Natumaini wanajamvi wote wazima...nimewamiss wote baada ya kuadimika kwa muda kidogo.
Back to the topic, Kuna kaka niliwahi kua na mahusiano nae miaka kama mitatu iliyopita, nilimpenda sana lakini tuliachana baada ya kugundua alikua ananicheat, niliumia sana kwani nilimpenda ila sikua na jinsi sababu alinidanganya.
Maisha yaliendelea na nikamsahau kabisa. Yapata kama miezi miwili sasa huyu kaka amekua akiniandikia na kunipigia na bila kuchanganya maneno aliniambia anajutia kosa alilofanya na anaomba tuanze upya9 mwanzo aliomba msamaha nikamwambia nimemsamehe ila tusiendelee).
Sijamkubalia ila nimekua nikimuuliza kwanini amerudi wakati alinichanganya akadai ule ulikua ni ujana unamsumbua na hakua amewaza kusettle bado ila sasa anataka kuoa na kutulia hivyo anaomba nimkubalie niwe nae.
Kwa upande wangu siwezi sema namchukia ila alichofanya nilichukulia kama challenge za mahusiano nika move on.
Hivi amerudi kuna sparks na feelings kwake zinarudi ila siziamini ukizingatia tuko mbali nimemuambia tuwe tu marafiki (najipa muda kumsoma kama amebadilika naweza rudiana nae sipo kwenye mahusiano kwa sasa na kama nimpango wa Mungu huko mbeleni mengine yatakua.)
Kilichonifanya nije kwenu niombe mawazo yenu nashindwa kujua kama yupo serious? Nini kitanihakikishia kua hataniumiza tena?
Naamini wapo waliona experience ya urudiana na ex watanisaidia lakini na pia naamini people desrve a second chance if they earn it!
Nadhani nimeeleweka mnisamehe mimi sio mwandishi mzuri ila nimejitahidi kuwasilisha la moyoni.
Natanguliza shukrani.
Kusema kwa experience nilyopitia hata sikushauri urudiane unless kama unataka kulizwa tena . I have learned that a cheater is a cheater they will be always a cheater. Move on my dear I know you are lonely now . Jitahidi kujikeep busy. I remember nilipoachana na ex wangu ni sababu hiyo hiyo nilimsamehe akarudia tena na tena . Nilikuwa na volunteer sana kanisani kujikeep busy ya kumsahau ilinidaidia sana sana . Dada move on mume wako yuko njiani . Asante.