Iringa: Basi la New Force la Mbeya - Dar, lapata ajali mlima Kitonga

Iringa: Basi la New Force la Mbeya - Dar, lapata ajali mlima Kitonga

Tuafanye utafiti wa ajali zinazotokea sasa je zina uhusiano nA mabasi au malori ya sasa naya zamani.

Zamani tulikuwa na Scania sasa utong
 
Watu kadhaa wamenusurika kifo katika Mlima Kitonga Mkoani Iringa baada ya basi la kampuni ya New Force lililokuwa likitokea Mbeya kuelekea Dar es Salaam kugongana na gari nyingine linalodaiwa kuwa ni la Kampuni ya Golden deer lilokuwa likitokea Dar kwenda Tunduma na kisha kuanguka chini ya mlima huo wenye mteremko mkali.

Kaimu Kamanda Polisi wa mkoa wa Iringa, Deusdedit Kashindo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa taarifa za awali zinasema kuna majeruhi tu.
 
Hizi new force sipandi yaan juzi tu zimegonga na leo nyingine ínaanğuka
 
Hawa madereva wa haya mabasi wanakimbia Sana!!
Na wanahonga trafiki wakipigwa kamera.
Akiwa anaendesha kile Cha spidi kinapiga kelele Sana lakini hawajali. Mwaka huu mwanzoni nilipanda nikaapa kutorudia tena.
Sitaki mabasi ya kukimbizana barabarani
 
Back
Top Bottom