Israel Sasa inatosha

Israel Sasa inatosha

Hii ni dalili kuwa hii vita Israel vita imewashinda.
 
Mimi nasimama na Israel kwenye mapigano haya, ila tu kwa niliyoyaona Jana naweza kushauri kwamba Sasa inatosha. Nadhani kwa Sasa Israel isistishe mapigano na Hamas maana kwa Sasa wanaoumia sio Hamas ni raia wa kawaida wa Gaza. Kama ni kisasi kimeshalipwa. Maana mpaka Sasa wameuawa wapalestina 11,500. Ambao watoto waliokwisha uawa wanakaribia 5,000 hii inaumiza Sana.

IDF kashamsambaratisha Hamas sidhani Kama Kuna haja ya kuendelea na mashambulizi. Kwa Sasa Hamas Hana nguvu na wapalestina wamejifunza kwamba mbeleni wasifanye uchokozi kwa Israel wa aina ile.

Kuna mambo matatu nimeyaona yamenifanya nifikirie hivyo.

1. Kwanza, Jana Israel kashambulia na kuilipua kwa makombora shule ya watoto na kuua watu hamsini ikiwemo watoto wadogo. Shule hiyo inaitwa Al Buraq, na inasemekana mjukuu wa kiongozi mkuu wa Hamas Ismail Haniyeh aliuawa kwenye mashambulizi hayo.

Sababu kuu ya IDF kuishambulia shule hiyo ni baada ya kamanda wa Hamas Ahmed Siam aliyekuwa kwenye mapambano na IDF kwenye eneo la Hospitali ya Rantisi Kuzidiwa na kwenda kujificha kwenye shule hiyo. Hivyo Israel ikaona immalize pamoja na watoto waliokuwemo humo. Kwa kweli niliumia kuona watoto wasiokuwa na hatia wakiuawa kwa ujinga wa Hamas. Nikawaza itakuwaje kwa huko mbeleni?.

2. Pili, Kuna Jambo la kusikitisha kwenye Hospitali ya Al Shifa. Ni kwamba IDF imeizunguka hiyo Hospitali na kuanza mashambulizi. Tatizo ni kwamba Kuna vitoto vichanga karibia 39 vimo humo ndani, ndio kwanza vipo kwenye incubator. Sasa ninachoogopa IDF asije akailipua Hospitali nzima na kuua hao watoto.

Nasema hivyo kwa sababu IDF anaweza kuilipua Hospitali nzima ya Al Shifa kwa kuwa kiongozi wa Hamas Yahya Sinwar kajificha humo pamoja Viongozi wachache waliobakia.

Kingine ni kwamba ndani ya Hospitali hiyo Kuna wagonjwa wengi mahtuti na wazee. Hivyo kuilipua itasababisha mauaji ya halaiki.

3. Tatu, iwapo IDF itailipua Hospitali hiyo Kuna uwezekano wa Mataifa ya kiarabu kulazimishwa kuingilia kati na kuendeleza mgogoro kuwa mkubwa na kupelekwa hata vita vya tatu vya dunia.

Maana Al Shifa imekuwa Kama mtego. Ndio maana Hamas wameruhusu watu wengi wawe pale ili Israel asipate nafasi ya kuishambulia. Maana lile ndio eneo la mwisho kabisa kwa Hamas kujilinda. Hivyo hakuna haja ya kumwaga damu nyingi. Wakubaliane Israel asogee nyuma na Hamas wawaachie mateka basi. Mambo mengine yaendelee.

Hivyo basi, naishauri Israel ifanye yafuatayo.

1. Kutangaza kusitisha haya mapigano, maana wanaoadhirika ni watoto, wanawake na wazee na sio Hamas Tena.

2. Israel atangaze kuwepo na Kambi ya jeshi itakayosimamiwa na Umoja wa Mataifa. Kambi hiyo iwe kilometa ishirini kati ya mpaka wa Israel na Gaza.

3. Israel ifanye makubaliano na Hamas ya kuondoka Al Shifa na Hamas wawaachie mateka waliowashika. Na makubaliano haya yasimamiwe na Umoja wa Mataifa.

4. Jukumu la kuisimamia Gaza liwe chini ya Mahmoud Abbas ambaye kisheria ndio Rais wa Palestina, Gaza ikiwemo. Ili kuendeleza makubaliano ya Oslo ya mwaka 1993 ili mchakato wa kuanzisha taifa la Palestine lianze..

4. Nanshauri kuwepo na makubaliano kati ya Palestina kwa niaba ya Hamas na Israel upande mwingine , kwamba hawatovamiana Tena.
Hayo yote yanatokea, Je? Palestine hawana Jeshi?
 
