Israeli yaelekea kushindwa kuwamaliza na kuwateketeza kundi la Hamas kama walivyoahidi

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
Israeli yaelekea kushindwa kuwamaliza kwa kuwaua wapiganaji wa kundi la Hamas kama walivyoitangazia dunia.

Ni siku 90 (miezi mitatu) imepita tangu Israeli iingize majeshi yake ya ardhini ndani ya Ukanda wa Gaza huku wizara ya afya ya Gaza ikisema kuwa wapalestina wapato 22,000 wamepoteza maisha wengi wakiwa ni watoto, akina mama na akina mama wengine wakiwa wajawazito.

Israeli kwa upande wao imepoteza wanajeshi wapatao 175 huku wengine wapatao 129 kubaki kushikiliwa na kundi la Hamas.

Israeli ilianzisha kampeni ya mashambulizi ya anga kuwashughulikia Hamas baada ya wapiganaji wa kundi hilo wakitumia njia za juu kwa juu, ardhini na majini kuvunja uzio wa ulinzi na kuwaua raia wa Israeli wapatao 1200. Ilikuwa ni tarehe 7 mwezi wa October pale wapiganaji hao walipovuka mpaka sehemu ya kusini mwa Israeli kwenye mji huo wa Ashkelon.

Umoja wa mataifa umesema wapalestina wapatao milioni 2 wamepoteza makazi yao huku wengi wakikabiliwa na njaa kali. Hata upande wa Israeli katika mji wa Ashkelon wakazi wengi wameachwa bila makazi yaoo baada ya kuteketezwa kwa moto au kuharibiwa vibaya.

Stratejia ya Israeli katika vita hii na Hamas imegawanywa katika hatua tatu ya kwanza au Phase One ilikuwa ni kufanya mashambulizi makali ya anga. Mashambulizi hayo yamefanya uharibifu mkubwa wa miundombinu ikiwemo hospitali ya Al-Shifa na kuua wapalestina wengi khasa watoto, akina mama na wale wagonjwa na wengi akina mama wakiwa na ujauzito.

Lakini uharibifu wa mabomu katika hospitali kubwa katika Gaza ya Al-Shifa ulisababisha dunia kulaani kitendo hicho cha Israeli kushambulia hospitali hiyo huku jeshi la Israeli likidai kuwepo kwa kituo cha kuongozea mashambulizi ya Hamas yaani "Command Centre".

Mwezi Novemba Israeli ikakubali kusitisha mashambulizi na kubadilishana mateka ambapo Hamas wakawaachilia mateka 80 huku Israeli ikiwaachilia wafungwa wapatao 240 walokuwa wakishikiliwa katika magereza mbalimbali nchini Israeli. Nje ya makubaliano hayo pia mateka wapatao 25 wa kutoka nchini Thailand ambao walikuwa wakifanya kazi katika mashamba ya Israeli waliachiliwa na Hamas.

Baada ya kipindi cha kusitisha mapigano kuisha, mapema mwezi Disemba jeshi la Israeli likaanza hatua ya pili yaani "Phase Two" ya mapigano kwa kuingiza jeshi na vifaru ndani ya ukanda wa Gaza. Israeli iliita wanajeshi wake wa akiba (reservists) wapatao 300,000 na kuanza vita ya ardhini "Ground offensive" dhidi ya kundi la Hamas.

Hatua hii ndo hatua ngumu ambayo jeshi la Israeli limekumbana nayo ambapo wapiganaji wa Hamas wameweza kufanikiwa kuwaua wanajeshi wengi wa Israeli kwa kutumia njia ya kushtukiza adui "ambush", mjengo kwa mjengo au "urban warfare" na ile ya kuvizia au "asymmetric war" ambayo wapiganaji hawa hujificha katika majengo na kushambulia kifaru kinopita nje.

Ugumu wa hatua hii pia ni kitendo cha wapiganaji wa Huthi wa Yemen ambao wamezuia meli kadhaa ambazo zilikuwa zikipeleka mzigo wa silaha nchini Israeli. Algeria pia ilizuia meli moja ambayo ilikuwa na shehena ya silaha ilokuwa ikielekea Israeli. Marekani ambayo ni mshirika mkubwa wa Israeli imekuwa ikiwasaidia IDF (Israel Defence Forces) kwa kushambulia kambi za makundi ya Hamas na kundi la Huthi na pia kundi la Hezbollah lililoko upande wa kaskazini mwa Israeli kuingia nchini Jordan.

Kwa kuweka meli zake za kivita katika bahari ya Mediterranean, Marekani imeweza kukabiliana na wapiganaji hao wa kutoka Yemen, na pia hata nchini Iraq ambapo ni juzi tu wapiganaji kadhaa wanohusiana na Hamas waliuawa kwa makombora.

Iran ambayo ni wafadhili wakubwa wa makundi ya Hamas na Hezbollah mpaka sasa haijachukua hatua zozote za kujibu mashambulizi ya jeshi la Israeli dhidi ya mmoja wa makamanda wake Saleh Al Arouri. Al Aroui aliuawa pamoja na wapiganaji kadhaa wa Hamas kusini mwa mji wa Beirut kwa makombora. Kwa kujibu wa idara ya ujasusi ya Mossad, Arouri amekuwa akishiriki mipango mingi dhidi ya Israeli likiwemo shambulizi la tarehe 7 Octoba mwaka jana.

Mapema mwaka huu Israeli imeingia katika hatua ya tatu yaani Phase Three ambayo yahusisha vita iso na nguvu sana yaani "low intensity". Hatua hii yaweza kuonekana kuwa ni hatua iso na mwelekeo maalum au ulo wazi au Vague isoweza kusema kama Hamas imemalizwa nguvu zake au bado wana uwezo uleule ukizingatia kuwa eneo la Khan Yunis ambalo majeshi ya IDF yamo kwa sasa bado Hamas wameweza kurusha makombora hivyo kuonekana wana uwezo uleule wa tokea mwanzo.

Khan Yunis ni mji ulioko kusini mwa ukanda wa Gaza na ndio yaaminika kuwepo kwa mahandaki na njia nyingi za chini kwa chini. Pia yaaminika kuwa ndipo walipo mateka wa Israeli wanoshikiliwa na kundi la Hamas.

