Ismail Ramadhan, aliyemuua mwenzake kisa mapenzi, ahukukumiwa mwaka mmoja jela

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,981
Hakimu Mkazi Mkuu, Joyce Minde, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu amemuhukumu mkazi wa Vingunguti, Dar es Salaam, Ismail Ramadhan, kwenda jela mwaka mmoja, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumuua mwenzake bila kukusudia wakiwa wanagombania mwanamke. baada ya mshitakiwa kukiri kosa, wakati shauri hilo lilipopelekwa kwa ajili ya kuanza usikilizwaji upande wa mashitaka.

Mshitakiwa huyo, kabla ya kuanza na usikilizwaji wa shauri hilo upande wa mashitaka waliomba kumkumbusha mshitakiwa kosa lake ambapo baada ya kukumbushwa alikiri kosa la kuua bila kukusudia.

Baada ya mshitakiwa kukiri alisomewa maelezo ya awali na wakili wa Serikali Mosie Kaima kisha mshitakiwa kusomewa maelezo ya awali.

Wakili Mosie alidai Novemba 13, mwaka 2015, maeneo ya Vingunguti mji mpya wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, mshitakiwa alimuua Mohamed Kamogela bila kukusudia.

Alidai siku hiyo saa 2, usiku mtuhumiwa walikuwa wanagombania mwanamke ambaye anaitwa Ester ambaye walikuwa wanamahusiano naye kwa muda tofauti.

Wakili Mosie alidai ugomvi huo uliibuka baada ya marehemu kumtuhumu kuwa anaendelea na huyo mwanamke huku mshitakiwa akamueleza kwamba hana tena mahusiano wa kimapenzi na huyo mwanamke.

Alidai wakati wa mabishano hayo marehemu alikuwa ameambatana na watu wanne wakiwa na mapanga ambapo walianza kumpiga mshitakiwa kwa bapa na mapanga hayo.

Akiendelea kusoma maelezo hayo, Wakili Mosie alidai wakati tukio hilo linaendelea kuna mtu ambaye alijulikana kwa jina la Ally rafiki na mshitakiwa akiwa eneo hilo alimrushia kisu ili aweze kujiokoa.

Baada ya kudaka kisu hicho mshitakiwa alikitumia kisu hicho na kisha alimchoma katika mkono wa kushoto ambapo marehemu alikimbia na kuangukia varanda ya nyumba ambayo ilikuwa karibu na eneo hilo kisha kufariki.

Marehemu baada ya kufariki askari polisi walipata taarifa ambapo mwili wa marehemu ulichukuliwa na kupelekwa hospitali ya Amana na kisha Hospitali ya Taifa Muhimbili na katika uchunguzi ulibaini kuwa alipoteza damu nyingi.

Alidai askari polisi walikwenda eneo la tukio kisha kuchora ramana na Novemba 16, mwaka 2015 mshitakkwa alikamatwa.

Baada ya maelezo hayo mshitakkwa alikiri kosa la kuua bila kukusudia na Hakimu Joyce alisema Mahakama inamtia hatiani kama alivyoshitakiwa.

Kabla ya kutolewa kwa adhabu hiyo, Wakili wa Serikali Mosie, aliomba Mahakama itoe adhabu kwa mujibu wa sheria kwani mshitakkwa alitumia kisu kumchoma marehemu.

," Marehemu akiwa na wenzake kama walikuwa wanataka kumuua mshitakkwa wangemuua muda mfupi, hawakuwa na nia ya kumuua, hivyo mshitakiwa apewe adhabu kwa mujibu wa sheria," alidai.

Kwa upande wa Wakili wa utetezi, Yohana Kibinda, aliomba Mahakama kwamba mteja wake amekaa gerezani kwa kipindi cha miaka saba ni muda mrefu kwani wakati huo alikuwa na miaka 20.

