Ipi siri ya shetani kuwa mjanja sana?

Ipi siri ya shetani kuwa mjanja sana?

KISIWAGA

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
8,021
Reaction score
16,599
Nimejaribu kuipitia pitia biblia na kusikiliza sikiliza mahubiri ya wahubiri wetu hawa

Nimegundua kitu,shetani eiza ni mjanja sana ama amezungukwa na team ya wajanja sana maana kwa jinsi dunia ilivyo sasa huwezi kuishi bila angalau kudokoa chochote kitu kutoka kwa huyu kiumbe shetani

Hebu fikiria watoto wa nabii fulani wanasoma shule fulani ambayo kwenye mtaala wake wa history wameandika bila aibu kuwa binadamu tunayemuona sasa zamani alikuwa ni sokwe

Fikiri tena ile zahanati anayotibiwa mchungaji fulani ilijengwa kutokana na kodi ya bia & vileo vikali

Naona mbele yangu kuna ustadh mmoja anapita amevaa jezi ya simba yenye tangazo la sportpesa, hivi kamali sio dhambi kweli

Shikamoo shetani aliyekuumba alikuwa fundi kwelikweli sasa kama wewe uko hivi sijui aliekuumba ana akili kiasi gani



Mungu fundi
 
Hahahahaa mimi huwa nashangaa Walokole wanaanza kumkandia shetani kwenye maombezi yao yaani utakuta jitu vivu halina kazi linaamini shetani ndio anamfunga asifanikiwe
Hua nacheka na kusema

Hiiiii bha ghoshaaaaa
Yaani Shetani alivyo tajiri na anamiliki dunia leo aanze kumzuia maskini wa akili na mali et asipate hata hela ya kula hayo ni zaidi ya maajabu!

Walokole hawajui wanapigana vita ambavyo haviwahusu yaani wao wameamua kuwa machawa wa Mungu kwenye bifu la shetani na Mungu ambalo hata haliwahusu na inaonesha ni jinsi gani walivyo mapunguani
Ila ukija kwa Wafuasi wa shetani wao wapo normal hata hawana ugomvi na mtu yeyote hua wanatoa ushirikiano kote kote tu wanaweza watoe utajiri waliopewa na shetani kusaidia watu wa mungu bila hata kinyongo na kwele
Ila sasa watu wa mungu wana ujuaji mwingi na kujiona special sana kuwatenga wenzao wa upande wa pili na hapo wakipata shida wakipewa msaada hawakatai!

Anyway huo ni mtazamo wangu mimi sipo upande wowote ule!
 
In the Devil Kingdom;

Ramsey: Uwezo wa Mungu una kikomo?
Kanumba: Hapana, uwezo wa Mungu hauna kikomo
Ramsey: Kama uwezo wake hauna kikomo je unaamini Mungu anaweza kuumba kiumbe chenye nguvu zaidi yake (akimaanisha shetani)
Kanumba: aa aa aah(akijiumauma) hapana hawezi
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Back
Top Bottom