisi kama anatusubiri kabisa 😂😂😂 heh

Moyo ukaanza kwenda mbio kuliko mtumbwi

Nilipofika upande wa pili, kweli polisi akaniita
Umetoka wapi?
Malawi
Ulikuwa unafanya nini?
Hapo nikarudia script ile ile akili mtu wangu 🤭

Nilikuwa nafanya kazi za ndani, bosi ananitesa, nimekimbia 🤣
Akauliza kitambulisho
Hakuna
Kibari
Hakuna
Simu
Hakuna
Kila kitu kilikuwa hakuna😂
Yule polisi akaniangalia halafu akasema
Wewe mtoto una ujanja sana
Akaandika namba yake kwenye karatasi na kuniambia

Ukifika Dar nitafute🤣😒
Mimi nikasema sawa, lakini kichwani nilikuwa nawaza basi lisiniondokee tu
🤣
Nikakimbia mpaka sehemu niliyoelekezwa

Baada ya muda gari likafika
Nikapanda
Safari ikaendelea mpaka Dar es Salaam

Leo nikikumbuka hii safari, najiuliza nilikuwa na ujasiri au nilikuwa na hofu ya mama yangu? 😂😂😂

Mom S 🥹🙌

Kwa sababu uongo wote huo, mipango yote hiyo, kuvuka mipaka, mtumbwi, polisi na hatari zote hizo tena mtoto wakike mdogo baso sijakomaa sura katika ya majangili (wanaume jokes)

chanzo chake kilikuwa kimoja tu

Mama yangu alikuwa mkali mno! 😭😭
Lakini pamoja na yote

Mama, nakupenda sana ❤️ ila ukweli ni kwamba ulikuwa mkali mnoooo!
Kwanza hongera pili umenikumbusha kipindi natoka DRC kuja bongo,aisee ni km Hivi ,huu ujasiri huwa unakujaga na Mungu akuwepo
 
Back
Top Bottom