Mkuu;pole Sana. Kiranga hafundishiki lakini huwa tunamtumia Kama ubao wa kufundishia wengine.
Katika hilo anafaa Sana.
Tusimwache aendelee kumwaga uchafu wake ambao waweza kuharibu watu wengine wasio na uelewa mzuri. Kiranga ni mmoja wa binadam wengi ambao sayansi imewafunga milango ya udadisi juu ya mambo ambayo yanaonekana ya kawaida lakini sayansi haiyajui.
Anajua kwamba Upendo upo. Anajua kwamba busara IPO,anajua kwamba huruma IPO na vingi vinavyofanana na hivyo lakini kwa kuwa hakuna maabara ya kuvipima na sayansi imezima kitengo cha kutafakari na kujitafakari amebakia kukariri Kama kasuku...
He need laws to proves that "he is perfect "
Narudia tena kwamba Mungu anaumba kwa maamuzi yake atakavyo,haumbi kwa kuamuliwa na upendo, kwahiyo angetaka kuumba ulimwengu wenye starehe tu mwanzo mwisho usio na mabaya asingeshindwa. Ila lengo la kutuwekea maisha haya unayoyaona, ni ili atakayefaulu mitihani yake basi amemwaandalia maisha mazuri zaidi.
Sasa kuhoji kwanini asingeumba ulimwengu usio na maovu, jibu hakutaka hivyo angetaka angefanya.
Halafu Mwenyewe unasema kabisa kuwa kwa sababu ya Upendo wake "alikuwa na uwezo(sio lazima) wa kuumba ulimwengu usio na maovu" lakini nashangaa unakuja kudai kuwa anajipinga!
Na Mungu ana sifa nyingi tu. anaupendo na pia anauvumilivu na zengine nyingi .
Mbona vingi tu Visivyoonekana vina sifa za kupewa Majina ya namna mbali mbali?
We kifo unakiona? Mbona kina Jina?
We Busara (intelligence) unaiona?
Mbona unaipa majina tofauti?
Ile force of gravity Unaiona?
Mbona unaipa jina na kuidadavua kwa kirefu.
they can't be seen neither they can't be touched but they can be felt,experienced hence they can be proven.
Hii haijakaa sawa kwa nn atupe mtihani wakati anajua kila kitu kijacho?,nn maana ya mungu kumpa mwanadam mtihani?,hivi umefikiri kabla ya kuandika,?,kwa hiyo mungu akitupa mtihani maana yake ni kwamba hata yeye hajui mambo yajayo!,na ndo mana utasikia kauli kama eti mungu akaghadhabika mara eti hasira ya mungu ikawaka juu yao?,kwel huyu mungu anajua yajayo?,
Umejibiwa Sana,Bahati mbaya majibu hayafanani na ulichokaririshwa ndiyo sababu huyataki ?
Hata ukiulizwa ni nini kimekufanya ugundue kwamba ni uwezo wote na Upendo wote pekee kinachofanya Mungu afikie au asifikie uamuzi wa kuumba aina ya ulimwengu ambao umejikaririshwa kwamba ndiyo bora ?
Huna majibu baridi unarejea kwenye default position yako....
Angeweza kuumba na kufanyabinadam wote wawe sawa misukule au wawe wanakariri pasipo kufikiri Kama wewe
Umahiri wa busara za mtu huonekana pale anapojadili na watu ktk mada tofauti.
Nadhani wewe hauko hapa Kuelewa bali ni kuleta ubishi usiokuwa na Tija na kupoteza muda wako na wangu.
Unarudia maneno km matangazo ya vifo. Hali ukitambua kuwa km ungeamua Kufikiri kidogo usingefanya hivyo. Na mada hii isingekuwa na mlolongo mrefu namna hii bila sababu za msingi.
Nadhani kwa mtu mwenye busara itakuwa si jambo la busara kuendelea Kujadili na wewe manake Umeziba njia zote za Uelewi.
Nakusikitia sana kiranga Kwa kumkana MUNGU aliyekupa nafasi ya kuuona Utukufu wake uliokuzunguka.
Ni masikitiko kuona kwamba Mpaka leo hii 2015 kuna baadhi ya binaadamu wanakubali kabisa kuwa wao wako hapa duniani na kila kitu kinachowazunguka vyote vimekuwepo hapa kwa BAHATI NASIBU (Chance).
Nakutakia mjadala mwema.
Mkuu;pole Sana. Kiranga hafundishiki lakini huwa tunamtumia Kama ubao wa kufundishia wengine.
Katika hilo anafaa Sana.
Tusimwache aendelee kumwaga uchafu wake ambao waweza kuharibu watu wengine wasio na uelewa mzuri. Kiranga ni mmoja wa binadam wengi ambao sayansi imewafunga milango ya udadisi juu ya mambo ambayo yanaonekana ya kawaida lakini sayansi haiyajui.
Anajua kwamba Upendo upo. Anajua kwamba busara IPO,anajua kwamba huruma IPO na vingi vinavyofanana na hivyo lakini kwa kuwa hakuna maabara ya kuvipima na sayansi imezima kitengo cha kutafakari na kujitafakari amebakia kukariri Kama kasuku...
Nimekuelewa mkuu.
Tatizo SIO sayandi hatta kidogo.
Tatizo ni weledi wa wadau humu jukwaani.
Hakuna ktk historia ya mwanadamu Ukakuta mtu anafundisha wanafunzi wa shulr ya msingi masomo ya chuo kikuu!
!Kiranga anataka kujifunza MUNGU ni nani hali ya kuwa Vitu vilivyoko mbele ya macho yake Amekubali Kuwa HAVIJUI.
