Israel siyo taifa teule

Israel siyo taifa teule

Taifa teule kwa sababu tu "wanaouliwa ni waislamu" lau ingelikua wanauwa wakristo hiyo kauli yenu ya "taifa teule isingekuwepo" hizo ni chuki dhidi ya waislamu na si kingine.
Aliyesoma wapalestina ni waislamu Nani? Kule kuna wakristo na wayahudi.
 
Sasa hoja yako hapo iko wapi ? Kwani mtume hii aya ameifasiri vipi ? Mirza Gulamu Allau amlaani yeye amefasiri vipi hii aya. Maana aya iko wazi.

Kama wangekuwa Mayahudi na Wakristo na Wasabii wameamini aya isinge sema " ...na wakristo,walio muamini..." maana yake ni miongoni mwa walio muamini Allah,sababu Mayahudi katika maana husemwa ni wale Watu ambao nabii Mussa alitumwa kwao.


Wewe umedai kwamba UYAHUDI ni UKAFIRI na mimi nimekuletea aya (wala si Hadhrat Ahmad as aliyekuletea) aya inayowataja Wayahudi na Wakristo na wasabii waliomuamini Allah ambao kwa kwa kumuamini Allah watalipwa malipo yao, sasa kama Uyahudi ni Ukafiri kwa maoni yako ya kijinga iweje Mayahudi walipwe kwa matendo ya uyahudi wao???-----Kumbuka Uyahudi ni dini yao aliyokuja nayo nabii Musa (as).
 
Taifa teule kwa sababu tu "wanaouliwa ni waislamu" lau ingelikua wanauwa wakristo hiyo kauli yenu ya "taifa teule isingekuwepo" hizo ni chuki dhidi ya waislamu na si kingine.
Hapana tangu mwanzo Waisraeli walikuwa watu wa shari ukiwachokoza,sasa kama kuna mauaji huko basi mimi na wewe hatujui.
 
Wewe umedai kwamba UYAHUDI ni UKAFIRI na mimi nimekuletea aya (wala si Hadhrat Ahmad as aliyekuletea) aya inayowataja Wayahudi na Wakristo na wasabii waliomuamini Allah ambao kwa kwa kumuamini Allah watalipwa malipo yao, sasa kama Uyahudi ni Ukafiri kwa maoni yako ya kijinga iweje Mayahudi walipwe kwa matendo ya uyahudi wao???-----Kumbuka Uyahudi ni dini yao aliyokuja nayo nabii Musa (as).
Aya haijaonyesha ya kuwa Mayahudi si makafiri na wala Wakristo si makafiri,nilikuwekea aya inayo onyesha ya kuwa Mayahudi ni Makafiri na ni washirikina.

Nimemgusia Gulamu sababu ndiyo kiongozi wako.

Ukafiri maana yake ni kuificha haki na kuikataa. Ushirikina ni kuabudu miungu kinyume na Allah.

Weka ushahidi ambao unaonyesha Nabii Musa alikuja na dini ya Uyahudi ? Kwanini unamzulia uongo mtume wa Allah ?

Lakini Mayahudi wenye Dini ya Uyahudi walilaaniwa. Anasema Allah aliye juu :

64. Na Mayahudi walisema: Mkono wa Mwenyezi Mungu umefumba. Mikono yao ndiyo iliyo fumba, na wamelaaniwa kwa sababu ya waliyo yasema. Bali mikono yake iwazi. Hutoa apendavyo. Kwa yakini yaliyo teremshwa kwako kutoka kwa Mola wako Mlezi yatawazidisha wengi katika wao uasi na kufuru. Na Sisi tumewatilia uadui na chuki baina yao mpaka Siku ya Kiyama. Kila mara wanapo washa moto wa vita, Mwenyezi Mungu anauzima. Na wanajitahidi kuleta uharibifu katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu hawapendi waharibifu. (al Maaidah : 64)

Sasa vipi Mtume wa Allah aje na dini ambayo ni ukafiri na Ushirikina hali ya kuwa mitume na manabii wote walikuwa Waislamu.

Nabii Musa alikuwa dini gani ?
 