Pamoja na Israeli kufikia hatua hii ya tatu, bado imewaruhusu wanajeshi wake kurudi makwao kujumuika na familia zao wakionekana kuvuka mpaka wa Israeli na Gaza kurudi Gaza.

Mapema mwanzoni kwa vita hii, waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu aliahidi kuhakikisha kundi la Hamas likiteketezwa, kuvunja uwezo wake wa kijeshi na pia kuwaokoa mateka wake wote.

Leo hii miezi yaenda minne bado Israeli haijafanikiwa kuimaliza Hamas jambo linohatarisha Hamas kujitangaza washindi katika vita hii na kisha kuendelea na vita vyake dhidi ya Israeli kutokea pande zote za kaskazini na kusini mwa Gaza kwa maana kwamba majeshi ya Israeli sasa hivi yapo katikati ya Gaza (Mji wa Khan Yunis) na yamezungukwa.

Pia hali hii yaonyesha kwamba kunaanza kuonekana uwazi mkubwa kati ya malengo ya Israeli juu ya vita yake hii dhidi ya Hamas na hali halisi ya kinotokea ndani ya uwanja wa vita. Halikadhalika mauaji ya Arouri yanoaminiwa yamefanywa na Mossad (ingawa israeli haijakiri) yamewalazimisha wapiganaji wa Hamas kutoa kauli kwamba "watalipiza kisasi".

Jambo jingine kubwa ni hofu ya kutokea vita kubwa ya mashariki ya kati kati ya Lebanon Hezbollah na Hamas, wapiganaji wa Hauthi, wanamgambo wa Iran walioko nchini Iraq (Islamic Resistance) wenye makao yao makuu mjini Baghdad ambayo ilishambuliwa na makombora Marekani na wapiganaji wa ISIS walioko nchini Syria sehemu ya Bukamal.

Hofu hiyo pia yajiongeza zaidi pale Iran ilipoamua kutuma meli yake ya kivita iitwayo Alborz Destroyer kwenda katika mfereji wa Bab El Mandep ikiwa ni baada ya Marekani kushambulia wapiganaji wa Huthi wa Yemen.

Kwa kutambua hilo, Marekani wamemtuma tena Antony Blinken waziri wake wa mambo ya nje kwenda tena mashariki ya kati kujaribu kuishawishi Israeli namna ya kumaliza vita hii ambayo imekuwa ngumu kwake. Ikumbukwe kuwa bila msaada mkubwa wa Marekani kuzuia wapiganaji wa Huthi, na khasa Hizbollah wasijiingize katika vita hii,hali ingekuwa mbaya kwa Israeli.

Hivyo katika ziara zake hizo (hii ikiwa ni ya nne ndani ya miezi mitatu) Blinken amelenga kuishawishi Israeli khasa wale waisraeli wenye msimamo mkali na wanounda baraza la mawaziri la Benjamini Netanyahu kuachana na wazo la kuwahamisha wapalestina na kuwapeleka katika kambi za wakimbizi katika nchi jirani za kiarabu.

Hizbollah wahofiwa kuwa na silaha khasa makombora yanoweza kufika mjini TelAviv na miji mingine nchini Israeli na kusababisha maafa makubwa khasa miundombinu mingi ya kimkakati. Marekani imejaribu mara nyingi kuweka mapendezo katika umoja wa mataifa ili kuwazuia Hizbullah kutokuwepo mpakani na Israeli mipango ambayo imeshindwa. Mara ya mwisho Israeli kupigana na Israeli ilikuwa ni mwaka 2006 ambapo vita ile haikutoa mshindi.

Israeli leo kupitia waziri wake wa Ulinzi Yohav Gallant wametoa mpango wa kuitawala Gaza kijeshi huku wapalestina wakiishi ndani ya Gaza wakijitawala lakini bila uhuru wa kujiamulia mambo yao. Pia Hamas hawataweza kutawala Gaza,na Israeli itaratibu shughuli zote za kiutawala zitofanywa na uongozi wa Gaza chini ya wapelestina.

Gallant ametoa leo mpango huo uitwao "Vision for Phase 3 of the war" huku ikisemwa kuwa ni mpango aloubuni yeye binafsi na bado wahitaji kusomwa na kupitiwa na baraza la mawaziri na lile baraza la mawaziri la vita au War Cabinet. Hiyo ndo moja ya sababu kubwa Marekani wamemtuma Blinken haraka.

Ni dhahiri kuwa Israeli ipo katika kitendawili kikubwa cha ni namna gani waimaliza vita hii ama kwa kuendelea nayo hadi mwisho au kuishia katikati. Kuendelea kuwepo mjini Gaza kwaleta mfarakano zaidi kwa kuonekana bado waitawala Gaza na wapalestina hivyo kufifisha zaidi makusudio ya tokea mwanzo yanotaka kuwepo na mataifa mawili ya Israeli na Palestina.

Pia kuendelea kwa Israeli kuwepo Gaza ni kuendeleza chuki kutoka kwa Hamas na kuongeza idadi ya wapiganaji wa kipalestina ambao hawataki kuwaona waisraeli ndani ya Gaza.

Hivyo, kidogokidogo hali ya Israeli kushindwa kuhimili vita hii imeanza kujionyesha huku wanadiplomasia kadha wa kadha waliishauri Israeli ianze kufikiria kuondoa majeshi yake kutoka Gaza. Hii yaonyesha wazi kuwa Israeli yaelekea kushindwa vita hii ambayo imekwenda kinyume na mipango yake ya kijeshi dhidi ya kundi la Hamas.

Tusijeshangaa kuona wapiganaji hawa wa Hamas wakijitangazia ushindi lakini huku wakiendeelelea kupigana hali ambayo itapekelea Israeli kuchukua maamuzi magumu ambayo yatazidi kuifanya itengwe na mataifa mengi duniani.
 
Ilikuwa kosa kubwa kwa Israeli kuingiza jesh nsdani ya Gaza yanayotokea saivi ni maajabu kwa udogo wa eneo LA Gaza na uwezo wa jeshi la Israeli pamoja na washirika wake imekuwa jambo LA kushangaza sana kuwa bdo hawajawatoa hamas mashimoni
 
Israeli yaelekea kushindwa kuwamaliza kwa kuwaua wapiganaji wa kundi la Hamas kama walivyoitangazia dunia.

