MUNGU WA ISAKA, MUNGU WA IBRAHIM, MUNGU WA YAKOBO. MUNGU WA ISRAELI.
MUNGU WA BABA YENU (waisraeli) NILIYEKUTOENI KATIKA NCHI YA UTUMWA.
Kwanini hatajwi kama MUNGU MUUMBA ULIMWENGU? Kwanini aliongea na kuingia mikataba(maagano) na hao jamaa tu?!
Hawa jamaa huyu ni Mungu wao sie wengine tumemshobokea tu lazma tuwe kama watoto wa kambo.
Misri walikua na miungu yao, Ugiriki walikua na miungu yao, Ulaya Kaskazini walikua na miungu yao, kila sehem walikua na imani zao na walidili na miungu yao kwa namna tofauti tofauti. (Tusome sana historia na maandiko tusikariri Biblia tu na Qurani).
Wana wa Israel Mungu wao alikua anawaacha kama wakimsahau, hata sehem zingine ilikua ni hivo hivo tu.
Sasa swala la kila taifa kumkubali mungu wa Israeli maana yake ni kwamba Miungu yetu tumeikataa na mkataa kwao ni mtumwa.
Nisiwachoshe sana ila dunia ilijichanganya sana kumgeuza Mungu wa Israeli kuwa Mungu wa ulimwengu mzima, na kwa MUNGU WA ISRAELI, HILI NI TAIFA LAKE TEULE.