Israel ni nchi ya Wayahudi, soma Hesabu 34:1-15

Israel ni nchi ya Wayahudi, soma Hesabu 34:1-15

1. Kabla ya Israel kuwekwa pale mwaka 1948 kulikuwa na utawala wa kikoloni wa Uingereza (British Mandate), hii haikuwa Taifa la Palestina
Kabla ya 1960 kulikua na taifa la Tanganyika au Rwanda au Burundi? Je ina maana turuhusu tu wayahudi waichukue Tanzania sababu hakukuwahi kuwa na taifa la Tanzania kabla ya 1960??

Tuanzie hapa
 
19. Kabla ya makabila 12 kulikuwa utawala wa dola ndogo ndogo za Caanan, nayo haikuwa Palestina
Point ni kwamba Israel hapakua kwao hapo walipora kwa kuchinja watu wote waliowakuta yaani ndio genocide ya kwanza duniani!!

Sasa kama wao walikuta watu wakaishi, na baadae wakaondoka wakaja wengine kwanini iwe nongwa? Je mfano jamii ya vizazi vya caanan nao wakijitokeza wakadai hiyo palestina patatosha hapo?

Hata Tanzania kuna watu walitoka magharibi ya Afrika na wengine pembe ya Afrika ndio wakaunda hii nchi je leo mfano wasukuma nao wana haki ya kwenda kuidai Ghana au Ivory Coast?
 
2. Kabla ya Ukoloni wa Mwingereza mwaka 1917 kulikuwa utawala wa Dola ya Ottoman, hii pia haikuwa Palestina
Tanganyika kabla ya 1960 ilikua chini ya Uingereza kabla ya hapo chini ya mjerumani na kabla ya hapo mwambao wa pwani ulikua chini ya sultan wa zanzibar!! Tanganyika haikuwahi kuwa taifa!! Hivyo basi ni halali mtu yeyote kuja kulichukua hili taifa maana halikuwa kuwa taifa la watanganyika!!

Kwahiyo British Palestine walikua wanaishi wazungu si ndio? Kazi kwelikweli
 
Swala la msingi ni kuwa wayahudi hawaamini katika Christ au bible,

Sasa wanapata Imani ya nchi yao kama kitabu au nabii aliwanyanyua hawamuamini,

Huu ni uwendawazimu Tu, how do you justify something from nothing (unbelievable things)
Umepotosha. Wayahudi wanafuata Agano la Kale kama Wakristu. Mwendawazimu ni wewe
 
Kabla ya 1960 kulikua na taifa la Tanganyika au Rwanda au Burundi? Je ina maana turuhusu tu wayahudi waichukue Tanzania sababu hakukuwahi kuwa na taifa la Tanzania kabla ya 1960??

Tuanzie hapa
Kama nilivyokuwekea diaspora ya wana wa Israel pale kwenye post namba 73. Wenyewe walitoka, na ilipofika muda wakatudi kwenye nchi yao
 
Point ni kwamba Israel hapakua kwao hapo walipora kwa kuchinja watu wote waliowakuta yaani ndio genocide ya kwanza duniani!!

Sasa kama wao walikuta watu wakaishi, na baadae wakaondoka wakaja wengine kwanini iwe nongwa? Je mfano jamii ya vizazi vya caanan nao wakijitokeza wakadai hiyo palestina patatosha hapo?

Hata Tanzania kuna watu walitoka magharibi ya Afrika na wengine pembe ya Afrika ndio wakaunda hii nchi je leo mfano wasukuma nao wana haki ya kwenda kuidai Ghana au Ivory Coast?

Ni mpaka Mwaka 1947 umoja wa mataifa ukaandaa mpango wa kugawa ardhi ya Palestina ili kuwe na mataifa mawili, la waarabu ambalo litaitwa Palestina na la wayahudi ambalo litaitwa Israel, Mji wa Jerusalem ukaachwa kama ukanda huru kutokana na umuhimu wake katika dini zote tatu za eneo lile.

"Ramani ya pendekezo la umoja wa mataifa mwaka 1947 kuigawa ardhi ili kuwe na mataifa mawili"
asa-1.png


Waarabu wakaukataa mpango huu lakini wayahudi wakaupokea na kuanzisha taifa lao la Israel, na waarabu kujikuta ndani ya taifa hilo.
 
Tanganyika kabla ya 1960 ilikua chini ya Uingereza kabla ya hapo chini ya mjerumani na kabla ya hapo mwambao wa pwani ulikua chini ya sultan wa zanzibar!! Tanganyika haikuwahi kuwa taifa!! Hivyo basi ni halali mtu yeyote kuja kulichukua hili taifa maana halikuwa kuwa taifa la watanganyika!!

Kwahiyo British Palestine walikua wanaishi wazungu si ndio? Kazi kwelikweli
Hakujawahi kuwa na Taifa linaitwa Palestina!! Rudi tena kwenye post yangu #73
 
Ni mpaka Mwaka 1947 umoja wa mataifa ukaandaa mpango wa kugawa ardhi ya Palestina ili kuwe na mataifa mawili, la waarabu ambalo litaitwa Palestina na la wayahudi ambalo litaitwa Israel, Mji wa Jerusalem ukaachwa kama ukanda huru kutokana na umuhimu wake katika dini zote tatu za eneo lile.

"Ramani ya pendekezo la umoja wa mataifa mwaka 1947 kuigawa ardhi ili kuwe na mataifa mawili"
asa-1.png


Waarabu wakaukataa mpango huu lakini wayahudi wakaupokea na kuanzisha taifa lao la Israel, na waarabu kujikuta ndani ya taifa hilo.
Hujajibu hoja bado? Kabla ya wayahudi kina yakobo kuishi hapo palestina ilikua chini ya nani?

Maana yake walikua wahamiaji tu sasa kwanini wajimilikishe eneo ambalo hata wao wamekuta lina wenyeji?
 
Umepotosha. Wayahudi wanafuata Agano la Kale kama Wakristu. Mwendawazimu ni wewe
Hawafuati agano la kale ni vitabu vichache tu ndio wanaamini!! Kwanza hawaamini Yesu ni Mungu meaning hao sio imani sawa na wakristo maana Mungu wao na Mungu wa wakristo ni tofauti kabisa!!
 
Kama nilivyokuwekea diaspora ya wana wa Israel pale kwenye post namba 73. Wenyewe walitoka, na ilipofika muda wakatudi kwenye nchi yao
Naongelea kabla ya yakobo hata Abraham nchi ilikua na mfalme tayari. In fact Abraham alikuta wafalme kibao tu hapo na hata Jerusalem ilikua na mfalme wake kabisa.

Je leo wakitokea wacanaan wakadai hiyo ardhi mpo tayari kuwapisha?

Lakini pia kibiblia kama ardhi alirithishwa Abraham ambaye ana watoto kibao ni kwanini ajimilikishe yakobo na wanawe ilihali Abraham alikua na warithi kibao tu?
 
Umepotosha. Wayahudi wanafuata Agano la Kale kama Wakristu. Mwendawazimu ni wewe
Hujaona wakatoliki wanavotemewa mate kule Jerusalem,

Kama hujui, wakristo ni watu wa hadhi ya chini kabisa pale TelaViv
 
Hujajibu hoja bado? Kabla ya wayahudi kina yakobo kuishi hapo palestina ilikua chini ya nani?

Maana yake walikua wahamiaji tu sasa kwanini wajimilikishe eneo ambalo hata wao wamekuta lina wenyeji?
Kab la ya Wayahudi kama Yakobo (karne ya 19 KK), eneo la Palestina (au Kanaani) lilikuwa na wenyeji asili kama Wakanaani, na mara nyingi chini ya ushawishi wa Misri au falme zingine za Mashariki ya Kati. Wayahudi walifika kama wahamiaji, na madai ya umiliki yanatokana na historia, dini na migogoro ya kisasa.
 
Hawafuati agano la kale ni vitabu vichache tu ndio wanaamini!! Kwanza hawaamini Yesu ni Mungu meaning hao sio imani sawa na wakristo maana Mungu wao na Mungu wa wakristo ni tofauti kabisa!!
Dini ya Wayahudi (Uyahudi au Judaism) inafuata Agano la Kale (Old Covenant au Old Testament katika mtazamo wa Kikristo).Hii inajulikana kama Tanakh (Biblia ya Kiebrania), ambayo inajumuisha hasa Torah (Sheria ya Musa), Nevi'im (Manabii), na Ketuvim (Maandiko mengine). Hii ndiyo msingi wa imani na sheria za Wayahudi.Wayahudi wengi wanaamini kwamba agano hili (covenant) kati ya Mungu na Waisraeli (kupitia Abrahamu, Musa n.k.) bado linaendelea na halijabadilishwa au kuondolewa.
 
