Umeongea kwa lugha ya mjinga lakini kuna ukweli mwingi ktkt maneno yako.Labda ni vyema muungano usingetokea kabisa kuliko kuzungumzia kuuvunja. Maana vilivyoshikana havitaacha kunyofoana ikibidi kutengana. Pia si wazanzibari tu bali wote wana manufaa na Muungano. Kwa Bara ni prestige na labda kuhofia usalama. Na hilo si jambo dogo. Wazanzibari wanapata soko la means of labour.Huyu ni Jusa au Juha? Maana sioni anachoongea zaidi ya kuzua. Kwa mfano anasema eti Nyerere ni adui wa Zanzibar asijue kuwa muungano ukivunjika watapinduana kama Comoro! Ni mwendawazimu wa kiwango cha kutisha anayeweza kusema haya. Juha hajui kuwa tukivunja huo muungano na kuwataka wanzanzibari waliozaliana bara watakosa pa kuwaweka! Amesahau jinsi Mtikila alivyoungwa mkono na watanganyika kama ishara yao kuwa na hasira na ma********* hawa! Juha anapinga kuwa hatuwapi umeme bure ukiachia mbali mchele wetu wanaoupenda sana! Juha kashiba sana kiasi cha kujiropokea asijue anakata tawi alilokalia. Kama matone ya mafuta yanaanza kuwatoa roho waroho hawa, kama kweli yatakuwapo itakuwaje? Akina Juha na wengine wenye mawazo kama yao wanapaswa waambiwe: kama wamechoka na muungano na wana ubavu na hoja wapeleke hoja ya kuvunja huo muungano waone kama ni rahisi na ni nani ataanza kulia.Jusa kimsingi, kaongelea personalities badala ya issues. Mie nadhani wanzanzibari waache unafiki wa kula huku na kule. Waseme wamechoka muungano na uvunjwe tuone. Pia waache mchezo mchafu wa changu kichungu chako kitamu.