," Mteja wangu hakuwa na nia ya kumuua marehemu bali alitaka kujiami na kujiokoa kwa bahati mbaya wakati wa purukushani aliweza kuua bila kukisudia

Kwani ugomvi unatokea mshitakiwa hakuwa na silaha, hivyo hakuwa na nia ya kusababisha kifo naomba apewe adhabu nafuu ili aweze kutumikia taifa lake kwani ana wazazi na mtoto mdogo wanamtegemea, "alidai
 
Hizi manslaughter cases za bongo ni za ajabu Sana. Kama ile ya Ditopile. Lakini laana Bado inaandama familia yake Binti yake Kawa msagaj aliyekubuhu anatongoza wanawake wenzake kwa nguvu na kuwahonga na wivu juu .

Yule wa Mjengoni?
 
Hakimu Mkazi Mkuu, Joyce Minde, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu amemuhukumu mkazi wa Vingunguti, Dar es Salaam, Ismail Ramadhan...
Kama maelezo ya polisi ni ya kweli na kwamba hakuna mchongo kifungo alichofungwa sii haki.
Angalau basi kingekuwa kifungo cha nje.

Ukosefu wa msukumo kwa sheria na kanuni za kutoa haki kwa wakati nchini zimepelekea mtuhumiwa kutumikia kifungo cha miaka saba bila hukumu ya mahakama ya sheria.

Hii nayo ni aibu kwa mahakama zetu.
 
Hakimu Mkazi Mkuu, Joyce Minde, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu amemuhukumu mkazi wa Vingunguti, Dar es Salaam, Ismail Ramadhan, kwenda jela mwaka mmoja, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumuua mwenzake bila kukusudia wakiwa wanagombania mwanamke. baada ya mshitakiwa kukiri kosa, wakati shauri hilo lilipopelekwa kwa ajili ya kuanza usikilizwaji upande wa mashitaka.

Mshitakiwa huyo, kabla ya kuanza na usikilizwaji wa shauri hilo upande wa mashitaka waliomba kumkumbusha mshitakiwa kosa lake ambapo baada ya kukumbushwa alikiri kosa la kuua bila kukusudia.

Baada ya mshitakiwa kukiri alisomewa maelezo ya awali na wakili wa Serikali Mosie Kaima kisha mshitakiwa kusomewa maelezo ya awali.

Wakili Mosie alidai Novemba 13, mwaka 2015, maeneo ya Vingunguti mji mpya wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, mshitakiwa alimuua Mohamed Kamogela bila kukusudia.

Alidai siku hiyo saa 2, usiku mtuhumiwa walikuwa wanagombania mwanamke ambaye anaitwa Ester ambaye walikuwa wanamahusiano naye kwa muda tofauti.

Wakili Mosie alidai ugomvi huo uliibuka baada ya marehemu kumtuhumu kuwa anaendelea na huyo mwanamke huku mshitakiwa akamueleza kwamba hana tena mahusiano wa kimapenzi na huyo mwanamke.

Alidai wakati wa mabishano hayo marehemu alikuwa ameambatana na watu wanne wakiwa na mapanga ambapo walianza kumpiga mshitakiwa kwa bapa na mapanga hayo.

Akiendelea kusoma maelezo hayo, Wakili Mosie alidai wakati tukio hilo linaendelea kuna mtu ambaye alijulikana kwa jina la Ally rafiki na mshitakiwa akiwa eneo hilo alimrushia kisu ili aweze kujiokoa.

Baada ya kudaka kisu hicho mshitakiwa alikitumia kisu hicho na kisha alimchoma katika mkono wa kushoto ambapo marehemu alikimbia na kuangukia varanda ya nyumba ambayo ilikuwa karibu na eneo hilo kisha kufariki.

Marehemu baada ya kufariki askari polisi walipata taarifa ambapo mwili wa marehemu ulichukuliwa na kupelekwa hospitali ya Amana na kisha Hospitali ya Taifa Muhimbili na katika uchunguzi ulibaini kuwa alipoteza damu nyingi.

Alidai askari polisi walikwenda eneo la tukio kisha kuchora ramana na Novemba 16, mwaka 2015 mshitakkwa alikamatwa.

