Ipo siku yaja Buguruni itawaka moto utakaoshitua ulimwengu. Amini hilo

DON YRN

JF-Expert Member
Jan 14, 2019
474
999
Pale Buguruni darajani kuna mchezo unaofanyika ni hatari sana kwa maisha ya watu kuliko maelezo.
Kuna siku kadhaa nimekuwa nikishuhudia vijana wako pale Buguruni darajani wakifungua koki za malori ya mafuta na kujaza kwenye mifuko ya nylon kwa kushirikiana na madereva.

Iko hivi; Lori la mafuta likifika pale darajani(njia ya kutokea Ubungo kwenda mjini) likiwa linasubiri foleni ya mataa, kuna vijana huwa wanatokea na kufungua koki ya tank kisha hukinga na kujaza mafuta kwenye mifuko ya nylon kwa ruhusa ya dereva kisha baada ya mataa kuruhusu mchezo unaisha, linasubiriwa lori la mafuta litakalosimama usawa wa daraja. Na hali hii huendelea hadi siku inaisha.

Cha kusikitisha ni kwamba huu mchezo unafanyika kwenye foleni ya magari mengi zikiwemo daladala za abiria, magari binafsi, n.k. Je!, yakitokea km yale ya Morogoro tutalaumu nani km tunashindwa kuchukua hatua na tahadhari mapema?.

Mbaya zaidi, Polisi na viongozi mbalimbali wanaona mchezo huu ukiwa unafanyika.

Anyway, naamini mm siyo wa kwanza kuona hili jambo kwa watu wote tuliomo humu.
 
Ambacho hujui ni kwamba yale malorry yanakuwa yapo EMPTY, wanachokinga ni yale matone ya mwisho mwisho , wanafanya hivyo kwa malorry mengi hadi Rambo linajaa.
Kwa kumalizia mkumbushe atuambie huo moto utawakaje buguruni nzima maana amesahau, sio mbaya akitusimulia madereva wanaoruhusu wananufaikaje ikiwa foleni ikitembea hawana fursa ya kumwona mkingaji. Ahsante.
 
Wanakusanya kikipatikana kidumu anauziwa mtu wa daladala.....wengine hadi dereva wa lori anakua kwenye chain akishapeleka gari la watu anaibuka kijiwe nae anapata chake maisha yanaenda..........huo mchezo hio njia ni wa muda mrefu sana hasa hayo maeneo, labda wameshakua wabobezi wa kazi, akitokea mjukuu mmoja siku akasahau miiko ya kazi akachomoa betri habari kwisha
 
Pale buguruni darajani kuna mchezo unaofanyika ni hatari sana kwa maisha ya watu kuliko maelezo.
Kuna siku kadhaa nimekuwa nikishuhudia vijana wako pale buguruni darajani wakifungua koki za malori ya mafuta na kujaza kwenye mifuko ya nylon kwa kushirikiana na madereva.
Iko hivi; Lori la mafuta likifika pale darajani(njia ya kutokea ubungo kwenda mjini) likiwa linasubiri foleni ya mataa, kuna vijana huwa wanatokea na kufungua koki ya tank kisha hukinga na kujaza mafuta kwenye mifuko ya nylon kwa ruhusa ya dereva kisha baada ya mataa kuruhusu mchezo unaisha, linasubiriwa lori la mafuta litakalosimama usawa wa daraja. Na hali hii huendelea hadi siku inaisha.
Cha kusikitisha ni kwamba huu mchezo unafanyika kwenye foleni ya magari mengi zikiwemo daladala za abiria, magari binafsi, n.k. Je!, yakitokea km yale ya Morogoro tutalaumu nani km tunashindwa kuchukua hatua na tahadhari mapema?.
Mbaya zaidi, Polisi na viongozi mbalimbali wanaona mchezo huu ukiwa unafanyika.
Anyway, naamini mm siyo wa kwanza kuona hili jambo kwa watu wote tuliomo humu.
Ubarikiwe sana na hakika ipo siku utakumbukwa, kimya chetu kwenye mambo ya msingi ndio ishara ya makaburi tuliyochimba tukisubiri kufukiwa. Signs of life ending by a society, hayanihusu sawa ngoja tuone.
 
Ambacho hujui ni kwamba yale malorry yanakuwa yapo EMPTY, wanachokinga ni yale matone ya mwisho mwisho , wanafanya hivyo kwa malorry mengi hadi Rambo linajaa.
Hamna kitu km hicho, nilishawahi kupeleleza hii kitu ndg. Kunakuwa na mafuta tena full tank.
Hebu nambie, ni matone gani yanajaza hata lita 10 kwa muda wa dk 5?
 
mtoa mada hakufahamu kuwa madereva hawahusiki na hao wafunguwa koki. mimi ni dereva ukweli hao jamaa huwezi kuwazuia ukiwazuia wanakuvunjia koki zote na huwezi kuwafanya kitu maana wanakimbia na sisi tunakuwa bize na foleni . tatizo lipo kwa askari wetu wanaona na hawafanyi chochote. ni kweli moto unaweza kutokea ikiwa itatokea shoti au cheche za moto inaweza kusababisha mfunguwa koki kuungua na gari pia kuungua, hii ndio nchi yetu mpaka ajali itokee ndio wajipange
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom