INTARAHAMWE WA Prof.LIPUMBA

Kwa matamshi aliyotoa Lipumba anaanza kukosa sifa za Kitaifa!
Sana sana anamsarandia Lissu, amejidowngrade kweli kweli.

Kawaida ukisema Kweli wenye nguvu watagengeza mazingira ili uonekane muongo, mbaya. Kama unakumbuka An enemy of the people. Viongozi wenye mamlaka Wanatake advantage ya ujinga wa watu.
 


Hivi wewe huoni hatari ya Lukuvi na baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo kupinga serikali tatu kwa sababu zanzibar itatawaliwa kiislam;hiyo ni kauli ya kuzungumzia kanisani? Hivi waislam wakianza kuhamaki na kuleta fujo nani atalaumiwa?Au hukusikia CCM wakisema Wapemba nyie ni waarabu hamna undugu na watanganyika?Lipumba afafanue nini tena.
Au CCM wanaposema Zanzibar itajiunga na OIC sio ahadi za kidini?
 
intera= fight/amua/do
hamwe= pamoja limetokana na neno imwe = moja, so maana kamili ya interahamwe ni fight together/do together.
 
Kwa ya elimu na exposure ya Lukuvi tunaweza kumwelewa, lakini kwa elimu na exposure ya Lipumba hatumwelewi.
 

Kati ya prof na yule alieenda kuleta siasa kanisani,yupi mchochezi?? Umepaniki
 
Nijuavyo mimi Intarahamwe ni kundi ambalo lilihusika ktk mauaji ya kimbari(genocide) kule Rwanda,
Ni nini kimemsukuma Prof.LIPUMBA kuwaita wajumbe bunge la katiba wanaounga mkono serikali 2 kuwa ni Intarahamwe?

hukuona maneno ya kibaguzi na ya kuchochea chuki kama yaliokuwa yakitolewa na interahamwe kutoka kwenye vinywa vya wajumbe waunga mkono serikali 2 ulikuwa wapi mkuu?
 

badala ya kulaumu walotoa kauli za ubaguzi unalaumu mkemeaji kweli vichwa vingine sio kwa ajili ya kufikiri ni vya kufugia nywele.
 
Lipumba ni ibilisi na adui mkubwa wa taifa hili amejenga chuki sana na kutamani kuzuka kwa mapigano miongoni mwa watanzania kwa kua amekua hakubaliki ktk siasa za Tanzania ndio maana limejivua utu limekua SHETANI adui mkubwa wa Tanzania,,kwa ivo hata lile neno lake la hatari alilolitamka bungeni la kuchochea mauaji si geni kwake ila sisi waTZ wapenda amani na utulivu tunathubutu kusema OLE WAKE.
 
Mzee unawapiga shule kweli..sijui km wataweza kujibu
 
Mipasho mipasho..toa hoja..mambo ya mvuto na nini hayahisiki kwenye katiba..ccm inawatu ambao mpo km mna akili za kuku
 
Nijuavyo mimi Intarahamwe ni kundi ambalo lilihusika ktk mauaji ya kimbari(genocide) kule Rwanda,
Ni nini kimemsukuma Prof.LIPUMBA kuwaita wajumbe bunge la katiba wanaounga mkono serikali 2 kuwa ni Intarahamwe?

Kwasababu hawaitakii mema Tanganyika.
 
Kwa jinsi CCM inavyokandamiza mwazo ya umma, nadhani kuitwa intrahammwe haitoshi. Tuwatafutie jina linalowafaa…labda wabakaji wa KATIBA? Pia ikumbukwe kuwa Nyerere siyo na hatakuwa Mungu, alikuwa mwanadamu aliyekosea na anapaswa kukosolewa pia. Vinginevyo mnaturudisha enzi za kidumu fikra za mwenyekiti…….
 
vipi na yule ambae alienda kanisani kuchochea udini unamzungumziaje!
 

Acha kupotosha maoni ya wananchi yapo katika kura ya maoni.
 
Mwache Lipumba kasema ukweli na wewe itakuchukua decade (miaka 10) kulijua hili kwasababu hutaki kumwelewa
 
Nawewe umekalilishwa kama wenzio ccm mfuata mkumbo!!
 
We pia intarahamwe kama asemavyo Lipumba umeshalishwa sumu ya ccm!!
 
Uelewa wa lipumba ni mdogo ukilinganisha elimu yake na vitendo vyake kwani hata ndani ya cuf ameshindwa kujenga demokrasia anayoihubiri majukwaani, yeye na maalim seif wanajiona kama vile cuf ni chama chao binafsi. Anafaa kupuuzwa!
 
Wewe hujielewe na ccm yako ndio open space za wananchi mmejimilikisha nakuziita ccm!!
Jalini wananchi kwanza na si chama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…