Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,397
- 829,701
Kasumba Bekar, kijana mwenye umri wa miaka 21, mfuasi wa Bobi Wine na mmoja wa vijana wanaomkosoa Rais Yoweri Museveni mitandaoni, alitekwa juzi na watu wasiojulikana. Leo ameokotwa eneo la Kasanda (nje kidogo ya jiji la Kampala) akiwa amepigwa hadi kupoteza fahamu, na mikononi amepigiwa misumari.
Huyu ni mfuasi mwingine wa Bobi Wine kufanyiwa vitendo vya kikatili na watu wasiojulikana katika kipindi cha hivi karibuni. August 5 mwaka huu mwanamuziki Ziggy Wine, ambaye alikua akifanya kazi kwenye label ya Bobi nae alitekwa, kupigwa na kutobolewa macho, siku chache baada ya kuandika mtandaoni kuwa Rais Museveni hana tena uhalali wa kuongoza nchi hiyo. Ziggy aliokotwa akiwa mahututi lakini alifariki siku chache baadae.
Bobi Wine ametuhumu vyombo vya usalama kuhusika na vitendo hivyo vya kikatili, lakini Polisi nchini Uganda wamekanusha madai hayo na kusema wanawatafuta wahalifu wanaofanya vitendo hivyo ili kuwafikisha mahakamani.!
Huyu ni mfuasi mwingine wa Bobi Wine kufanyiwa vitendo vya kikatili na watu wasiojulikana katika kipindi cha hivi karibuni. August 5 mwaka huu mwanamuziki Ziggy Wine, ambaye alikua akifanya kazi kwenye label ya Bobi nae alitekwa, kupigwa na kutobolewa macho, siku chache baada ya kuandika mtandaoni kuwa Rais Museveni hana tena uhalali wa kuongoza nchi hiyo. Ziggy aliokotwa akiwa mahututi lakini alifariki siku chache baadae.
Bobi Wine ametuhumu vyombo vya usalama kuhusika na vitendo hivyo vya kikatili, lakini Polisi nchini Uganda wamekanusha madai hayo na kusema wanawatafuta wahalifu wanaofanya vitendo hivyo ili kuwafikisha mahakamani.!