Ni siku 90 (miezi mitatu) imepita tangu Israeli iingize majeshi yake ya ardhini ndani ya Ukanda wa Gaza huku wizara ya afya ya Gaza ikisema kuwa wapalestina wapato 22,000 wamepoteza maisha wengi wakiwa ni watoto, akina mama na akina mama wengine wakiwa wajawazito.

Israeli kwa upande wao imepoteza wanajeshi wapatao 175 huku wengine wapatao 129kubaki kushikiliwa na kundi la Hamas.

Israeli ilianzisha kampeni ya mashambulizi ya anga kuwashughulikia Hamas baada ya wapiganaji wa kundi hilo wakitumia njia za juu kwa juu, ardhini na majini kuvunja uzio wa ulinzi na kuwaua raia wa Israeli wapatao 1200. Ilikuwa ni tarehe 7 mwezi wa October pale wapiganaji hao walipovuka mpaka sehemu ya kusini mwa Israeli kwenye mji huo wa Ashkelon.

Umoja wa mataifa umesema wapalestina wapatao milioni 2 wamepoteza makazi yao huku wengi wakikabiliwa na njaa kali. Hata upande wa Israeli katika mji wa Ashkelon wakazi wengi wameachwa bila makazi yaoo baada ya kuteketezwa kwa moto au kuharibiwa vibaya.

Stratejia ya Israeli katika vita hii na Hamas imegawanywa katika hatua tatu ya kwanza au Phase One ilikiwa ni kufanya mashambulizi makali ya anga. Mashambulizi hayo yamefanya uharibifu mkubwa wa miundombinu ikiwemo hospitali ya Al-Shifa na kuua wapalestina wengi khasa watoto, akina mama na wale wagonjwa na wengi akina mama wakiwa na ujauzito.

Lakini uharibifu wa mabomu katika hospitali kubwa katika Gaza ya Al-Shifa ulisababisha dunia kulaani kitendo hicho cha Israeli kushambulia hospitali hiyo huku jeshi la Israeli likidai kuwepo kwa kituo cha kuongozea mashambuliz ya Hamas yaani "Command Centre".

Mwezi Novemba Israeli ikakubali kusitisha mashambulizi na kubadilishana mateka ambapo Hamas wakawaachilia mateka 80 huku Israeli ikiwaachilia wafungwa wapatao 240 walokuwa wakishikiliwa katika magereza mbalimbali nchini Israeli. Nje ya makubaliano hayo pia mateka wapatao 25 wa kutoka nchini Thailand ambao walikuwa wakifanya kazi katika mashamba ya Israeli waliachiliwa na Hamas.

Baada ya kipindi cha kusitisha mapigano kuisha, mapema mwezi Disemba jeshi la Israeli likaanza hatua ya pili yaani "Phase Two" ya mapigano kwa kuingiza jeshi na vifaru ndani ya ukanda wa Gaza. Israeli iliita wanajeshi wake wa akiba (reservists) wapatao 300,000 na kuanza vita ya ardhini "Ground offensive" dhidi ya kundi la Hamas.

Hatua hii ndo hatua ngumu ambayo jeshi la Israeli limekumbana nayo ambapo wapiganaji wa Hamas wameweza kufanikiwa kuwaua wanajeshi wengi wa Israeli kwa kutumia njia ya kushtukiza adui "ambush", mjengo kwa mjengo au "urban warfare" na ile ya kuvizia au "asymmetric war" ambayo wapiganaji hawa hujificha katika majengo na kushambulia kifaru kinopita nje.

Ugumu wa hatua hii pia ni kitendo cha wapiganaji wa Huthi wa Yemen ambao wamezuia meli kadhaa ambazo zilikuwa zikipeleka mzigo wa silaha nchini Israeli. Algeria pia ilizuia meli moja ambayo ilikuwa na shehena ya silaha ilokuwa ikielekea Israeli. Marekani ambayo ni mshirika mkubwa wa Israeli imekuwa ikiwasaidia IDF (Israel Defence Forces) kwa kushambulia kambi za makundi ya Hamas na kundi la Huthi na pia kundi la Hezbollah lililoko upande wa kaskazini mwa Israeli kuingia nchini Jordan.

Kwa kuweka meli zake za kivita katika bahari ya Mediterranean, Marekani imeweza kukabiliana na wapiganaji hao wa kutoka Yemen, na pia hata nchini Iraq ambapo ni juzi tu wapiganaji kadhaa wanohusiana na Hamas waliuawa kwa makombora.

Iran ambayo ni wafadhili wakubwa wa makundi ya Hamas na Hezbollah mpaka sasa haijachukua hatua zozote za kujibu mashambulizi ya jeshi la Israeli dhidi ya mmoja wa makamanda wake Saleh Al Arouri. Al Aroui aliuawa pamoja na wapiganaji kadhaa wa Hamas kusini mwa mji wa Beirut kwa makombora. Kwa kujibu wa idara ya ujasusi ya Mossad, Arouri amekuwa akishiriki mipango mingi dhidi ya Israeli likiwemo shambulizi la tarehe 7 Octoba mwaka jana.

Mapema mwaka huu Israeli imeingia katika hatua ya tatu yaani Phase Three ambayo yahusisha vita iso na nguvu sana yaani "low intensity". Hatua hii yaweza kuonekana kuwa ni hatua iso na mwelekeo maalum au ulo wazi au Vague isoweza kusema kama Hamas imemalizwa nguvu zake au bado wana uwezo uleule ukizingatia kuwa eneo la Khan Yunis ambalo majeshi ya IDF yamo kwa sasa bado Hamas wameweza kurusha makombora hivyo kuonekana wana uwezo uleule wa tokea mwanzo.

Khan Yunis ni mji ulioko kusini mwa ukanda wa Gaza na ndio yaaminika kuwepo kwa mahandaki na njia nyingi za chini kwa chini. Pia yaaminika kuwa ndipo walipo mateka wa Israeli wanoshikiliwa na kundi la Hamas.

Pamoja na Israeli kufikia hatua hii ya tatu, bado imewaruhusu wanajeshi wake kurudi makwao kujumuika na familia zao wakionekana kuvuka mpaka wa Israeli na Gaza kurudi Gaza.

Mapema mwanzoni kwa vita hii, waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu aliahidi kuhakikisha kundi la Hamas likiteketezwa, kuvunja uwezo wake wa kijeshi na pia kuwaokoa mateka wake wote.

