Ukishaona mjadala na maswali kuhusu uwepo wa Mungu (awali ya yote nakusudia Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na nwenye upendo wote), huo mjadala tu ni ushahidi kuwa Mungu huyo hayupo.
Kwa sababu Mungu huyo mwenye sifa hizo hatakiwi kuwa mkatili hivyo kuwanyima uwezo watu kujua kwa uhakika, bila mjadala wala maswali, kuwa yeye Mungu yupo.
Mungu angekuwapo kweli, isingewezekana kuwa na mjadala kuhusu uwepo wake.
Uwepo wake ungejulikana, ungejulikana kwa wote, wakati wote, pahali pote, muda wote, bila shaka yoyote, kwa namna ambayo mjadala kuhusu uwepo wake usingewezekana.
Kwa hiyo, ukiona swali, mjadala, mabishano yoyote, kuhusu uwepo wa Mungu, hilo swali, huo mjadala, hayo mabishano, ni uthibitisho kuwa huyo Mungu hayupo.
Yani huyo Mingu ni kwa kwenye hadithi za kutungwa na watu tu, zaidi ya hizo hadithi, hayupo.