Inategemea na company gani na simu yako ilianza na android ngap.
Kwa samsung a series na m zote zinapata 2 years of OS updates. Ina maana kma simu yako ilikuja na android 9 itapata 10 na 11.
Kwa samsung za S series, Fold, flip, na Note series zinapata 3 years kunanzia s10/note 10. Kwa mfano s10 ilikuja na android 9, ikaenda 10 na inatakiwa kupata 11 na 12 huko mbeleni (miaka mi3)
Kwa simu za google zote nazo ni miaka mi3
Nokia, Motorola, Xiaomi, Oppo ni miaka mi2
Brand nyingi zinafanya miaka mi3 kwa flagship zao na miaka mi2 kwa simu za bei ya kawaida mpk chini
Akina Tecno, Infinix na itel wao kwakweli sahau kuhusu kupanda android version. Watakupa security updates basi. Simu chache sana za tecno zinapandishwa android version sikuhz na mara nyingi inakua ni moja tu.
Kwa huku bongo ukitaka simu ya bei rahisi itakayopanda android version huko mbeleni ni Nokia, Xiaomi na Samsung A series
Sent from my Pixel 3a using
JamiiForums mobile app