Leo hii miezi yaenda minne bado Israeli haijafanikiwa kuimaliza Hamas jambo linohatarisha Hamas kujitangaza washindi katika vita hii na kisha kuendelea na vita vyake dhidi ya Israeli kutokea pande zote za kaskazini na kusini mwa Gaza kwa maana kwamba majeshi ya Israeli sasa hivi yapo katikati ya Gaza (Mji wa Khan Yunis) na yamezungukwa.

Pia hali hii yaonyesha kwamba kunaanza kuonekana uwazi mkubwa kati ya malengo ya Israeli juu ya vita yake hii dhidi ya Hamas na hali halisi ya kinotokea ndani ya uwanja wa vita. Halikadhalika mauaji ya Arouri yanoaminiwa yamefanywa na Mossad (ingawa israeli haijakiri) yamewalazimisha wapiganaji wa Hamas kutoa kauli kwamba "watalipiza kisasi".

Jambo jingine kubwa ni hofu ya kutokea vita kubwa ya mashariki ya kati kati ya Lebanon Hezbollah na Hamas, wapiganaji wa Hauthi, wanamgambo wa Iran walioko nchini Iraq (Islamic Resistance) wenye makao yao makuu mjini Baghdad ambayo ilishambuliwa na makombora Marekani na wapiganaji wa ISIS walioko nchini Syria sehemu ya Bukamal.

Hofu hiyo pia yajiongeza zaidi pale Iran ilipoamua kutuma meli yake ya kivita iitwayo Alborz Destroyer kwenda katika mfereji wa Bab El Mandep ikiwa ni baada ya Marekani kushambulia wapiganaji wa Huthi wa Yemen.

Kwa kutambua hilo, Marekani wamemtuma tena Antony Blinken waziri wake wa mambo ya nje kwenda tena mashariki ya kati kujaribu kuishawishi Israeli namnaya kumaliza vita hii ambayo imekuwa ngumu kwake. Ikumbukwe kuwa bila msaada mkubwa wa Marekani kuzuia wapiganaji wa Huthi, na khasa Hizbollah wasijiingize katika vita hii,hali ingekuwa mbaya kwa Israeli.

Hivyo katika ziara zake hizo (hii ikiwa ni ya nne ndani ya miezi mitatu) Blinken amelenga kuishawishi Israeli khasa wale waisraeli wenye msimamo mkali na wanounda baraza la mawaziri la Benjamini Netanyahu kuachana na wazo la kuwahamisha wapalestina na kuwapeleka katika kambi za wakimbizi katika nchi jirani za kiarabu.

Hizbollah wahofiwa kuwa na silaha khasa makombora yanoweza kufika mjini TelAviv na miji mingine nchini Israeli na kusababisha maafa makubwa khasa miundombinu mingi ya kimkakati. Marekani imejaribu mara nyingi kuweka mapendezo katika umoja wa mataifa ili kuwazuia Hizbullah kutokuwepo mpakani na Israeli mipango ambayo imeshindwa. Mara ya mwisho Israeli kupigana na Israeli ilikuwa ni mwaka 2006 ambapo vita ile haikutoa mshindi.

Israeli leo kupitia waziri wake wa Ulinzi Yohav Gallant wametoa mpango wa kuitawala Gaza kijeshi huku wapalestina wakiishi ndani ya Gaza wakijitawala lakini bila uhuru wa kujiamulia mambo yao. Pia Hamas hawataweza kutawala Gaza,na Israeli itaratibu shughuli zote za kiutawala zitofanywa na uongozi wa Gaza chini ya wapelestina.

Gallant ametoa leo mpango huo uitwao "Vision for Phase 3 of the war" huku ikisemwa kuwa ni mpango aloubuni yeye binafsi na bado wahitaji kusomwa na kupitiwa na baraza la mawaziri nalile baraza la mawaziri la vita au War Cabinet. Hiyo ndo moja ya sababu kubwa Marekani wamemtuma Blinken haraka.

Ni dhahiri kuwa Israeli ipo katika kitendawili kikubwa cha ni namna gani waimaliza vita hii ama kwa kuendelea nayo hadi mwisho au kuishia katikati. Kuendelea kuwepo mjini Gaza kwaleta mfarakano zaidi kwa kuonekana bado waitawala Gaza na wapalestina hivyo kufifisha zaidi makusuduo ya tokea mwanzo yanotaka kuwepo na mataifa mawili ya Israeli na Palestina.

Pia kuendelea kwa Israeli kuwepo Gaza ni kuendeleza chuki kutoka kwa Hamas na kuongeza idadi ya wapiganaji wa kipalestina ambao hawataki kuwaona waisraeli ndani ya Gaza.

Hivyo, kidogokidogo hali ya Israeli kushindwa kuhimili vita hii imeanza kujionyesha huku wanadiplomasia kadha wa kadha waliishauri Israeli ianze kufikiria kuondoa majeshi yake kutoka Gaza. Hii yaonyesha wazi kuwa Israeli yaelekea kushindwa vita hii ambayo imekwenda kinyume na mipango yake ya kijeshi dhidi ya kundi la Hamas.

Tusijeshangaa kuona wapiganaji hawa wa Hamas wakijitangazia ushindi lakin ihuku wakiendeelelea kupigana hali ambayo itapekelea Israeli kuchukua maamuzi magumu ambayo yatazidi kuifanya itengwe na mataifa mengi duniani.
Hamas anachapika sana ...
 
Israeli yaelekea kushindwa kuwamaliza kwa kuwaua wapiganaji wa kundi la Hamas kama walivyoitangazia dunia.

Ni siku 90 (miezi mitatu) imepita tangu Israeli iingize majeshi yake ya ardhini ndani ya Ukanda wa Gaza huku wizara ya afya ya Gaza ikisema kuwa wapalestina wapato 22,000 wamepoteza maisha wengi wakiwa ni watoto, akina mama na akina mama wengine wakiwa wajawazito.

Israeli kwa upande wao imepoteza wanajeshi wapatao 175 huku wengine wapatao 129kubaki kushikiliwa na kundi la Hamas.

