Ipi top 3 yako ya nyama tamu?

salam!!!
wale wazee wa misosi ipi top 3 yako ya nyama tamu
ya kwangu hiyapa

1. Kuku
Asee huyu ndege hadi leo binafsi naona nyama yake haina mpinzani yani hana mbadala yani nyama iwe mchemsho rosti choma au ya kukaanga nitamu zote nadhani sote tunafahamu jinsi supu ya kuku ilivyo tamu

2. Ng'ombe
Akitoka kuku anafata ng'ombe huyu myama nae yupo vizuri lakini huyu utamu wa nyama yake una depend na maufundi ya mpishi. laini na yeye nyama yake iwe mchemsho rosti choma au ya kukaanga nitamu zote

3 Kitimoto
kwangu huyu namba yake inashika namba 3 kwasababu tu nyama yake inanoga tu kwa rosti na kukaanga lakini mchemsho wake hahaha hapana asee

hiyo ndo top 3 yangu ya nyama tamu Je ya kwako ni ipi?

NB: Kuku anautamu wa asili tu yeye haitaji ata ufundi wa mpishi....
1 Kondoo choma
2. Mbuzi choma na Ka red wine
 
Back
Top Bottom