ITV mmewakosea sana watanzania

ITV mmewakosea sana watanzania

Kwa taarfa yako hata redio one magazetini pamoja na kulisoma gazeti la Tanzania daima hawjagusa kabisa taarifa hiyo
 
Vipi channel nyingine zilionesha habari ya Lema?? Channel 10, Azam 2, Tv1, clouds tv na nyingine??
Kama sio kwa nn unawahukumu ITV tu?
 
Ukawa, acheni upuuzi, anzisheni TV na Radio zenu, kwani RUZUKU MNAPELEKA WAPI? kila siku mnachota ruzuku kwa ajiri ya kesi za kijinga
Wewe kwa akili yako unafikiri wapinzani hawataki kuanzisha TV na REDIO zao?!

Kwa akili yako unadhani kabisa Serikali za kiafrika zinaweza kuruhusu hilo?!

Tumia akili kufikiri..!
 
Nadhani muhimu ni chama kuanzisha vyombo vya habari vyake, redio, tv na magazeti
 
Diamond yuko sahihi kusema hategemei ITV wala EATV ......hahaaahaaa...just yu tube inatosha.
 
Tatizo kukaa ndani kwa Lema mliona ndio kutamuongezea umaarufu......

Sasa ametoka ndio kwanza watu wanampotezea....

Shida ni kutafuta Umandela uchwara kwa lazima.
 
Acha hisia za kitoto! Kwani habari hiyo ilikuwa na maslahi gani kwa taifa?
Taifa linaendeshwa na sera za vyama. Bila upinzani chama tawala hakitajua wapi kinapwaya sababu nyani haoni kundule.Inabidi jicho la nje kuweza ona. Jifunze wenzetu wanavyopokezana vijiti si mbali tu hata Kenya, Malawi, Zambia ni vijiti tu na maendeleo mbele kwa mbele sisi tutabaki kuimba wee namba one na push ups mpaka liamba wakati waliopatikana na vyeti vya bandia wapo bench ila mmoja wao Daudi anapeta kwa Malema. Watoto bado maabara hazina kemikali na zana nyingine hata gas inayozalishwa hapa nchini. Walimu wakiagiza pesa wanashtakiwa eti elimu bure. Mtajijuuu. Kumbuka wengi wa wanaojitambua wana maisha mazuri na wanataka kusaidia umma wa wasiojitambua ambao kila kitu ni bora liende. Mtajijuuuuuuu.
 
team wema aka ukawa hamuishi kulalama.Simuanzishe tv yenu mjioneshe kwa muda wote?
 
Huko tuendako watu watutumia zaidi mitandao yz kijamii kupata habari kuliko vyombo hivi vya habari ambavyo vinaonekana kutokizi malengo.

Media hizi zitaathirika kama jinsi mashirika ya Posta dunani lilivyoathiriwa na ujio wa simu za mikunoni kiasi kwamba utumaji wa barua siku hizi umepungua sana na wamebakiwa na huduma ya kushughulikia barua za kikazi tu(za maofisi,n.k) .

Huko tuendako watu watatumia zaidi clip za mitandaoni na maandishi kupitia mitandao kupashana habari kama ilivyo sasa.
Kuna watu wameacha kabisa kuangalia taarifa za habari siku hizi, wamehamia katika social media.
 
Tatizo kukaa ndani kwa Lema mliona ndio kutamuongezea umaarufu......

Sasa ametoka ndio kwanza watu wanampotezea....

Shida ni kutafuta Umandela uchwara kwa lazima.
Lema ni mbunge wa Arusha na wana Arusha walimind sana na wamekuwa naye. Wanasheria wa Ukawa wamepigana mpaka ametoka.
Ulitaka wafanye nini zaidi? Vyombo vya habari tanzania haviko huru hpa tunadai vyama vingi ila hatuna tofauti na urusi na china hata cuba kwa taarifa yako hasa kuanzia Nov.2015
 
.

Mkutano wa Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema (Mb) ambaye pia ni Waziri kivuli wa mambo ya ndani, habari yake sio tu kwamba haijapewa kipaumbele, Bali haijaoneshwa kabisa katika kituo cha televisheni cha ITV.Kuna taarifa kwamba kituo hicho na vingine vilionywa kutorusha taarifa hiyo.

Kituo cha televisheni cha ITV kimeonesha mapungufu makubwa mno kupata kutokea nchini Kwa Kutokuonesha habari ya Waziri Kivuli wa Mambo ya ndani, ambaye alikuwa Magereza Kwa zaidi ya miezi minne kwasababu ya kesi za kisiasa.

ITV mmeitia doa tasnia ya habari, mmeonesha mapungufu makubwa katika kuiishi demokrasia ambayo watanzania wanaipigania, na mmesahau kwamba vyombo vya habari ni wadau wakubwa wa demokrasia kwani bila demokrasia hata uwepo wenu kama wanahabari utakuwa mashakani.

Watanzania hawajawahi kukata tamaa, jua liwake, mvua inyeshe, mabadiliko ya kisiasa tutayafikia lazima, ambayo ndiyo msingi wa maendeleo yote.


ITV ilishapoteza mwelekeo
 
Back
Top Bottom