Iringa Mjini kitimoto inatafunwa ni balaa

Iringa Mjini kitimoto inatafunwa ni balaa

Nyama ya nguruwe aka Kitimoto inauzika na kuliwa Iringa mjini sijawahi kuona. Karibu na ofisi ya CCM Mkoa kuna mabanda mengi sana zaidi ya 100 yanauza na kukaanga nyama ya kitimoto kila siku kuanzia asubuhi mpaka usiku wa manane, na nyama inaisha aisee.

Unakuta bar moja imezungukwa na majiko mpaka 8 ya kitimoto, unakula lager, unatafuna mdudu kiroho safi kabisa , ukitaka na ugali au ndizi ni wewe tu.

Moshi, Arusha hawawafikii waHehe kwa kutafuna kitimoto aisee, siyo mbwa tena kama zamani.

Wanaikaanga vyema sana, makachumbari kama yote.

Na hali ya hewa ya Iringa ni kama imechujwa hivyo bia zinatembea tu.

Heko Iringa, watoto wa Mkwawa.
Ndio maana Iringa haina Waislam KABISA
 
Nguruwe ndio nyama salama kwa matumizi ya kila siku. Wenye kuipiga vita shauri lao. Hatuna cha minyoo wala nini tunakulaaa.
 
Wanyalukolo binti yetu huyu
Screenshot_20220619-193019.jpg
 
Hata mgeta, morogoro kiti moto kingi
Tatizo upishi tu

Ova
 
Huku TUKUYU kilo ni 7k unapata na ndizi mbili kwa kila mlaji wa hiyo kilo moja ila kama utakua alone utapewa ndizi 6 ukiwa na option ya kuongeza 4 kama hazijakutosha plus parachichi,kachumbari na mchicha.
Mwisho wa ofa ni ndizi kumi kwa kilo moja zaidi ya hapo itabidi ulipie jero kwa kila ndizi 3
Naona sasa unatuletea shida wengine. Maana hatuchelewi kuchoma naul kutok dar kuifuata hyo offer
 
Ndio maana Iringa haina Waislam KABISA
Kitimoto kinapendwa kinoma, kuna kipindi zilikuwepo sosage za kitimoto tamu kinoma kuliko sosage za aina yoyote ile, na iringa wachinjaji nguruwe iringa waislam wapo sasa sijui ni majina tu ila sio waislam coz unakuta mtu jina lake abdul ila anachinja kitimoto balaa 😂😂😂🤣🤣🤣
 
Kitimoto ya Iringa sili. Wahehe watakosa kuongeza finyanga mbili tatu za ile mboga ya nyumbani 🐶kweli?
 
Naona sasa unatuletea shida wengine. Maana hatuchelewi kuchoma naul kutok dar kuifuata hyo offer
tena ukijitambulisha kuwa umetoka DSM utapatiwa na Mikungu ya ndizi za kuiva na maparachichi kama zawadi kwa familia yako
 
Back
Top Bottom