Israeli ilianzisha kampeni ya mashambulizi ya anga kuwashughulikia Hamas baada ya wapiganaji wa kundi hilo wakitumia njia za juu kwa juu, ardhini na majini kuvunja uzio wa ulinzi na kuwaua raia wa Israeli wapatao 1200. Ilikuwa ni tarehe 7 mwezi wa October pale wapiganaji hao walipovuka mpaka sehemu ya kusini mwa Israeli kwenye mji huo wa Ashkelon.

Umoja wa mataifa umesema wapalestina wapatao milioni 2 wamepoteza makazi yao huku wengi wakikabiliwa na njaa kali. Hata upande wa Israeli katika mji wa Ashkelon wakazi wengi wameachwa bila makazi yaoo baada ya kuteketezwa kwa moto au kuharibiwa vibaya.

Stratejia ya Israeli katika vita hii na Hamas imegawanywa katika hatua tatu ya kwanza au Phase One ilikiwa ni kufanya mashambulizi makali ya anga. Mashambulizi hayo yamefanya uharibifu mkubwa wa miundombinu ikiwemo hospitali ya Al-Shifa na kuua wapalestina wengi khasa watoto, akina mama na wale wagonjwa na wengi akina mama wakiwa na ujauzito.

Lakini uharibifu wa mabomu katika hospitali kubwa katika Gaza ya Al-Shifa ulisababisha dunia kulaani kitendo hicho cha Israeli kushambulia hospitali hiyo huku jeshi la Israeli likidai kuwepo kwa kituo cha kuongozea mashambuliz ya Hamas yaani "Command Centre".

Mwezi Novemba Israeli ikakubali kusitisha mashambulizi na kubadilishana mateka ambapo Hamas wakawaachilia mateka 80 huku Israeli ikiwaachilia wafungwa wapatao 240 walokuwa wakishikiliwa katika magereza mbalimbali nchini Israeli. Nje ya makubaliano hayo pia mateka wapatao 25 wa kutoka nchini Thailand ambao walikuwa wakifanya kazi katika mashamba ya Israeli waliachiliwa na Hamas.

Baada ya kipindi cha kusitisha mapigano kuisha, mapema mwezi Disemba jeshi la Israeli likaanza hatua ya pili yaani "Phase Two" ya mapigano kwa kuingiza jeshi na vifaru ndani ya ukanda wa Gaza. Israeli iliita wanajeshi wake wa akiba (reservists) wapatao 300,000 na kuanza vita ya ardhini "Ground offensive" dhidi ya kundi la Hamas.

Hatua hii ndo hatua ngumu ambayo jeshi la Israeli limekumbana nayo ambapo wapiganaji wa Hamas wameweza kufanikiwa kuwaua wanajeshi wengi wa Israeli kwa kutumia njia ya kushtukiza adui "ambush", mjengo kwa mjengo au "urban warfare" na ile ya kuvizia au "asymmetric war" ambayo wapiganaji hawa hujificha katika majengo na kushambulia kifaru kinopita nje.

Ugumu wa hatua hii pia ni kitendo cha wapiganaji wa Huthi wa Yemen ambao wamezuia meli kadhaa ambazo zilikuwa zikipeleka mzigo wa silaha nchini Israeli. Algeria pia ilizuia meli moja ambayo ilikuwa na shehena ya silaha ilokuwa ikielekea Israeli. Marekani ambayo ni mshirika mkubwa wa Israeli imekuwa ikiwasaidia IDF (Israel Defence Forces) kwa kushambulia kambi za makundi ya Hamas na kundi la Huthi na pia kundi la Hezbollah lililoko upande wa kaskazini mwa Israeli kuingia nchini Jordan.

Kwa kuweka meli zake za kivita katika bahari ya Mediterranean, Marekani imeweza kukabiliana na wapiganaji hao wa kutoka Yemen, na pia hata nchini Iraq ambapo ni juzi tu wapiganaji kadhaa wanohusiana na Hamas waliuawa kwa makombora.

Iran ambayo ni wafadhili wakubwa wa makundi ya Hamas na Hezbollah mpaka sasa haijachukua hatua zozote za kujibu mashambulizi ya jeshi la Israeli dhidi ya mmoja wa makamanda wake Saleh Al Arouri. Al Aroui aliuawa pamoja na wapiganaji kadhaa wa Hamas kusini mwa mji wa Beirut kwa makombora. Kwa kujibu wa idara ya ujasusi ya Mossad, Arouri amekuwa akishiriki mipango mingi dhidi ya Israeli likiwemo shambulizi la tarehe 7 Octoba mwaka jana.

Mapema mwaka huu Israeli imeingia katika hatua ya tatu yaani Phase Three ambayo yahusisha vita iso na nguvu sana yaani "low intensity". Hatua hii yaweza kuonekana kuwa ni hatua iso na mwelekeo maalum au ulo wazi au Vague isoweza kusema kama Hamas imemalizwa nguvu zake au bado wana uwezo uleule ukizingatia kuwa eneo la Khan Yunis ambalo majeshi ya IDF yamo kwa sasa bado Hamas wameweza kurusha makombora hivyo kuonekana wana uwezo uleule wa tokea mwanzo.

Khan Yunis ni mji ulioko kusini mwa ukanda wa Gaza na ndio yaaminika kuwepo kwa mahandaki na njia nyingi za chini kwa chini. Pia yaaminika kuwa ndipo walipo mateka wa Israeli wanoshikiliwa na kundi la Hamas.

Pamoja na Israeli kufikia hatua hii ya tatu, bado imewaruhusu wanajeshi wake kurudi makwao kujumuika na familia zao wakionekana kuvuka mpaka wa Israeli na Gaza kurudi Gaza.

Mapema mwanzoni kwa vita hii, waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu aliahidi kuhakikisha kundi la Hamas likiteketezwa, kuvunja uwezo wake wa kijeshi na pia kuwaokoa mateka wake wote.

Leo hii miezi yaenda minne bado Israeli haijafanikiwa kuimaliza Hamas jambo linohatarisha Hamas kujitangaza washindi katika vita hii na kisha kuendelea na vita vyake dhidi ya Israeli kutokea pande zote za kaskazini na kusini mwa Gaza kwa maana kwamba majeshi ya Israeli sasa hivi yapo katikati ya Gaza (Mji wa Khan Yunis) na yamezungukwa.