Basi sawa wasiache kupigana
Suala la wao kuendelea au kuacha kupigana hilo ni juu yao mm na ww hatuna maamuzi juu ya hayo.

Lamsingi dunia nzima ime jua ya kuwa jeshi la Israel bila Marekani ni JWTZ iliyo chagamka, kwanza hata hapo nimewapendelea.
 
Vita kuisha inabidi hao hamas wadhibitiwe kisawasawa.

Kuuliwa hao watoto ni matokeo ya ujinga wa hao hamasi,wao ndo sababu.

Wakiachiwa wataendelea kufanya huo ujinga sana.
Sasa Hamas utaidhibitije hali ya kuwa uwaacha hao Hamas badala yake unaenda kushambulia watoto na wanawake?
 
Nimejiuliza hii thread sasa, jinsi kichwa cha habari kilivyoandikwa ni kwaajili yetu, au netanyahu. Na je! Kama ni kwaajili yake. Atapataje hizi salamu😂😂😂😂😂.
 
Sasa Hamas utaidhibitije hali ya kuwa uwaacha hao Hamas badala yake unaenda kushambulia watoto na wanawake?
Sidhani kama hao idf lengo lao ni kuwaua hao raia.

Hamas ndo mdudu anatakiwa aangamizwe ili palestina iwe sehem salama.
 
Israel haiwezi kuimaliza HAMAS, inahitaji HAMAS iendelee kuwepo ili kutimiza malengo yake ya kujiportray kwamba ina existential threat kwa wajomba zake wamarekani na waulaya huku kimyakimya ikiendelea kumega ardhi za wapalestina kwa visingizio vya security.
Kabisa mkuu, tena Israel imekuwa ikiitumia Hamas kudidimiza uhalali wa mamlaka ya kipalestina kule west bank na kama mamlaka inayowakilisha Wapalestina wote.

Ikiambiwa izungumze na PA ya Mahmoud Abbas inasingizia hiyo mamlaka haiwakilishi wapalestina wote maana inawatawala west bank tu na haipo Gaza.

Ikiambiwa izungumze na Hamas inasema ni magaidi hawawakilishi Wapalestina wote.

Hivyo uhasama wa Hamas na PLO ya Mahmoud Abbas umetumiwa na Israel kuzima ndoto za Wapalestina kuwa na taifa lao huru.
 
Sidhani kama hao idf lengo lao ni kuwaua hao raia.

Hamas ndo mdudu anatakiwa aangamizwe ili palestina iwe sehem salama.
Sasa mbona anawauwa hao raia anawaacha Hamas?
 
Kabisa mkuu, tena Israel imekuwa ikiitumia Hamas kudidimiza uhalali wa mamlaka ya kipalestina kule west bank.

Ikiambiwa izungumze na PA ya Mahmoud Abbas inasingizia hiyo mamlaka haiwakilishi wapalestina wote maana inawatawala west bank tu na haipo Gaza.

Ikiambiwa izungumze na Hamas inasema ni magaidi hawawakilishi Wapalestina wote.

Hivyo uhasama wa Hamas na PLO ya Mahmoud Abbas umetumiwa na Israel kuzima ndoto za Wapalestina kuwa na taifa lao huru.
Lakini hilo taifa lilishindwa kupatikana kwa zaidi ya miaka 60 kabla ya hiyo hamas haijaitawala gaza.
 
Mimi nasimama na Israel kwenye mapigano haya, ila tu kwa niliyoyaona Jana naweza kushauri kwamba Sasa inatosha. Nadhani kwa Sasa Israel isistishe mapigano na Hamas maana kwa Sasa wanaoumia sio Hamas ni raia wa kawaida wa Gaza. Kama ni kisasi kimeshalipwa. Maana mpaka Sasa wameuawa wapalestina 11,500. Ambao watoto waliokwisha uawa wanakaribia 5,000 hii inaumiza Sana.

IDF kashamsambaratisha Hamas sidhani Kama Kuna haja ya kuendelea na mashambulizi. Kwa Sasa Hamas Hana nguvu na wapalestina wamejifunza kwamba mbeleni wasifanye uchokozi kwa Israel wa aina ile.

Kuna mambo matatu nimeyaona yamenifanya nifikirie hivyo.

1. Kwanza, Jana Israel kashambulia na kuilipua kwa makombora shule ya watoto na kuua watu hamsini ikiwemo watoto wadogo. Shule hiyo inaitwa Al Buraq, na inasemekana mjukuu wa kiongozi mkuu wa Hamas Ismail Haniyeh aliuawa kwenye mashambulizi hayo.