MUNGU WA ISAKA, MUNGU WA IBRAHIM, MUNGU WA YAKOBO. MUNGU WA ISRAELI.

MUNGU WA BABA YENU (waisraeli) NILIYEKUTOENI KATIKA NCHI YA UTUMWA.

Kwanini hatajwi kama MUNGU MUUMBA ULIMWENGU? Kwanini aliongea na kuingia mikataba(maagano) na hao jamaa tu?!

Hawa jamaa huyu ni Mungu wao sie wengine tumemshobokea tu lazma tuwe kama watoto wa kambo.

Misri walikua na miungu yao, Ugiriki walikua na miungu yao, Ulaya Kaskazini walikua na miungu yao, kila sehem walikua na imani zao na walidili na miungu yao kwa namna tofauti tofauti. (Tusome sana historia na maandiko tusikariri Biblia tu na Qurani).

Wana wa Israel Mungu wao alikua anawaacha kama wakimsahau, hata sehem zingine ilikua ni hivo hivo tu.
Sasa swala la kila taifa kumkubali mungu wa Israeli maana yake ni kwamba Miungu yetu tumeikataa na mkataa kwao ni mtumwa.

Nisiwachoshe sana ila dunia ilijichanganya sana kumgeuza Mungu wa Israeli kuwa Mungu wa ulimwengu mzima, na kwa MUNGU WA ISRAELI, HILI NI TAIFA LAKE TEULE.
Uko vizuri bonge la point.
 
Aya haijaonyesha ya kuwa Mayahudi si makafiri na wala Wakristo si makafiri,nilikuwekea aya inayo onyesha ya kuwa Mayahudi ni Makafiri na ni washirikina.

Nimemgusia Gulamu sababu ndiyo kiongozi wako.

Ukafiri maana yake ni kuificha haki na kuikataa. Ushirikina ni kuabudu miungu kinyume na Allah.

Weka ushahidi ambao unaonyesha Nabii Musa alikuja na dini ya Uyahudi ? Kwanini unamzulia uongo mtume wa Allah ?

Lakini Mayahudi wenye Dini ya Uyahudi walilaaniwa. Anasema Allah aliye juu :

64. Na Mayahudi walisema: Mkono wa Mwenyezi Mungu umefumba. Mikono yao ndiyo iliyo fumba, na wamelaaniwa kwa sababu ya waliyo yasema. Bali mikono yake iwazi. Hutoa apendavyo. Kwa yakini yaliyo teremshwa kwako kutoka kwa Mola wako Mlezi yatawazidisha wengi katika wao uasi na kufuru. Na Sisi tumewatilia uadui na chuki baina yao mpaka Siku ya Kiyama. Kila mara wanapo washa moto wa vita, Mwenyezi Mungu anauzima. Na wanajitahidi kuleta uharibifu katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu hawapendi waharibifu. (al Maaidah : 64)

Sasa vipi Mtume wa Allah aje na dini ambayo ni ukafiri na Ushirikina hali ya kuwa mitume na manabii wote walikuwa Waislamu.

Nabii Musa alikuwa dini gani ?


Kiongozi wangu hahusiki hapa na wala Sheikh wako hahusiki hapa, hapa ni mimi na wewe:


Tofautisha kati ya UYAHUDI NA MAYAHUDI, Uyahudi ni dini kama ulivyo Uisilamu na Mayahudi ni Wafuadi wa dini ya Uyahudi kama ilivyokuwa kwa Waisilamu ni wafuasi wa dini ya Uisilamu.

Dini inaweza kuwa na mafundisho mazuri lakini wafuasi wa dini wakatenda kinyume na mafundisho ya dini yao, mfano: Kula nyama ya nguruwe haitakiwi na Uisilamu lakini Waisilamu wengi leo wanakula nyama ya nguruwe na wanafanya zinaa nk, je hapo tuulaumu Uisilamu au tuwalaumu hao waisilamu???, na ndivyo hivyo katika Dini ya Uyahudi, kuna Mayahudi wema ambao kwa matendo yao watalipwa na pia kuna mayahudi waovu kwa maovu yao watalipwa.

Ninachotaka ufahamu ni kwamba kuna UYAHUDI na MAYAHUDI na makosa ya binafsi ya mayahudi huwezi kuyanasibisha na dini yao ya UYAHUDI.