Unamwambia Kiranga ajifunze basic kwanza Kabla ya kukimbilia huko kwenye kumjua KING OF KINGS anakujibu kuwa "hata km hivyo vitu sivijui hio haimaanishi kuwa MUNGU YUPO!
Sasa hapo ndipo unapoona kuwa Huyu hayuki hapa kuelewa bali kupoteza wakati tu.
Na sisi wengine Wakati kidogo ni muhimu sana kwetu.
Ndio nikamtakia Mjadala mwema kwa wenye wakati mwingi wa Kupoteza km yeye.
Contradiction si jibu, ni swali.
Kusema "mungu kaamua hivyo" si jibu.
Ni kukubali kwamba hujui kwa nini kafanya hivyo na kwa hiyo hujui jibu.
Jibi gani lingine nililopewa?
Hujathibitisha kwamba mungu yupo.
Thibitisha, au kubali kwamba huwezi
Hivi hauna maswali mapya?
Hebu toa mfano wa aina la jibu ambalo unaitaji kujibiwa.ili tuone ni wapi tunapokosea.
Hii haijakaa sawa kwa nn atupe mtihani wakati anajua kila kitu kijacho?,nn maana ya mungu kumpa mwanadam mtihani?,hivi umefikiri kabla ya kuandika,?,kwa hiyo mungu akitupa mtihani maana yake ni kwamba hata yeye hajui mambo yajayo!,na ndo mana utasikia kauli kama eti mungu akaghadhabika mara eti hasira ya mungu ikawaka juu yao?,kwel huyu mungu anajua yajayo?,
Swali jipya hujapanda daraja la kupewa mpaka ujibu hili.
Aina ya jibu nipe wewe unayeamini mungu yupo.
Wenye kujua angalau kidogo washakubali kwamba hawajui ni kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya, mateso na maovu yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya, mateso na maovu hayawezekani.
Wamelikwepa swali la kwa nini mungu kaumba hivyo kwa kusema mungu anaamua anachotaka mwenyewe na sisi hatuna haki ya kuuliza kwa nini.
Hili si jibu muafaka, ni kukwepa kujibu muafaka.
Na kwa vile hawajui kwa nini mungu kaumba hivyo, hawamjui mungu huyo.
Wanaamini tu kitu wasichokielewa.
Na kwa vile wanaamini kitu wasichokielewa, wanaweza kuwa wanaamini kitu kisichopo.
Hususan kwa sababu nimeuliza pia kama kuna mtu anaweza kuthibitisha uwepo wa mungu sijajibiwa.
Maswali haya yakishindwa kujibiwa mpaka sasa mnanipa kila sababu ya kuendelea kusema kwamba huyo mungu mnayemuamini, mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, hayupo, ni wa kutunga tu.
Ndiyo maana anashindwa ku pass basic logical consistency tests.
Hebu toa mfano wa aina la jibu
ambalo unaitaji kujibiwa.ili tuone ni
wapi tunapokosea.
Kama kweli unaelewa unachokielewa basi tupe mfano wa aina ya jibu ambalo tunapaswa kulijibu.
they can't be seen neither they can't be touched but they can be felt,experienced hence they can be proven.
Jibu la mtu mwenye kufikiri, kama hajui, ni kusema hajui na kushukuru kwa mchango wangu katika kumpa yeye changamoto ya kuifikiria tena imani yake.
How could you resolve the contradiction?
Hehe..sasa kama hata wewe mwenyewe kutunga mfano wa jibu la swali ulilouliza mwenyewe huwezi, ni wazi kabisa hata hilo swali unaloliuliza hulielewa, kama swali unaloliuliza hulielewi pia huwezi kuwa na ubavu wa kujua lipi ni jibu sahihi na lipi si sahihi.
Mimi bado nataka unipe mfano wa aina ya jibu unalotaka kutokana na swali lako ambalo unadai tumeshindwa kujibu,maana nilichokigundua inaonekana hata swali unaloliuliza we mwenyewe hulielewi.
Hawa watu wengine hata hawaelewi ninachouliza hapa.
Sijauliza kupewa picha ya mungu.
Sijauliza kupewa sauti ya mungu.
Sijauliza kupewa harufu ya mungu.
Sijauliza kuletewa mungu nimshike.
Sijauliza kuletewa mungu nimuonje.
Hiyo ni milango mitano ya fahamu.
Nimeuliza swali la kutumia mlango wa sita, akili.
Swali langu limejikita katika logical consistency.
Kama mungu yupo, anajua yote, anaweza yote, ana upendo wote kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati ana uwezo na upendo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
Sijajibiwa swali hili.
Halafu mtu anakuja na habari chovu kwamba kuna vitu vipo lakini havionekani, kama vile mimi nimeuliza kuonyeshwa picha ya mungu!
Hawa watu wengine hata hawaelewi ninachouliza hapa.
Sijauliza kupewa picha ya mungu.
Sijauliza kupewa sauti ya mungu.
Sijauliza kupewa harufu ya mungu.
Sijauliza kuletewa mungu nimshike.
Sijauliza kuletewa mungu nimuonje.
Hiyo ni milango mitano ya fahamu.
Nimeuliza swali la kutumia mlango wa sita, akili.
Swali langu limejikita katika logical consistency.
Kama mungu yupo, anajua yote, anaweza yote, ana upendo wote kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati ana uwezo na upendo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
Sijajibiwa swali hili.
Halafu mtu anakuja na habari chovu kwamba kuna vitu vipo lakini havionekani, kama vile mimi nimeuliza kuonyeshwa picha ya mungu!