Pia hali hii yaonyesha kwamba kunaanza kuonekana uwazi mkubwa kati ya malengo ya Israeli juu ya vita yake hii dhidi ya Hamas na hali halisi ya kinotokea ndani ya uwanja wa vita. Halikadhalika mauaji ya Arouri yanoaminiwa yamefanywa na Mossad (ingawa israeli haijakiri) yamewalazimisha wapiganaji wa Hamas kutoa kauli kwamba "watalipiza kisasi".

Jambo jingine kubwa ni hofu ya kutokea vita kubwa ya mashariki ya kati kati ya Lebanon Hezbollah na Hamas, wapiganaji wa Hauthi, wanamgambo wa Iran walioko nchini Iraq (Islamic Resistance) wenye makao yao makuu mjini Baghdad ambayo ilishambuliwa na makombora Marekani na wapiganaji wa ISIS walioko nchini Syria sehemu ya Bukamal.

Hofu hiyo pia yajiongeza zaidi pale Iran ilipoamua kutuma meli yake ya kivita iitwayo Alborz Destroyer kwenda katika mfereji wa Bab El Mandep ikiwa ni baada ya Marekani kushambulia wapiganaji wa Huthi wa Yemen.

Kwa kutambua hilo, Marekani wamemtuma tena Antony Blinken waziri wake wa mambo ya nje kwenda tena mashariki ya kati kujaribu kuishawishi Israeli namnaya kumaliza vita hii ambayo imekuwa ngumu kwake. Ikumbukwe kuwa bila msaada mkubwa wa Marekani kuzuia wapiganaji wa Huthi, na khasa Hizbollah wasijiingize katika vita hii,hali ingekuwa mbaya kwa Israeli.

Hivyo katika ziara zake hizo (hii ikiwa ni ya nne ndani ya miezi mitatu) Blinken amelenga kuishawishi Israeli khasa wale waisraeli wenye msimamo mkali na wanounda baraza la mawaziri la Benjamini Netanyahu kuachana na wazo la kuwahamisha wapalestina na kuwapeleka katika kambi za wakimbizi katika nchi jirani za kiarabu.

Hizbollah wahofiwa kuwa na silaha khasa makombora yanoweza kufika mjini TelAviv na miji mingine nchini Israeli na kusababisha maafa makubwa khasa miundombinu mingi ya kimkakati. Marekani imejaribu mara nyingi kuweka mapendezo katika umoja wa mataifa ili kuwazuia Hizbullah kutokuwepo mpakani na Israeli mipango ambayo imeshindwa. Mara ya mwisho Israeli kupigana na Israeli ilikuwa ni mwaka 2006 ambapo vita ile haikutoa mshindi.

Israeli leo kupitia waziri wake wa Ulinzi Yohav Gallant wametoa mpango wa kuitawala Gaza kijeshi huku wapalestina wakiishi ndani ya Gaza wakijitawala lakini bila uhuru wa kujiamulia mambo yao. Pia Hamas hawataweza kutawala Gaza,na Israeli itaratibu shughuli zote za kiutawala zitofanywa na uongozi wa Gaza chini ya wapelestina.

Gallant ametoa leo mpango huo uitwao "Vision for Phase 3 of the war" huku ikisemwa kuwa ni mpango aloubuni yeye binafsi na bado wahitaji kusomwa na kupitiwa na baraza la mawaziri nalile baraza la mawaziri la vita au War Cabinet. Hiyo ndo moja ya sababu kubwa Marekani wamemtuma Blinken haraka.

Ni dhahiri kuwa Israeli ipo katika kitendawili kikubwa cha ni namna gani waimaliza vita hii ama kwa kuendelea nayo hadi mwisho au kuishia katikati. Kuendelea kuwepo mjini Gaza kwaleta mfarakano zaidi kwa kuonekana bado waitawala Gaza na wapalestina hivyo kufifisha zaidi makusuduo ya tokea mwanzo yanotaka kuwepo na mataifa mawili ya Israeli na Palestina.

Pia kuendelea kwa Israeli kuwepo Gaza ni kuendeleza chuki kutoka kwa Hamas na kuongeza idadi ya wapiganaji wa kipalestina ambao hawataki kuwaona waisraeli ndani ya Gaza.

Hivyo, kidogokidogo hali ya Israeli kushindwa kuhimili vita hii imeanza kujionyesha huku wanadiplomasia kadha wa kadha waliishauri Israeli ianze kufikiria kuondoa majeshi yake kutoka Gaza. Hii yaonyesha wazi kuwa Israeli yaelekea kushindwa vita hii ambayo imekwenda kinyume na mipango yake ya kijeshi dhidi ya kundi la Hamas.

Tusijeshangaa kuona wapiganaji hawa wa Hamas wakijitangazia ushindi lakin ihuku wakiendeelelea kupigana hali ambayo itapekelea Israeli kuchukua maamuzi magumu ambayo yatazidi kuifanya itengwe na mataifa mengi duniani.
Hizi faraja za uwongo mnazopeana huko misikitini na vijiwe vya kahawa
 
Endeleeni kujifariji huko msikitini wakati Israel ana mopango yake kabambe, kwamba wewe ndie mkuu wa Israel au unajua sana Israel??

Wakati hata katiba tu ktk nchi yako ni ya kijinga Africans bwana
Hivi nyinyi watu mmesomea shule gani mbona vichwa vyenu vimejaa mavi badala ya ubongo?

Katika maelezo ya mtoa mada mbona hakuna sehemu ameongelea mambo ya dini ?
Hivi ukikaa bila kutukana kukejeli dini za watu utapungukiwa na nn hasa ?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Hivi nyinyi watu mmesomea shule gani mbona vichwa vyenu vimejaa mavi badala ya ubongo?

Katika maelezo ya mtoa mada mbona hakuna sehemu ameongelea mambo ya dini ?
Hivi ukikaa bila kutukana kukejeli dini za watu utapungukiwa na nn hasa ?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Ndugu yangu ITR, mbona hata wewe shida yako ni hiyo hiyo? Pitia maandiko yako.
 
