Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Zipo sababu nyingi zinazowafanya watu wawe na mahusiano ya nje ya mahusiano yao rasmi (kucheat). Tangu enzi na enzi mambo haya yamekuwa yakiwatokea wanaume na wanawake wa kila kabila, dini, lugha na mahali na kila mtu anayo sababu yake ya kumfanya hivyo. Japo wakati mwingine inaendana na hisia ya kujisikia vibaya lakini ukweli ni kwamba watu huamua na kuhalalisha kwa sababu ambazo ni wao wanazijua na vigumu watu wengine kuweza kuzielewa. Wengine wanafikiria ni suala la tamaa tu za kimwili lakini sayansi ya jamii yote inaonesha kuwa kuna mambo mengi zaidi ambayo yanaweza kusababisha mtu kuikubali itikadi ya infidelism. Hata hivyo hili siyo somo langu la leo.
Kuna watu wanaamini kabisa kuwa wanawake ndio 'cheaters' wazuri sana na kuwa wana uwezo wa kuweza kuwachanganya watu wawili au zaidi bila mhusika mkuu kuweza hata kushuku. Wengine, hata hivyo wanaamini kuwa ni wanaume ambao ni cheaters 'wazuri' kwani anaweza kuwa na mahawara kadhaa kwenye mji ule ule mmoja bila hata kushukiwa. Lakini wengine hudai kuwa wanawake huweza kushuku mapema kuwa mtu anacheat lakini huwa wanaamua kumezea as long as yule mtu anatimiza wajibu wake wote wa pale nyumbani.
Wapo wanaume hata hivyo ambao hawaamini kabisa kuwa mke/mtu wake anaweza kucheat kwani amejiaminisha kuwa mwanamke yule yuko hoi bina taaban (hasa kama ni mwanamme anayeamini sarakasi za chumbani kama kigezo). Lakini mwisho wa siku mjadala ambao hudumu mara nyingi ni yupi rahisi kukamatatika. Wapo wanaosema wanaume ni rahisi sana kukamatika kwani kucheat kwao ni sawa na kurusha rusha mipira mitatu angani (juggling) kiasi kwamba anaweza kurushwa kwa muda fulani tu mwisho wa siku atadondosha mmoja au yote (wengine hudai wanaodondoshwa ni mahawara!). Lakini wapo wanaoamini kuwa ni wanawake ambao wanaweza kushikika kirahisi kwa sababu wao wakianza kweli kucheat huwa wanahamisha kabisa hisia na majeshi yao kule kwingine kiasi kwamba hawawezi kujitoa kule kwingine na wakarudi nyumbani wakawa kama kawaida.
Kwa wale wataalamu (wenye uzoefu au waliowahi kujisomea dhana hii wakiwa vyuoni) msimamo upi unaelekeana na ukweli na ni kwanini hasa?
Kuna watu wanaamini kabisa kuwa wanawake ndio 'cheaters' wazuri sana na kuwa wana uwezo wa kuweza kuwachanganya watu wawili au zaidi bila mhusika mkuu kuweza hata kushuku. Wengine, hata hivyo wanaamini kuwa ni wanaume ambao ni cheaters 'wazuri' kwani anaweza kuwa na mahawara kadhaa kwenye mji ule ule mmoja bila hata kushukiwa. Lakini wengine hudai kuwa wanawake huweza kushuku mapema kuwa mtu anacheat lakini huwa wanaamua kumezea as long as yule mtu anatimiza wajibu wake wote wa pale nyumbani.
Wapo wanaume hata hivyo ambao hawaamini kabisa kuwa mke/mtu wake anaweza kucheat kwani amejiaminisha kuwa mwanamke yule yuko hoi bina taaban (hasa kama ni mwanamme anayeamini sarakasi za chumbani kama kigezo). Lakini mwisho wa siku mjadala ambao hudumu mara nyingi ni yupi rahisi kukamatatika. Wapo wanaosema wanaume ni rahisi sana kukamatika kwani kucheat kwao ni sawa na kurusha rusha mipira mitatu angani (juggling) kiasi kwamba anaweza kurushwa kwa muda fulani tu mwisho wa siku atadondosha mmoja au yote (wengine hudai wanaodondoshwa ni mahawara!). Lakini wapo wanaoamini kuwa ni wanawake ambao wanaweza kushikika kirahisi kwa sababu wao wakianza kweli kucheat huwa wanahamisha kabisa hisia na majeshi yao kule kwingine kiasi kwamba hawawezi kujitoa kule kwingine na wakarudi nyumbani wakawa kama kawaida.
Kwa wale wataalamu (wenye uzoefu au waliowahi kujisomea dhana hii wakiwa vyuoni) msimamo upi unaelekeana na ukweli na ni kwanini hasa?