Sababu kuu ya IDF kuishambulia shule hiyo ni baada ya kamanda wa Hamas Ahmed Siam aliyekuwa kwenye mapambano na IDF kwenye eneo la Hospitali ya Rantisi Kuzidiwa na kwenda kujificha kwenye shule hiyo. Hivyo Israel ikaona immalize pamoja na watoto waliokuwemo humo. Kwa kweli niliumia kuona watoto wasiokuwa na hatia wakiuawa kwa ujinga wa Hamas. Nikawaza itakuwaje kwa huko mbeleni?.

2. Pili, Kuna Jambo la kusikitisha kwenye Hospitali ya Al Shifa. Ni kwamba IDF imeizunguka hiyo Hospitali na kuanza mashambulizi. Tatizo ni kwamba Kuna vitoto vichanga karibia 39 vimo humo ndani, ndio kwanza vipo kwenye incubator. Sasa ninachoogopa IDF asije akailipua Hospitali nzima na kuua hao watoto.

Nasema hivyo kwa sababu IDF anaweza kuilipua Hospitali nzima ya Al Shifa kwa kuwa kiongozi wa Hamas Yahya Sinwar kajificha humo pamoja Viongozi wachache waliobakia.

Kingine ni kwamba ndani ya Hospitali hiyo Kuna wagonjwa wengi mahtuti na wazee. Hivyo kuilipua itasababisha mauaji ya halaiki.

3. Tatu, iwapo IDF itailipua Hospitali hiyo Kuna uwezekano wa Mataifa ya kiarabu kulazimishwa kuingilia kati na kuendeleza mgogoro kuwa mkubwa na kupelekwa hata vita vya tatu vya dunia.

Maana Al Shifa imekuwa Kama mtego. Ndio maana Hamas wameruhusu watu wengi wawe pale ili Israel asipate nafasi ya kuishambulia. Maana lile ndio eneo la mwisho kabisa kwa Hamas kujilinda. Hivyo hakuna haja ya kumwaga damu nyingi. Wakubaliane Israel asogee nyuma na Hamas wawaachie mateka basi. Mambo mengine yaendelee.

Hivyo basi, naishauri Israel ifanye yafuatayo.

1. Kutangaza kusitisha haya mapigano, maana wanaoadhirika ni watoto, wanawake na wazee na sio Hamas Tena.

2. Israel atangaze kuwepo na Kambi ya jeshi itakayosimamiwa na Umoja wa Mataifa. Kambi hiyo iwe kilometa ishirini kati ya mpaka wa Israel na Gaza.

3. Israel ifanye makubaliano na Hamas ya kuondoka Al Shifa na Hamas wawaachie mateka waliowashika. Na makubaliano haya yasimamiwe na Umoja wa Mataifa.

4. Jukumu la kuisimamia Gaza liwe chini ya Mahmoud Abbas ambaye kisheria ndio Rais wa Palestina, Gaza ikiwemo. Ili kuendeleza makubaliano ya Oslo ya mwaka 1993 ili mchakato wa kuanzisha taifa la Palestine lianze..

4. Nanshauri kuwepo na makubaliano kati ya Palestina kwa niaba ya Hamas na Israel upande mwingine , kwamba hawatovamiana Tena.


Hao magaidi ndo wanaua hao watoto, sio Israel, hamas wamejenga mahandaki chini ya hizo shule na hospital, hakuna namna, watauwawa tu.
 
ingeshatosha kitambo, lakini haiwezi kutosha wakati hamas bado wanaendelea kurusha roketi na bado wameshikilia raia wao kama mateka. naamini kama wangeachia mateka na wangeacha kurusha roketi jamani israel nao ni wanadamu wangeona aibu, wangeweza kusitisha. lakini unaambiwa usitishe wakatu mtu ananyesha mvua ya roketi kwa watoto wako na amekamata mateka wako hataki kuachia, inawezekana kweli?

Kwa Sasa Hamas Hana uwezo wa kurusha roketi. Roketi anarusha Hizbollah. Kwa kuwa Israel kashamdhibiti Hamas , ni Bora wakubaliane wawaachie mateka na Hamas waliobakia waendee Misri au Lebanon.
 
Hapo wa kulaumiwa ni Hamas, kwa nini wanapigana vita halafu wanakimbilia kujificha hospitali?!
Ukute kuna lango la kuingilia kwenye mtandao wa mahandaki humo hospital.
Naunga mkono hoja kama tu Hamas wakiachia mateka, vinginevyo kipigo kiendelee

Hamas ni wajinga Sana. Na sidhani Kama wanawapigania wapalestina. Maana ni hao Hamas waliwatimua PLO au Fatah hapo Gaza ili wabaki wenyewe, na kujifanya Gaza kujitawala. Nadhani wakiondoka Palestina itakuwa huru.
 
Back
Top Bottom