Ndugu yangu ITR, mbona hata wewe shida yako ni hiyo hiyo? Pitia maandiko yako.
Ni lini mm lisha wahi kuchangia mada isiyo ya kidini na nikachanganya na mambo ya dini, ukiona mm nimemshambulia mtu jua najibu kejeli alizo zianzisha tena huwa sishambulii dini huwa namshambulia yeye binafisi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Asante kwa uchambuzi wako! Lakini hata hivyo Wapalestina wamehesabu gharana kubwa kuliko Israeli.
Wapalestina wamekufa kwa wingi, miundo mbinu imeharibiwa, wakazi 2.5 milioni hawana makazi!
Kwa ujumla Wapalestina wameumizwa vibaya sana!
Mimi binafsi sijaona ushindi wa Hamas, wala kushindwa kwa Israeli.
Hapa Jumuia ya Kimataifa ndiyo imeshindwa kwa kushuhudia Wapalestina wakiangamizwa huku dunia inatazama kwa macho!
 
Israeli yaelekea kushindwa kuwamaliza kwa kuwaua wapiganaji wa kundi la Hamas kama walivyoitangazia dunia.

Ni siku 90 (miezi mitatu) imepita tangu Israeli iingize majeshi yake ya ardhini ndani ya Ukanda wa Gaza huku wizara ya afya ya Gaza ikisema kuwa wapalestina wapato 22,000 wamepoteza maisha wengi wakiwa ni watoto, akina mama na akina mama wengine wakiwa wajawazito.

Israeli kwa upande wao imepoteza wanajeshi wapatao 175 huku wengine wapatao 129kubaki kushikiliwa na kundi la Hamas.

Israeli ilianzisha kampeni ya mashambulizi ya anga kuwashughulikia Hamas baada ya wapiganaji wa kundi hilo wakitumia njia za juu kwa juu, ardhini na majini kuvunja uzio wa ulinzi na kuwaua raia wa Israeli wapatao 1200. Ilikuwa ni tarehe 7 mwezi wa October pale wapiganaji hao walipovuka mpaka sehemu ya kusini mwa Israeli kwenye mji huo wa Ashkelon.

Umoja wa mataifa umesema wapalestina wapatao milioni 2 wamepoteza makazi yao huku wengi wakikabiliwa na njaa kali. Hata upande wa Israeli katika mji wa Ashkelon wakazi wengi wameachwa bila makazi yaoo baada ya kuteketezwa kwa moto au kuharibiwa vibaya.

Stratejia ya Israeli katika vita hii na Hamas imegawanywa katika hatua tatu ya kwanza au Phase One ilikiwa ni kufanya mashambulizi makali ya anga. Mashambulizi hayo yamefanya uharibifu mkubwa wa miundombinu ikiwemo hospitali ya Al-Shifa na kuua wapalestina wengi khasa watoto, akina mama na wale wagonjwa na wengi akina mama wakiwa na ujauzito.

Lakini uharibifu wa mabomu katika hospitali kubwa katika Gaza ya Al-Shifa ulisababisha dunia kulaani kitendo hicho cha Israeli kushambulia hospitali hiyo huku jeshi la Israeli likidai kuwepo kwa kituo cha kuongozea mashambuliz ya Hamas yaani "Command Centre".

Mwezi Novemba Israeli ikakubali kusitisha mashambulizi na kubadilishana mateka ambapo Hamas wakawaachilia mateka 80 huku Israeli ikiwaachilia wafungwa wapatao 240 walokuwa wakishikiliwa katika magereza mbalimbali nchini Israeli. Nje ya makubaliano hayo pia mateka wapatao 25 wa kutoka nchini Thailand ambao walikuwa wakifanya kazi katika mashamba ya Israeli waliachiliwa na Hamas.

Baada ya kipindi cha kusitisha mapigano kuisha, mapema mwezi Disemba jeshi la Israeli likaanza hatua ya pili yaani "Phase Two" ya mapigano kwa kuingiza jeshi na vifaru ndani ya ukanda wa Gaza. Israeli iliita wanajeshi wake wa akiba (reservists) wapatao 300,000 na kuanza vita ya ardhini "Ground offensive" dhidi ya kundi la Hamas.

Hatua hii ndo hatua ngumu ambayo jeshi la Israeli limekumbana nayo ambapo wapiganaji wa Hamas wameweza kufanikiwa kuwaua wanajeshi wengi wa Israeli kwa kutumia njia ya kushtukiza adui "ambush", mjengo kwa mjengo au "urban warfare" na ile ya kuvizia au "asymmetric war" ambayo wapiganaji hawa hujificha katika majengo na kushambulia kifaru kinopita nje.

Ugumu wa hatua hii pia ni kitendo cha wapiganaji wa Huthi wa Yemen ambao wamezuia meli kadhaa ambazo zilikuwa zikipeleka mzigo wa silaha nchini Israeli. Algeria pia ilizuia meli moja ambayo ilikuwa na shehena ya silaha ilokuwa ikielekea Israeli. Marekani ambayo ni mshirika mkubwa wa Israeli imekuwa ikiwasaidia IDF (Israel Defence Forces) kwa kushambulia kambi za makundi ya Hamas na kundi la Huthi na pia kundi la Hezbollah lililoko upande wa kaskazini mwa Israeli kuingia nchini Jordan.

Kwa kuweka meli zake za kivita katika bahari ya Mediterranean, Marekani imeweza kukabiliana na wapiganaji hao wa kutoka Yemen, na pia hata nchini Iraq ambapo ni juzi tu wapiganaji kadhaa wanohusiana na Hamas waliuawa kwa makombora.

Iran ambayo ni wafadhili wakubwa wa makundi ya Hamas na Hezbollah mpaka sasa haijachukua hatua zozote za kujibu mashambulizi ya jeshi la Israeli dhidi ya mmoja wa makamanda wake Saleh Al Arouri. Al Aroui aliuawa pamoja na wapiganaji kadhaa wa Hamas kusini mwa mji wa Beirut kwa makombora. Kwa kujibu wa idara ya ujasusi ya Mossad, Arouri amekuwa akishiriki mipango mingi dhidi ya Israeli likiwemo shambulizi la tarehe 7 Octoba mwaka jana.

Mapema mwaka huu Israeli imeingia katika hatua ya tatu yaani Phase Three ambayo yahusisha vita iso na nguvu sana yaani "low intensity". Hatua hii yaweza kuonekana kuwa ni hatua iso na mwelekeo maalum au ulo wazi au Vague isoweza kusema kama Hamas imemalizwa nguvu zake au bado wana uwezo uleule ukizingatia kuwa eneo la Khan Yunis ambalo majeshi ya IDF yamo kwa sasa bado Hamas wameweza kurusha makombora hivyo kuonekana wana uwezo uleule wa tokea mwanzo.