Hiyo ni sawa na kunasibisha Ukristo uliofundishwa na Yesu na imani potofu ya Wakristo juu ya utatu mtakatifu, hapo huwezi kulaumu Ukristo bali Wakristo ndio wa kulaumiwa kutokana na imani hiyo mbovu ya kishirikina.

Hapo nadhani utakuwa umepata somo.

Hivyo mada ipo pale pale Kwamba Uyahudi kama dini sio UKAFIRI.
 
Kiongozi wangu hahusiki hapa na wala Sheikh wako hahusiki hapa, hapa ni mimi na wewe:


Tofautisha kati ya UYAHUDI NA MAYAHUDI, Uyahudi ni dini kama ulivyo Uisilamu na Mayahudi ni Wafuadi wa dini ya Uyahudi kama ilivyokuwa kwa Waisilamu ni wafuasi wa dini ya Uisilamu.

Dini inaweza kuwa na mafundisho mazuri lakini wafuasi wa dini wakatenda kinyume na mafundisho ya dini yao, mfano: Kula nyama ya nguruwe haitakiwi na Uisilamu lakini Waisilamu wengi leo wanakula nyama ya nguruwe na wanafanya zinaa nk, je hapo tuulaumu Uisilamu au tuwalaumu hao waisilamu???, na ndivyo hivyo katika Dini ya Uyahudi, kuna Mayahudi wema ambao kwa matendo yao watalipwa na pia kuna mayahudi waovu kwa maovu yao watalipwa.

Ninachotaka ufahamu ni kwamba kuna UYAHUDI na MAYAHUDI na makosa ya binafsi ya mayahudi huwezi kuyanasibisha na dini yao ya UYAHUDI.

Hiyo ni sawa na kunasibisha Ukristo uliofundishwa na Yesu na imani potofu ya Wakristo juu ya utatu mtakatifu, hapo huwezi kulaumu Ukristo bali Wakristo ndio wa kulaumiwa kutokana na imani hiyo mbovu ya kishirikina.

Hapo nadhani utakuwa umepata somo.

Hivyo mada ipo pale pale Kwamba Uyahudi kama dini sio UKAFIRI.
Duh! yani Baba, Mwana na Roho mtakatifu ni ushirikina? Unaweza kudadavua zaidi mkuu
 
Hivi kumbe JF kuna watu wanauelewa mdogo hivi?? nyie wote bado vitoto vya secondary!!! kwa maana hiyo yesu alikuwa mzungu au muarabu?? yesu huyo hana Melanin? basi alikuwa kilema
 
Duh! yani Baba, Mwana na Roho mtakatifu ni ushirikina? Unaweza kudadavua zaidi mkuu


Ushirikina ni nini??

Ushirikina ni ile hali ya kumshirikisha Mungu na waungu wengine katika sifa, heshima, utegemezi nk, vitu ambavyo ni Mungu pekee anastahili. Hii ni definition fupi.

Katika Baba, Mwana na Roho mtakatifu, hapo Baba katika imani ya Ukristo ni Mungu na Mwana ndiye Yesu na Roho mtakatifu, hapo unaona Mungu amepewa nafsi tatu, yaani Mungu ameshirikishwa na nafsi mbili za Mwana na Roho na hapo ndio ushirikina unapokuwepo.
 
Kiongozi wangu hahusiki hapa na wala Sheikh wako hahusiki hapa, hapa ni mimi na wewe:


Tofautisha kati ya UYAHUDI NA MAYAHUDI, Uyahudi ni dini kama ulivyo Uisilamu na Mayahudi ni Wafuadi wa dini ya Uyahudi kama ilivyokuwa kwa Waisilamu ni wafuasi wa dini ya Uisilamu.

Dini inaweza kuwa na mafundisho mazuri lakini wafuasi wa dini wakatenda kinyume na mafundisho ya dini yao, mfano: Kula nyama ya nguruwe haitakiwi na Uisilamu lakini Waisilamu wengi leo wanakula nyama ya nguruwe na wanafanya zinaa nk, je hapo tuulaumu Uisilamu au tuwalaumu hao waisilamu???, na ndivyo hivyo katika Dini ya Uyahudi, kuna Mayahudi wema ambao kwa matendo yao watalipwa na pia kuna mayahudi waovu kwa maovu yao watalipwa.