Baada ya maelezo hayo mshitakkwa alikiri kosa la kuua bila kukusudia na Hakimu Joyce alisema Mahakama inamtia hatiani kama alivyoshitakiwa.

Kabla ya kutolewa kwa adhabu hiyo, Wakili wa Serikali Mosie, aliomba Mahakama itoe adhabu kwa mujibu wa sheria kwani mshitakkwa alitumia kisu kumchoma marehemu.

," Marehemu akiwa na wenzake kama walikuwa wanataka kumuua mshitakkwa wangemuua muda mfupi, hawakuwa na nia ya kumuua, hivyo mshitakiwa apewe adhabu kwa mujibu wa sheria," alidai.

Kwa upande wa Wakili wa utetezi, Yohana Kibinda, aliomba Mahakama kwamba mteja wake amekaa gerezani kwa kipindi cha miaka saba ni muda mrefu kwani wakati huo alikuwa na miaka 20.

," Mteja wangu hakuwa na nia ya kumuua marehemu bali alitaka kujiami na kujiokoa kwa bahati mbaya wakati wa purukushani aliweza kuua bila kukisudia

Kwani ugomvi unatokea mshitakiwa hakuwa na silaha, hivyo hakuwa na nia ya kusababisha kifo naomba apewe adhabu nafuu ili aweze kutumikia taifa lake kwani ana wazazi na mtoto mdogo wanamtegemea, "alidai
Ester kazua balaa
 
rumande miaka 7 , hukumu mwaka moja, aisee

Self defense anafungwaje?

Mtu anakaa rumande miaka saba asee

Kama maelezo ya polisi ni ya kweli na kwamba hakuna mchongo kifungo alichofungwa sii haki.
Angalau basi kingekuwa kifungo cha nje.
Ukosefu wa msukumo kwa sheria na kanuni za kutoa haki kwa wakati nchini zimepelekea mtuhumiwa kutumikia kifungo cha miaka saba bila hukumu ya mahakama ya sheria.
Hii nayo ni aibu kwa mahakama zetu.
System ya Bongo ndugu yako likimpata balaa kama hili na case ikabadirishwa kutoka murder case mpaka manslaughter ushukuru Mungu tu upambane atatoka, maana ikibaki murder ni issue ya mahakama kuu Kwa Jaji.

Huyo ninaamini alikuwa na murder case ndio walipombadirishia shtaka baada ya kusota jela amekubali kosa ndio hukumu ikaja hivyo.
 
System ya Bongo ndugu yako likimpata balaa kama hili na case ikabadirishwa kutoka murder case mpaka manslaughter ushukuru Mungu tu upambane atatoka, maana ikibaki murder ni issue ya mahakama kuu Kwa Jaji.

Huyo ninaamini alikuwa na murder case ndio walipombadirishia shtaka baada ya kusota jela amekubali kosa ndio hukumu ikaja hivyo.
Sasa hapa amehukumiwa kwa kosa lipi wakati ni salf defense?
 
Manslaughter na ameshakaa jela miaka 7, ni hukumu ya haki, jumla miaka 8 hapo atakuwa amejifunza mbunye haigombaniwi.
halafu kumbe alikuwa na miaka 20 kipindi hiko, aisee vijana Hawa Wana usela mavi sana,
Self defense anafungwaje?
Sheria zetu za hovyo,unaweza ukavamiwa na vibaka kwako,ukifanikiwa kumuua mmoja usishangae ukafungwa wewe , yaani bora wakuue wewe au wakujeruhi nadhani.
 
Mtu anakaa rumande miaka saba asee
Kesi za mauji unakaa jela muda mrefu, nafikiri pia Ni kwa usalama wako, maana Kama ukikosekana ushaidi ndani ya mwaka mmoja na ukaachiwa huru, unafikiri ndugu wa marehemu watakuacha hivihivi? ni afadhali wakisikia bado upo gerezani huku kesi ikipigwa kalenda kidogo hasira zinawapungua hata Kama ndugu yao ambae ni marehemu alikuwa teja asiye na msaada kwa familia
 
Back
Top Bottom