Iris season 5 imeshatoka ?

Iris season 5 imeshatoka ?

tafuta Series inaitwa Hostage .
.
Pretty-Little-Liars-hd-wallpapers.jpg

.
Ngoja nimalizane na hii apa PRETTY LITTLE LIARS!!
.
 
Mbona hazina huo utofauti mkuu wangu? Tatizo ni kwamba hizi series kama unanunua Bongo ni full uchakachuzi hadi maudhi. Kwanza IRIS mwisho ni Season 2, Season I ilitoka 2009 or 2010 wakati Season II imetoka 2014. TZ wamechakachua na kufanya IV Seasons badala ya II.

So, ikiwa ya kwako uchakachuzi ulikuwa too much basi inawezekana ndio maana unaona kama zipo tofauti...nilishaacha kununua series za kariakoo baada ya kununua Series ya 24 ikiwa na only 1 episode badala ya 24!

Nakubaliana na wewe kabisa, mimi nijuavyo Athena haijatoka season 2 ila wabongo wanachakachua mnooo, hata Iris nijuavyo mimi imeishia season 2.
 
Nakubaliana na wewe kabisa, mimi nijuavyo Athena haijatoka season 2 ila wabongo wanachakachua mnooo, hata Iris nijuavyo mimi imeishia season 2.
You're RIGHT! Hata Athena nayo, kuna Seaon I pekee ingawaje kibongobongo kuna I&II. Niliacha kununua CD za Kariakoo pale nilipokuta Prison Break wametoa hadi Season XI....
 
Wahusika wa season 1 walobakia ni baek san na mr
Black tu

Daaaah.........tangu nihamie usukumani(Mwanza) hata hzo dzain za kariakoo sizipati. Naitafuta sana ATHENA episode13 ambayo kibongo ni seasonII. Msaada kwa aliye Mwanza kama naweza pata movies za season za ukweli.
 
Wahusika wa season 1 walobakia ni baek san na mr
Black tu
Na kama umefatilia vizuri tokea episode ya kwanza Sterling ni Baek san na Mr Black sababu ile ya kwanza Mr. Black hakuonekana kabisa sura yake ila sauti yake ilikuwa inasikika season 2 ndo ilipoishia hizo 3&4 zilipaswa kuwa season 2 hata mimi nilishawahi lizwa mwenge
 
Sasa kwa nini wahusika wa season 1 wengi hawapo katka season 2 harafu bung'o boy kasema ktk season 2 wahusika walikuwepo season 1 ni mr black na baek san lakin amemsahau yule babu mwanasayansi wa NSS mwenye kipara kama comedi comedi vile. Nilitegemea season two ningemuona mchumba wa kim hyu juan ambaye naye ni ex-agent wa NSS na reaction yake baada ya mchumba wake kuuawa ila wameishia kumuonyesha pale juu ya tower na mchezo ukaishia hapo. Lakini hawa jamaa series zao wanajitahidi sana zinasisimua.
 
ila mnaweza download kw akutumia pc,kuna app kwa ajili ya kudownload muvies za kikorea,inaitwa drama 5,
au ngoja ntafte linki yake ila humu kuna thread kabisa kuhusu iyo kitu
 
Unaponunua IRIS mtu unatakiwa kuwa makini sana! Kimsingi, IRIS ipo Season 1 na 2 pekee; sema wabongo wamechakachua na kwamba ile season 1, wametoa 1&2, na seaosn 2(ambayo imetoka mwaka jana) wameifanya 3&4! So, suala la Season 5, itabidi msahau kidogo manake jamaa wapo slow sana katika kutoa hizi series! Don't forget, Season 1 ilitoka 2010 na season 2 ndo kwanza ikatoka mwaka jana!

Kuhusu Athena, bado ipo season ile ile ya kwanza (2011) ambayo hata hivyo wabongo wameifanya season 1&2. Kwa kuwa IRIS 2 imetoka mwakajana, probably Athena 2 nayo ikaja mwaka huu!

But all in all, ogopa kununua zile DVD ambzo makasha yake ni mafupi...ni full magumashi!!
Asante kwa ushauri. Bongo nimeona yadi season 4 na bado haijaisha. Sasa wapi tutapata hiyo unayosema yaani 1 na 2 zikiwa hazijachakachuliwa
 
Asante kwa ushauri. Bongo nimeona yadi season 4 na bado haijaisha. Sasa wapi tutapata hiyo unayosema yaani 1 na 2 zikiwa hazijachakachuliwa
Mkuu, hakuna namna ya haraka zaidi ya ku-download. Kwanza, download µtorrent, link hii hapa: Downloads - ?Torrent® (uTorrent) - a (very) tiny BitTorrent client. Then, download IRIS 2 kupitia hii link: http://kickass.to/iris-2-2013-complete-series-t8224887.html

NB: Sina uhakika kama ina English subtitles. Just download it, kama haina subtitles, let me know na nitakuelekeza jinsi ya kuingiza subtitles. Kama unakaa eneo zuri, kifurushi cha 1000 kinatosha kabisa ku-download hiyo series ambayo ukuwa wake ni 3.64 GB.

Enjoy the show.
 
Jama mtoa mada kaulizia IRIS 5 Imeshatoka au bado. Nami naitaka hiyo,tujibuni!
 
Acha Uongo! hebu tazama hii short trailer afu urudie kuandika huo utu..mbo wako!

USITUKARIRISHE!

NGOJA nikuulize... lengo la post yako ni kuonesha jinsi ulivyo mjuzi wa maneno machafu na ya hovyo, au? Unachosema uongo ni kipi? Ni kwamba IRIS imetoka hadi Season 2 na Athena kuna Season 1, au unachobisha hadi unaongea maneno ya hovyo ni nini? Au unamaanisha si kweli kwamba kibongo bongo wamechakachua to the point kuna Iris 1 hadi 4 na ile Athena kuna season ya kwanza na ya pili?? Where's your point? Au ilikuwa ni njia ya kunionesha hiyo video yako? Kama ndivyo, then am sorry coz' sina muda wa kuangalia hiyo video yako.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom