iPhone 15 imetambulishwa tujiandae na msiba

iPhone 15 imetambulishwa tujiandae na msiba

iPhone 12 ni kama iPhone 11s
iPhone 14 ni kama iPhone 13s
iPhone 15 ndio italeta major changes kwenye design.

Refer 5 & 5s, 6 & 6s, 7 & 8, X & Xs.

Maono yangu tu.
Mi ngoja nitulie kwa samsung tu, jamaa wako vizuri camera kali, storage kubwa, battery capacity 5000mAh inakaa na chaj had unasahau kuuliza kama umeme upo.
Watu wanaokimbizana na matoleo ya iPhone wanakazi ngum sana maana matoleo mengi hayana mabadiliko makubwa zaidi ya kubadilishwa muonekano
 
Mi ngoja nitulie kwa samsungu tu, jamaa wako vizuri camera kali, storage kubwa, battery capacity 5000mAh inakaa na chaj had unasahau kuuliza kama umeme upo.
Watu wanaokimbizana na matoleo ya iPhone wanakazi ngum sana maana matoleo mengi hayana mabadiliko makubwa zaidi ya kubadilishwa muonekano
Watasema tutafute hela, Samsung ni calculator sio simu.

Hapa najichanga nidake S20 au 21 au zile Note. Ile screen ya izo simu ni next level aisee
 
Mtakoma
JamiiForums-1145621062.jpeg
 
😅😅😅 nishatoka huko kwenye simu za daraja la juu.. sasa hivi naishi na simu za mitumba za mafungu.. kazi ya simu ni kupiga, pokea, tume message na kupokea basi
Kukimbizana na izi vitu utajiona masikini bure. Utapeleka iPhone 14 Pro yako Makumbusho kutop up watasema ongezea Mil 1.5 upewe 15 Pro Max. Hapo ndio utapojiuliza value ya simu yako ni tsh ngp?
 
Kukimbizana na izi vitu utajiona masikini bure. Utapeleka iPhone 14 Pro yako Makumbusho kutop up watasema ongezea Mil 1.5 upewe 15 Pro Max. Hapo ndio utapojiuliza value ya simu yako ni tsh ngp?
Bana wee, haya mambo yanaenda na upenzi wa tech, sababu, na hela... Sie tunaona shida kwasababu tu reason sanaa mkuu.. tunachambua sana hadi unaona ulicho nacho kinatoshaa.. mfano RR ya mwaka 2023 utalinganisha na RR 2015 ... Ulaya waweke mashart simu ziwe zinatolewa matoleo kila baada ya miaka mitatu hivi wanakwiba hela za watu
 
🤣🤣🤣hili nalo neno
Usifanye biashara ya topup ata siku moja. Ni biashara ya kifala haujawahi tokea.

Niliyaka iPhone 11 nikaenda na 8 plain yangu. Wakasema iPhone 11 plain Mil 1 hivi nikasema nikiweka 8 je? Wakakagua wee wakasema nitaongezea 850k. Kwahiyo iPhone 8 yangu ni Laki 1 na Nusu.

Nikasema sawa ngoja nikajipange. Nikamcheki mshikaji wangu nikamwambia akasema nipe namba yao, akawapigia, akasema anaomba used iPhone 8, nyeusi, GB64 battery health kuanzia 90%. Yaani kila kitu kama ile 8 yangu. Wajamaa wakamwambia 450k. Akawaambia anakuja dukani kuicheki sahivi.

Dakika 5 hazijaisha, wananipigia simu wananiambia vipi kwahiyo deal ya top up? Yaani wananibembeleza kabisa.

Kumbe wanataka kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Mi wanipige. Na wamuuzie mtu tena iPhone 8 yangu walionunua kwa 150k waiuze 450k.

Hii biashara ya topup ni bora uuze simu separately, kisha uongeze hela ukanunue simu mwenyewe.
 
Bana wee, haya mambo yanaenda na upenzi wa tech, sababu, na hela... Sie tunaona shida kwasababu tu reason sanaa mkuu.. tunachambua sana hadi unaona ulicho nacho kinatoshaa.. mfano RR ya mwaka 2023 utalinganisha na RR 2015 ... Ulaya waweke mashart simu ziwe zinatolewa matoleo kila baada ya miaka mitatu hivi wanakwiba hela za watu
Sure. Waweke tu vigezo aisee. Kama wameweza kuforce jamaa wameweka charger Type C kama Samsung watashindwaje iyo.

Ingawa kwa wenzetu nasikia simu wengi hawanunui cash, wanakua wanakatwa kidogo kidogo mfano unaingia mkopo wa mwaka mmoja kila mwezi unakatwa Laki na Nusu hadi mwaka unaisha umeshalipia 1.8m simu inatoka nyingine unaingia tena Mkopo ile nyingine unaiuza.
 
Sure. Waweke tu vigezo aisee. Kama wameweza kuforce jamaa wameweka charger Type C kama Samsung watashindwaje iyo.

Ingawa kwa wenzetu nasikia simu wengi hawanunui cash, wanakua wanakatwa kidogo kidogo mfano unaingia mkopo wa mwaka mmoja kila mwezi unakatwa Laki na Nusu hadi mwaka unaisha umeshalipia 1.8m simu inatoka nyingine unaingia tena Mkopo ile nyingine unaiuza.
Kwa simu waweke mashart, ni wizi wa mchana kweupe.. wawe wanatoa matolea mapya kila baada ya miaka miwili au mitatu haijalishi mtindo wa ulipaji wake.. ni kupigwa tu.. hapa Pixel 8 Pro wanatoa, watafatana hadi samsung.. tofauti ni ndogo sana.. walete simu inayopima ukimwi papo hapo.. hiyo itakuwa ina jipyaa 😅😅
 
Back
Top Bottom