Khan Yunis ni mji ulioko kusini mwa ukanda wa Gaza na ndio yaaminika kuwepo kwa mahandaki na njia nyingi za chini kwa chini. Pia yaaminika kuwa ndipo walipo mateka wa Israeli wanoshikiliwa na kundi la Hamas.

Pamoja na Israeli kufikia hatua hii ya tatu, bado imewaruhusu wanajeshi wake kurudi makwao kujumuika na familia zao wakionekana kuvuka mpaka wa Israeli na Gaza kurudi Gaza.

Mapema mwanzoni kwa vita hii, waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu aliahidi kuhakikisha kundi la Hamas likiteketezwa, kuvunja uwezo wake wa kijeshi na pia kuwaokoa mateka wake wote.

Leo hii miezi yaenda minne bado Israeli haijafanikiwa kuimaliza Hamas jambo linohatarisha Hamas kujitangaza washindi katika vita hii na kisha kuendelea na vita vyake dhidi ya Israeli kutokea pande zote za kaskazini na kusini mwa Gaza kwa maana kwamba majeshi ya Israeli sasa hivi yapo katikati ya Gaza (Mji wa Khan Yunis) na yamezungukwa.

Pia hali hii yaonyesha kwamba kunaanza kuonekana uwazi mkubwa kati ya malengo ya Israeli juu ya vita yake hii dhidi ya Hamas na hali halisi ya kinotokea ndani ya uwanja wa vita. Halikadhalika mauaji ya Arouri yanoaminiwa yamefanywa na Mossad (ingawa israeli haijakiri) yamewalazimisha wapiganaji wa Hamas kutoa kauli kwamba "watalipiza kisasi".

Jambo jingine kubwa ni hofu ya kutokea vita kubwa ya mashariki ya kati kati ya Lebanon Hezbollah na Hamas, wapiganaji wa Hauthi, wanamgambo wa Iran walioko nchini Iraq (Islamic Resistance) wenye makao yao makuu mjini Baghdad ambayo ilishambuliwa na makombora Marekani na wapiganaji wa ISIS walioko nchini Syria sehemu ya Bukamal.

Hofu hiyo pia yajiongeza zaidi pale Iran ilipoamua kutuma meli yake ya kivita iitwayo Alborz Destroyer kwenda katika mfereji wa Bab El Mandep ikiwa ni baada ya Marekani kushambulia wapiganaji wa Huthi wa Yemen.

Kwa kutambua hilo, Marekani wamemtuma tena Antony Blinken waziri wake wa mambo ya nje kwenda tena mashariki ya kati kujaribu kuishawishi Israeli namnaya kumaliza vita hii ambayo imekuwa ngumu kwake. Ikumbukwe kuwa bila msaada mkubwa wa Marekani kuzuia wapiganaji wa Huthi, na khasa Hizbollah wasijiingize katika vita hii,hali ingekuwa mbaya kwa Israeli.

Hivyo katika ziara zake hizo (hii ikiwa ni ya nne ndani ya miezi mitatu) Blinken amelenga kuishawishi Israeli khasa wale waisraeli wenye msimamo mkali na wanounda baraza la mawaziri la Benjamini Netanyahu kuachana na wazo la kuwahamisha wapalestina na kuwapeleka katika kambi za wakimbizi katika nchi jirani za kiarabu.

Hizbollah wahofiwa kuwa na silaha khasa makombora yanoweza kufika mjini TelAviv na miji mingine nchini Israeli na kusababisha maafa makubwa khasa miundombinu mingi ya kimkakati. Marekani imejaribu mara nyingi kuweka mapendezo katika umoja wa mataifa ili kuwazuia Hizbullah kutokuwepo mpakani na Israeli mipango ambayo imeshindwa. Mara ya mwisho Israeli kupigana na Israeli ilikuwa ni mwaka 2006 ambapo vita ile haikutoa mshindi.

Israeli leo kupitia waziri wake wa Ulinzi Yohav Gallant wametoa mpango wa kuitawala Gaza kijeshi huku wapalestina wakiishi ndani ya Gaza wakijitawala lakini bila uhuru wa kujiamulia mambo yao. Pia Hamas hawataweza kutawala Gaza,na Israeli itaratibu shughuli zote za kiutawala zitofanywa na uongozi wa Gaza chini ya wapelestina.

Gallant ametoa leo mpango huo uitwao "Vision for Phase 3 of the war" huku ikisemwa kuwa ni mpango aloubuni yeye binafsi na bado wahitaji kusomwa na kupitiwa na baraza la mawaziri nalile baraza la mawaziri la vita au War Cabinet. Hiyo ndo moja ya sababu kubwa Marekani wamemtuma Blinken haraka.

Ni dhahiri kuwa Israeli ipo katika kitendawili kikubwa cha ni namna gani waimaliza vita hii ama kwa kuendelea nayo hadi mwisho au kuishia katikati. Kuendelea kuwepo mjini Gaza kwaleta mfarakano zaidi kwa kuonekana bado waitawala Gaza na wapalestina hivyo kufifisha zaidi makusuduo ya tokea mwanzo yanotaka kuwepo na mataifa mawili ya Israeli na Palestina.

Pia kuendelea kwa Israeli kuwepo Gaza ni kuendeleza chuki kutoka kwa Hamas na kuongeza idadi ya wapiganaji wa kipalestina ambao hawataki kuwaona waisraeli ndani ya Gaza.

Hivyo, kidogokidogo hali ya Israeli kushindwa kuhimili vita hii imeanza kujionyesha huku wanadiplomasia kadha wa kadha waliishauri Israeli ianze kufikiria kuondoa majeshi yake kutoka Gaza. Hii yaonyesha wazi kuwa Israeli yaelekea kushindwa vita hii ambayo imekwenda kinyume na mipango yake ya kijeshi dhidi ya kundi la Hamas.

Tusijeshangaa kuona wapiganaji hawa wa Hamas wakijitangazia ushindi lakin ihuku wakiendeelelea kupigana hali ambayo itapekelea Israeli kuchukua maamuzi magumu ambayo yatazidi kuifanya itengwe na mataifa mengi duniani.
Umeandika mambo mengi ila hujaonyesha ni vipi IDF imefeli kuiangamiza Hamas.
 
Back
Top Bottom