Wazee wa THIBITISHA.
Kwa akili zetu finyu na limited tunamuwekea Mungu standards za kuthibiitishwa kama juice za moo! kama TBS yani!
Kwa akili zetu chache, tunataka kumpangia, Mungu nini afanye na nn asifanye. "kama kuna mungu kwa nini kuna njaa" moja ya reasoning ya kipuuzi kabisa
Mungu ni mysterious, sisi binadamu atuwezi kumfahamu kama tunavyotamani kumfahamu, kitendo cha kuanziasha mjadala kama huu na kuomba uthibitisho wake ni jibu kuwa mnaamini Mungu yupo lakini ni mysterious one, na yeye yupo nje ya uelewa wetu, kushindwa kumthibitisha hakufanyi Mungu hayupo bali kunaonesha sisi ni wadunchu sana kwake kupata majibu ya tunayo jiuliza. Mungu haitaji uthibitisho mkubwa wa kisayansi na vitabu pages kwa pages No. ni simple common sense ya mtoto wa miaka 9 inakwambia Mungu yupo
Mfano wa sisimizi na binadamu, Inawezekana sisimizi akawa anakuwaza min -me kama ni limungu flani unaweza ukambinya sisimizi kwa kijidole tu akakulaani au unaweza kudondosha visukari sisimizi akapita akakuona bonge la msaada, lakin milele sisimizi huo asielewe kwanini na kivipi unaweza kufanya unayomfanyia na sisimizi huyo anaweza akakuhoji kama wewe ni mungu au ni kiumbe gani lakini hasipate majibu, Kumbuka mpaka sisimizi amefika hatua ya kuhoji ni kwamba ameshakumbana na mikasa kwa kubinywa na kidole chako na mkasa wa kupewa sukari, so technically anajua kuna likiumbe lipo ila hana majibu nalo ni likiumbe la aina gani.
sijui kama nimeleweka! lakini sisi ni visismizi kwa Mungu. Kwa maswali yetu tunaojiuliza kila leo tukiyageuza kinyume ni dhahiri mnamzidi ku prove Uwepo wa Mungu na ukuu wake.