Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kama kuna mwananchi wa nchi hii (Jamiiforums) ambaye kifo chake (LifeBan) kilitingisha vyombo vya habari (Majukwaa) basi ni Dada/Kaka FaizaFoxy. Lakini haijajulikana ni nini hasa kilisababisha kifo chake. Mpaka sasa maelezo kuhusu kifo chake yanategemea zaidi porojo za mitaani na kwenye vile vikao vya ndani (Private Messages) vya vikundi mbalimbali.
Inawezekana FF yuko hai (Active in JF) lakini watu wanamhisi tu au wanamuona kama ni mzukule (Kupitia user name zingine) na wakati mwingine haileti Raha kujibishana na Mizukule. Kifo chake kimesababisha nadhani kupotea katika mazingira ya kutatanisha kwa Mohamed Said ambaye kwenye uchangiaji yeye na FF walikuwa kama pacha vile.
Ushauri wangu kwa wananchi wote (JF Members) tuishinikize serikali yetu (Moderators) iunde tume huru kuchunguza sakata hili la kifo cha FF. Na tume hiyo ihusishe wananchi wa kada zote bila kubagua na mtokeo yake yamwagwe humu bila ya kuvungavunga.
Napigania haki ya uhuru wa kutoa maoni unaohakikishwa na Katiba yetu!!
Inawezekana FF yuko hai (Active in JF) lakini watu wanamhisi tu au wanamuona kama ni mzukule (Kupitia user name zingine) na wakati mwingine haileti Raha kujibishana na Mizukule. Kifo chake kimesababisha nadhani kupotea katika mazingira ya kutatanisha kwa Mohamed Said ambaye kwenye uchangiaji yeye na FF walikuwa kama pacha vile.
Ushauri wangu kwa wananchi wote (JF Members) tuishinikize serikali yetu (Moderators) iunde tume huru kuchunguza sakata hili la kifo cha FF. Na tume hiyo ihusishe wananchi wa kada zote bila kubagua na mtokeo yake yamwagwe humu bila ya kuvungavunga.
Napigania haki ya uhuru wa kutoa maoni unaohakikishwa na Katiba yetu!!