Naongelea kabla ya yakobo hata Abraham nchi ilikua na mfalme tayari. In fact Abraham alikuta wafalme kibao tu hapo na hata Jerusalem ilikua na mfalme wake kabisa.

Je leo wakitokea wacanaan wakadai hiyo ardhi mpo tayari kuwapisha?

Lakini pia kibiblia kama ardhi alirithishwa Abraham ambaye ana watoto kibao ni kwanini ajimilikishe yakobo na wanawe ilihali Abraham alikua na warithi kibao tu?
Ndiyo, kabla ya Abraham, Kanaani ilikuwa na wafalme wengi (Salem, Sodom, Gomorra n.k.). Leo kama Wacanaan wangetokea na kudai ardhi hiyo kwa haki ya kihistoria, wengi hawangekubali kuwapa kwa sababu ya mabadiliko ya wakati na historia ndefu.Kibiblia, ahadi maalum ilipewa Isaka kisha Yakobo (sio kwa Ismael, Esau wala wengine), kwa sababu Mungu alichagua line moja ya agano (si warithi wote wa Abraham). Hivyo ni chaguo la Mungu, si wingi wa watoto
 
Hujaona wakatoliki wanavotemewa mate kule Jerusalem,

Kama hujui, wakristo ni watu wa hadhi ya chini kabisa pale TelaViv
Acha kudanganya watu. Mimi ni Mkristu Mkatoliki, nimetembea Israel mwaka 2006 nikakaa mwezi mzima na mwaka 2010 nikaishi majuma 2. Hakuna ubaguzi wa dini wowote kati ya dini ya Wayahudi vs Christianity au Wayahudi vs Islam.

Mnadanganywa sana na mitandao
 

Mwanzo 15:18 Siku ile Bwana akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,

Unadhani uzao wa Abraham unaoongelewa hapa ni upi?

Ni huu Abraham-Izaka-Yakobo
JIBU SWALI

Mwanzo 15 niliyotaja mimi inatamka Middle East nzima kupewa Israelites.

Wewe umetoa mstari tofauti unaotaja mipaka tofauti, Kaanani tu!

Nakuuliza sasa, wewe Mhubiri. Ni nchi gani, eneo gani, mipaka ipi twende nayo kati ya hiyo miwili kwenye biblia?

Umeelewa swaliiii ???

KINGINE nikakuuliza:

Umesema Wapalestina walivamia eneo. Jeeee, Waisraeli walipopewa eneo hilo Kaanani, au Middle East yote ( Mwanzo 15:18) palikuwa ni kama pori la Mabwepande ????
 


JIBU SWALI

Mwanzo 15 niliyotaja mimi inatamka Middle East nzima kupewa Israelites.

Wewe umetoa mstari tofauti unaotaja mipaka tofauti, Kaanani tu!

Nakuuliza sasa, wewe Mhubiri. Ni nchi gani, eneo gani, mipaka ipi twende nayo kati ya hiyo miwili kwenye biblia?

Umeelewa swaliiii ???

KINGINE nikakuuliza:

Umesema Wapalestina walivamia eneo. Jeeee, Waisraeli walipopewa eneo hilo Kaanani, au Middle East yote ( Mwanzo 15:18) palikuwa ni kama pori la Mabwepande ????
Kama unazungumzia ahadi ya awali kwa Abrahamu na maono ya Mungu ya mwisho, tumia Mwanzo 15 (eneo kubwa la Middle East).
Kama unazungumzia nchi ambayo Waisraeli walipewa kuichukua na kuishi (kama ilivyoelezwa wakati wa Musa na Yoshua), tumia Hesabu 34 (Kaanani yenye mipaka maalum).
Wengi wa Wakristo na Wayahudi wanaona Hesabu 34 kama mipaka ya urithi wa karibu (actual conquest), na Mwanzo 15 kama ahadi ya baadaye au ya kiroho/ya kimessia. Hakuna "contradiction" – ni vipimo viwili vya ile ile ahadi, moja pana na moja maalum.
Kwa muhtasari: Kwa maisha ya kila siku na historia ya Israeli ya kale, Hesabu 34 (Kaanani) ndiyo mipaka iliyotumiwa. Lakini ahadi ya Mungu kwa Abrahamu inabaki kuwa kubwa zaidi
 
Back
Top Bottom