Ninachotaka ufahamu ni kwamba kuna UYAHUDI na MAYAHUDI na makosa ya binafsi ya mayahudi huwezi kuyanasibisha na dini yao ya UYAHUDI.

Hiyo ni sawa na kunasibisha Ukristo uliofundishwa na Yesu na imani potofu ya Wakristo juu ya utatu mtakatifu, hapo huwezi kulaumu Ukristo bali Wakristo ndio wa kulaumiwa kutokana na imani hiyo mbovu ya kishirikina.

Hapo nadhani utakuwa umepata somo.

Hivyo mada ipo pale pale Kwamba Uyahudi kama dini sio UKAFIRI.
Hujanipa ushahidi wa kuonyesha ya kuwa Uyahudi si ukafiri wala hujanipa ushahidi wa kuonyesha ya kuwa mtume Musa amekuja na Uyahudi.

Soma katika Qur'aan kuanzia surat al Fat'ha mpaka surat an Nas hakuna sehemu ambayo Allah ameutaja Uyahudi na Mayahudi kwa sifa nzuri.

Mimi masheikh wangu hapa wanahusika sababu narejea kwao,wewe kadhalika Gulamu anahusika sababu yeye ndiyo kiongozi wenu.

Niambie Uyahudi ni Dini na inafundisha nini na uniambie nani amekwambia ya kuwa nabii Musa amekuja na dini ya UYAHUDI.
 
Hujanipa ushahidi wa kuonyesha ya kuwa Uyahudi si ukafiri wala hujanipa ushahidi wa kuonyesha ya kuwa mtume Musa amekuja na Uyahudi.

Soma katika Qur'aan kuanzia surat al Fat'ha mpaka surat an Nas hakuna sehemu ambayo Allah ameutaja Uyahudi na Mayahudi kwa sifa nzuri.

Mimi masheikh wangu hapa wanahusika sababu narejea kwao,wewe kadhalika Gulamu anahusika sababu yeye ndiyo kiongozi wenu.

Niambie Uyahudi ni Dini na inafundisha nini na uniambie nani amekwambia ya kuwa nabii Musa amekuja na dini ya UYAHUDI.


Wewe ndio unayetakiwa kuonyesha kwamba UYAHUDI ni UKAFIRI.

Mimi nimekuonyesha kwamba Kafiri au asiyekuwa kafiri ni Myahudi/Wayahudi na sio Uyahudi, Tofautisha kati ya UYAHUDI na MYAHUDI/MAYAHUDI, Uyahudi ni dini kama ilivyokuwa dini ya Uisilamu au Ukristo au Usabii nk, kama jinsi katika Uisilamu na Ukristo kuna watu wema na wabaya ni hivyohivyo kwenye Uyahudi kuna watu wema na wabaya, katika hali hiyo huwezi kuhukumu UYAHUDI kama dini kwa makosa ya wafuasi wake, -----hili nimeishalieleza hapo mwanzo, yaani mfano huwezi kuhukumu Uisilamu kwa makosa ya kigaidi ya Waisilamu.

Eti unauliza: Uyahudi ni dini inayofundisha nini na nani kasema Nabii Musa (as) alikuja na dini ya Uyahudi??!!----- Halafu maswali kama hayo bado unataka kujiita wewe ni Muisilamu safi mwenye elimu ya dini kupambana na "wenye elimu???

Hujui kwamba Uyahudi uliletwa na nani??!!, kesho utauliza Ukristo nao uliletwa na nani na ulifundisha nini??. Hamna lolote isipokuwa ni midomo myepesi kutusi watu kwa kuwaita "Maqadian" na kuwakufurisha watu wa dini zingine ambazo Allah mwenyewe anakiri baadhi ya wafuasi wao ni watu wema na atawalipa kwa wema wao. Allah mwenyewe anawakiri wafuasi wema wa dini hiyo ya Uyahudi wewe unapinga kwamba dini hizo ni UKAFIRI, sasa kama dini zao ni ukafiri iweje Allah awaahidi malipo siku ya Qiyama???!!, huo wema watakaolipwa nao wamejifunza kupitia mafundisho gani??


"------- Na lau kama Allah hakuwakinga watu kwa watu, basi hapana shaka zingalivunjwa nyumba za watawa na MAKANISA, na MASINAGOGI, na MISIKITI ambamo ndani yake jina la ALLAH linatajwa kwa wingi". (Qur'an 22:40)

Haya hebu niambie humo ndani ya MASINAGOGI ambamo jina la Allah linatajwa kwa wingi ni watu gani hao hulitaja jina la Allah kwa wingi???, tunawajua watu wanaotumia maKanisa na msiktini ndanimo kutaja jina la Allah.
 
Wewe ndio unayetakiwa kuonyesha kwamba UYAHUDI ni UKAFIRI.
Labda uniambie nikuonyeshe mara ngapi ?

Swali langu hujajibu na najua huwezi kujibu,umemzulia uongo nabii wa Allah Musa kwamba amekuja na Dini ya Uyahudi. Naomba uweke uthibitisho wa hayo uliyo yaandika.


Mimi nimekuonyesha kwamba Kafiri au asiyekuwa kafiri ni Myahudi/Wayahudi na sio Uyahudi, Tofautisha kati ya UYAHUDI na MYAHUDI/MAYAHUDI, Uyahudi ni dini kama ilivyokuwa dini ya Uisilamu au Ukristo au Usabii nk,
Unaposema Uyahudi ni kama ulivyo kuwa Uislamu ina maana Uyahudi ni usahihi maana yake kama si Ukafiri. Uko wapi na aya ya Allah katika sura ya 5,anasema Allah :

3. ".....Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini. " (al-Maaidah : 3)

Uyahudi ni kama Uislamu kwenye nini ? Kama Uyahudi si ukafiri wala si Ushirikina,niambie Uyahudi ni nini hasa ? Sababu hababu hata Ubudha nao ni Dini,je ni Dini ya Allah au ? Usikwepe swali.
 
Uisilamu au Ukristo au Usabii nk, kama jinsi katika Uisilamu na Ukristo kuna watu wema na wabaya ni hivyohivyo kwenye Uyahudi kuna watu wema na wabaya, katika hali hiyo huwezi kuhukumu UYAHUDI kama dini kwa makosa ya wafuasi wake, -----hili nimeishalieleza hapo mwanzo, yaani mfano huwezi kuhukumu Uisilamu kwa makosa ya kigaidi ya Waisilamu.
Kijana usikimbie swali langu. Uislamu ni dini ambayo Allah ameiridhia na matendo ya waislamu ni jambo kando.

Niambie Uyahudi ni fundisho gani ambalo Allah amewateremshia ? Kadhalika Ukristo nao unafundisha nini juu ya Allah ?

Nini maana ya Ushirikina na nini maana ya Ukafiri ?
 
Eti unauliza: Uyahudi ni dini inayofundisha nini na nani kasema Nabii Musa (as) alikuja na dini ya Uyahudi??!!----- Halafu maswali kama hayo bado unataka kujiita wewe ni Muisilamu safi mwenye elimu ya dini kupambana na "wenye elimu???
Ulisema huko nyuma ya kuwa nabii Musa alikuja na Dini ya Uyahudi,nakutaka sasa uweke uthibitisho huo. Mimo naweza kuthinitisha ya kuwa wewe si Muislamu ila wewe huwezi kuthibitisha ya kuwa mimi si Muislamu.

Sababu wewe ni Qadiani labda kama uwe umesilimu leo na Uqadiani ni Ushirikina na ni Ukafiri pia. Huwezi kumzulia nabii wa Allah uongo wa wazi na kupindisha maana za aya kwa ujinga wako na ujinga wa Mirza Gulamu (Laana ya Allah iwe juu yake).

Maswali yangu yako pale pale niambie Uyahudi ni nini na ni lini hasa Uyahudi ulianza kuwepo na unithibitishie ya kuwa kipindi cha nabii Musa Uyahudi ulikuwepo.
 
Back
Top Bottom